PSRS: Majibu ya Maswali na Hoja za wadau, Desemba 2014/Januari 2015

Status
Not open for further replies.

Maxence Melo

JF Founder
Feb 10, 2006
4,230
13,415
Sekretarieti ya Ajira katika Utumishi wa Umma, inapenda kuwashukuru wadau na wananchi wote waliotuandikia maoni pamoja na kuuliza maswali mbalimbali kwa kipindi chote cha mwezi Juni, Julai na Agosti, 2015.

Tunapenda kuwajulisha wale wote waliotuandikia maoni na maswali na hawajafungua baruapepe (Emails) na kurasa za Facebook wazifungue kwa kuwa kila swali limejibiwa na kutumwa katika anwani husika na baadae kuyaunganisha maswali na maoni yanayofanana na kuyatolea majibu ya jumla kwa faida ya wasomaji wetu wengine ili kuendelea kuelimishana kuhusu masuala ya uendeshaji wa mchakato wa ajira Serikalini.


Imetolewa na Kitengo cha Mawasiliano Serikalini-Ofisi ya Rais Sekretarieti ya Ajira katika Utumishi wa Umma.

24 Agosti, 2015.

Kwa mawasiliano zaidi +255687 624975, facebook page 'Sekretarietiajira', Barua pepe: gcu@ajira.go.tz au kupitia portal ya ajira sehemu iliyoandikwa feedback.
 
Ahsante kwa bandiko hilo hakika nimejifunza kitu hapa!
 
Mie huwa nakwazika saana na hili...WALE WALIOAJIRIWA,KUSTAAFU AU KUFUKUZWA KAZ HAWAPASWI OMBA....SASA SIE AMBAO TUMEAJIRIWA NA SERIKALI HAWAONI KUWA WATUNYIMA FURSA ZINGINE??
 
Zile ajira za SSRA ndo zmechinjiwa baharin, interview toka mwez wa saba mpka leo hakuna majibu..
 
Nimejifunza kitu ambacho ckukijua na hata ckujua kama ni muhimu kujua... Asante sana.
 
Mie huwa nakwazika saana na hili...WALE WALIOAJIRIWA,KUSTAAFU AU KUFUKUZWA KAZ HAWAPASWI OMBA....SASA SIE AMBAO TUMEAJIRIWA NA SERIKALI HAWAONI KUWA WATUNYIMA FURSA ZINGINE??

Huoni kuwa ni kuwazibia fursa ambao hawajaajiriwa?
 
1.swali langu kwa PSRS ni kwa nini mchakato wenu wa usahili unachukua muda mrefu sana kuanzia mnapo tangaza mmbaka kuwapangia vituo vya kazi?
 
1.swali langu kwa PSRS ni kwa nini mchakato wenu wa usahili unachukua muda mrefu sana kuanzia mnapo tangaza mmbaka kuwapangia vituo vya kazi?

swali la msingi sana hili,,yani mtu unaomba kazi mpaka majina yakija kutoka ushasahau km uliomba yani
 
tume ya ajira mchakato wao upo taratibu sana mpaka mtu unachoka usubiri au unasahau kama uliomba aisee
 
Mnaposema hand delivery ya application letters hairuhusiwi mnamaanisha hata hand delivery ya EMS au inakuaje?
msaada please
 
Vipi kuhusu vyuo vikuu vizembe, ambayo, kushindwa kutoka vyeti kwa baadhi ya wahitimu kwa muda husika?? Na je tutor taarifa au introduction letter inatosha!
 
Mimi ni mmoja wa walioomba kazi kwa kupitia mfumo wa elektroniki. Nimeitwa kwenye usaili na wakatuambia kuwa majibu yatatoka baada ya wiki mbili. Ila sasa unaenda wiki ya nne hakuna majibu yoyote.

Naomba ufafanuzi, tafadhali...
 
Status
Not open for further replies.
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…