Putin aahidi jibu 'kali' kwa ugaidi wa Ukraine

kimsboy

JF-Expert Member
Oct 17, 2016
8,991
17,888
Putin aahidi jibu 'kali' kwa ugaidi wa Ukraine

Oct 11, 2022 02:27 UTC

[https://media]

Iwapo Ukraine itapanga mashambulizi zaidi ya kigaidi dhidi ya Russia, kutakuwa na jibu kubwa la kijeshi sawa na lile lililotekelezwa Jumatatu.

Onyo hilo limetolewa na Rais wa Vladimir Putin wa Russia ambaye amethibitisha kwamba jeshi la nchi yake limefanya mashambulizi makubwa Jumatatu dhidi ya Ukraine kwa kutumia silaha za masafa marefu ambazo zimelenga vituo vya nishati na mawasiliano ya kijeshi vya Ukraine.

Shambulio hilo lilitokea siku mbili baada ya bomu kuharibu daraja la kimkakati la Crimea, ambalo Moscow imeliita shambulizi la kigaidi la Ukraine.

Rais Putin ameendelea kusema kuwa: "Iwapo kutakuwa na majaribio zaidi ya kufanya mashambulizi ya kigaidi katika ardhi yetu, Russia itajibu vikali na kwa kiwango kinacholingana na vitisho vilivyoibuliwa dhidi ya yake."

Kulingana na Waziri Mkuu wa Ukraine Denis Shmygal, Mapema Jumatatu, mikoa kadhaa ya Ukraine ilikumbwa na mashambulizi ya makombora, na miundombinu muhimu isiyopungua 11 iliharibiwa.

Rais Putin alisema kuwa Russia mashambulizi hayo ya kulipiza kisasi yamekuja baada ya majaribio kadhaa ya kuharibu miundombinu ya Russia ambayo yamehusishwa na Ukriane.

Rais Putin amessema miongoni mwa mambo mengine, Ukraine iliharibu sehemu ya mfumo wa kusambaza umeme wa kinu cha nyuklia cha Kursk na ilijaribu kuharibu bomba la gesi asilia la TurkStream linalosafirisha gesi asilia kutoka Russia hadi Uturuki. Aidha na Rais wa Russia amebaini kuwa Ukarine imehusishwa na mlipuko wa Jumamosi ulioharibu Daraja la Crimea.

[https://media]Hujuma ya kigaidi dhidi ya Daraja la Crimea

"Utawala wa Kiev umekuwa ukitumia mbinu za kigaidi kwa muda mrefu sana," rais wa Russia ameendelea kusema na kutaja mauaji ya watu mashuhuri, mashambulizi ya kiholela ya miji ya Donbass na Kiwanda cha Nyuklia cha Zaporozhye kuwa mifano ya vitendo kama hivyo.

"Kwa kweli, serikali ya Kiev imejiweka sawa na vikundi vya kigaidi vya kimataifa. Kuacha uhalifu kama huo bila jibu imekuwa haiwezekani," alisisitiza, kabla ya kuthibitisha kwamba Russia ilishambulia miundombinu ya Ukraine.

Mbali na kuilaumu Ukraine kwa mfululizo wa mashambulizi dhidi ya miundombinu ya Russia, Putin ameashiria kuvurugwa mabomba ya kusafirisha gesi ya Nord Stream. Alisema kuwa Russia inazuiwa na mataifa ya Ulaya kuchunguza hujuma hiyo na akasisitiza kuwa "sote tunamfahamu vyema mnufaika mkuu wa uhalifu huo."

Putin aliyasema hayo alipokuwa akiongoza kikao cha Baraza la Usalama la Taifa la Russia.

Mlipuko wa Jumamosi kwenye daraja la Crimea, kiungo muhimu kati ya peninsula hiyo Russia bara, uliua raia kadhaa na kuangusha sehemu ya daraja linalotumiwa na magari. Aleksandr Bastrykin, mkuu wa Kamati ya Uchunguzi ya Russia, aliripoti kwa Putin siku ya Jumapili kwamba Ukraine ndiyo iliyohusika na uhalifu huo, huku kiongozi huyo wa Russia akibaini kwamba "hakuna shaka" kuhusu hilo.
 
Ukraine kwenye daraja kaua 4 na Russia mabomu 100 kaua watu 13 samesame tu! Ukraine piiiga hao super power wa mchongo
Huruma ya Putin usiihesabu ni udhaifu.

Yeye alilenga miundo mbinu tu ya Ukraine. Hata hao 13 waliokufa ni kwa bahati mbaya tu.
Putin ni muungwana sana.

Akitaka kuua watu hata milioni anawaua tu kwa saa.

Tumia akili yako vizuri.
 
Akili zako zitumie vizuri!Nani amekwambia lengo la mashambulizi ya Urusi Jana ni kuua watu?Hujaona targets Ilikuwa miundombinu ya mawasiliano na umeme?
Unaacha kupambana frontline walipo wanaume unakuja kupiga uhani walipo wakina mama Na watoto huo si ni uchizi.
 
Huruma ya Putin usiihesabu ni udhaifu.

Yeye alilenga miundo mbinu tu ya Ukraine. Hata hao 13 waliokufa ni kwa bahati mbaya tu.
Putin ni muungwana sana.

Akitaka kuua watu hata milioni anawaua tu kwa saa.

Tumia akili yako vizuri.
Kuna watu ni vichwa vigumu kuelewa!Ila twende nao tu taratibu,kwenye bongo zao walishajiset Kwa namna ambayo haiwezekani akaona nyeupe ni nyeupe,atalazimisha iwe njano liyopauka!
 
Ngojea retaliation ya Ukraine ya mwana ukome ifanyike Vlad atachanganyikiwa.
 
Huruma ya Putin usiihesabu ni udhaifu.

Yeye alilenga miundo mbinu tu ya Ukraine. Hata hao 13 waliokufa ni kwa bahati mbaya tu.
Putin ni muungwana sana.

Akitaka kuua watu hata milioni anawaua tu kwa saa.

Tumia akili yako vizuri.
Ajaribu aone
 
Putin aahidi jibu 'kali' kwa ugaidi wa Ukraine

Oct 11, 2022 02:27 UTC

[https://media]

Iwapo Ukraine itapanga mashambulizi zaidi ya kigaidi dhidi ya Russia, kutakuwa na jibu kubwa la kijeshi sawa na lile lililotekelezwa Jumatatu.

Onyo hilo limetolewa na Rais wa Vladimir Putin wa Russia ambaye amethibitisha kwamba jeshi la nchi yake limefanya mashambulizi makubwa Jumatatu dhidi ya Ukraine kwa kutumia silaha za masafa marefu ambazo zimelenga vituo vya nishati na mawasiliano ya kijeshi vya Ukraine.

Shambulio hilo lilitokea siku mbili baada ya bomu kuharibu daraja la kimkakati la Crimea, ambalo Moscow imeliita shambulizi la kigaidi la Ukraine.

Rais Putin ameendelea kusema kuwa: "Iwapo kutakuwa na majaribio zaidi ya kufanya mashambulizi ya kigaidi katika ardhi yetu, Russia itajibu vikali na kwa kiwango kinacholingana na vitisho vilivyoibuliwa dhidi ya yake."

Kulingana na Waziri Mkuu wa Ukraine Denis Shmygal, Mapema Jumatatu, mikoa kadhaa ya Ukraine ilikumbwa na mashambulizi ya makombora, na miundombinu muhimu isiyopungua 11 iliharibiwa.

Rais Putin alisema kuwa Russia mashambulizi hayo ya kulipiza kisasi yamekuja baada ya majaribio kadhaa ya kuharibu miundombinu ya Russia ambayo yamehusishwa na Ukriane.

Rais Putin amessema miongoni mwa mambo mengine, Ukraine iliharibu sehemu ya mfumo wa kusambaza umeme wa kinu cha nyuklia cha Kursk na ilijaribu kuharibu bomba la gesi asilia la TurkStream linalosafirisha gesi asilia kutoka Russia hadi Uturuki. Aidha na Rais wa Russia amebaini kuwa Ukarine imehusishwa na mlipuko wa Jumamosi ulioharibu Daraja la Crimea.

[https://media]Hujuma ya kigaidi dhidi ya Daraja la Crimea

"Utawala wa Kiev umekuwa ukitumia mbinu za kigaidi kwa muda mrefu sana," rais wa Russia ameendelea kusema na kutaja mauaji ya watu mashuhuri, mashambulizi ya kiholela ya miji ya Donbass na Kiwanda cha Nyuklia cha Zaporozhye kuwa mifano ya vitendo kama hivyo.

"Kwa kweli, serikali ya Kiev imejiweka sawa na vikundi vya kigaidi vya kimataifa. Kuacha uhalifu kama huo bila jibu imekuwa haiwezekani," alisisitiza, kabla ya kuthibitisha kwamba Russia ilishambulia miundombinu ya Ukraine.

Mbali na kuilaumu Ukraine kwa mfululizo wa mashambulizi dhidi ya miundombinu ya Russia, Putin ameashiria kuvurugwa mabomba ya kusafirisha gesi ya Nord Stream. Alisema kuwa Russia inazuiwa na mataifa ya Ulaya kuchunguza hujuma hiyo na akasisitiza kuwa "sote tunamfahamu vyema mnufaika mkuu wa uhalifu huo."

Putin aliyasema hayo alipokuwa akiongoza kikao cha Baraza la Usalama la Taifa la Russia.

Mlipuko wa Jumamosi kwenye daraja la Crimea, kiungo muhimu kati ya peninsula hiyo Russia bara, uliua raia kadhaa na kuangusha sehemu ya daraja linalotumiwa na magari. Aleksandr Bastrykin, mkuu wa Kamati ya Uchunguzi ya Russia, aliripoti kwa Putin siku ya Jumapili kwamba Ukraine ndiyo iliyohusika na uhalifu huo, huku kiongozi huyo wa Russia akibaini kwamba "hakuna shaka" kuhusu hilo.
Zaidi kaangusha majengo na raia 19 kwenye mabomu 83, Huko Donbas maiti za majeshi ya russia zimetapakaa, amepanik jamaa wameahidi kuendeleza kugomboa ardhi yao, yeye kama ni kidume alitakiwa ashuke chini sio kukaa black sea ama kutoka russia na kurusha bomu la mpata mpatae

Wenzake wanashabaha na kwa sababu hiyo ndio matokeo ya daraja lakini mengi yajayo, tukitoka kwenye G7 ni kichapo tu, mizigo inamiminika Ukrean
 
Back
Top Bottom