Proving the Bible (1): Carbon 14 Dating

I gave you a link answering all these questions. You're lazy.

Plus you can't ignore the difference between kinds and species. It's part of the equation.
Look Man, this is a forum and it is expected that when you start a thread you'd know what you're talking about.
Theres no point in starting a thread when every question you're asked you put a link.
Not everybody is goint to have time or the resources to check those links from other platforms.
Otherwise we would've went to those platforms and not opened your thread at all.
Can you atleast summarize your answers in short words. Please
 
Look Man, this is a forum and it is expected that when you start a thread you'd know what you're talking about.
Theres no point in starting a thread when every question you're asked you put a link.
Not everybody is goint to have time or the resources to check those links from other platforms.
Otherwise we would've went to those platforms and not opened your thread at all.
Can you atleast summarize your answers in short words. Please
I didn't start a thread about the flood did I? I simply said I was gathering evidence.
 
Kwa tafsiri kilichoumbwa ni anga na ardhi kavu,maji yalikuwacp yameifunuka dunia nzima,mstari wa
 
My mistake, I apologise..I must be seeing things, I might be the first one to talk about the flood in this thread.
Well I talked of the flood in relationship with chemistry and geology, refer to the thread: Carbon-14.

You need concrete explanations of the flood in all other spheres which I wasn't prepared for. I gave you some links. If you specifically want the explanations from me you can wait......for weeks at the very least
 
Mbingu na nchi siyo mbingu na dunia

◄ Genesis 1:1 ►

New International Version
In the beginning God created the heavens and the earth.

New Living Translation
In the beginning God created the heavens and the earth.

English Standard Version
In the beginning, God created the heavens and the earth.

Berean Standard Bible
In the beginning God created the heavens and the earth.

King James Bible
In the beginning God created the heaven and the earth
...
I'm not going to start debating translations. Good day/night.
 
Well I talked of the flood in relationship with chemistry and geology, refer to the thread: Carbon-14.

You need concrete explanations of the flood in all other spheres which I wasn't prepared for. I gave you some links. If you specifically want the explanations from me you can wait......for weeks at the very least
Im patient, I'll wait.
 
UKITAKA KUAMINI bible na Mungu kwa asilimia 100 JIFUNZE VITABU VYA UNABII.
Mfano kitabu Cha UFUNUO na Daniel

1. Vinaeleza mambo yaliyopita nyuma kabisa.

2. Vinaelezea VIONGOZI na Empire mliosoma darasani. Babeli, Ujemi na umedi, Uyunani, Dora ya kirumi inayotawala sasa.

3. Vinaelezea umri na UNABII HALISI.
Mfano,
:Kuanzishwa kwa DINI ya kiislamu Hadi mwaka HALISI.
:Kuanzishwa kwa TAIFA la MAREKANI Hadi mwaka
Kugawanyika kwa bala la ULAYA.
:KUIBUKA KWA Dora ya Rumi.
:UPapa

4. Bible ni kitabu KIZURI mno ukiweza kuelewa VITABU Hivi viwili.
Vina sili nyingi mno.

NAIPENDA SANA BIBLIA
 
Dunia Ina miaka Elfu SITA tu.
6000.

Hizo ni kazi za ibilisi kuwadanganya.
HAO wote wanaokosoa UUMBAJI WA MUNGU tunajua wapo chini ya vikundi Gani Duniani na wanalipwa hela nyingi sana

Isac newton Alisoma Daniel akaelewa akamkori Mungu, kwamba kweli Mungu yupo.

Wewe ni nani kwa Izack newton????????
 
(usomaji wa dakika 14)

Tufanye hesabu!

Kabla hatujaanza, kuna maandiko haya matatu.

1 Wathesalonike 5:21

Pimeni kila kitu: Zingatieni kilicho chema.

Yohana 8:44

Yeye alikuwa muuaji tangu mwanzo. Siku zote alikuwa kinyume na ukweli. Hakuna ukweli ndani yake. Yuko kama uongo anaousema. Ndiyo, ibilisi ni mwongo. Na ni baba wa uongo.

Wakolosai 2:8

Angalieni mtu ye yote asiwateke kwa falsafa duni na potofu ambazo hutegemea mapokeo ya kibinadamu na mafundisho ya kidunia, na wala si Kristo mwenyewe.

Jambo kuu lililonifanya nitilie shaka biblia hapo zamani ni habari za historia. Tunajua historia ya Biblia inarudi nyuma takriban miaka 6000.

Lakini kadri muda ulivyoenda, wanahistoria na wanasayansi wa ki kidunia wanaoanza chunguzi zao kwa nadharia za kupinga biblia na Muumbaji walizidi kuja na "gunduzi" zao zenye kuelezea hali tofauti kabisa.

Imagine kusoma "mifupa ya miaka 200,000", "mabaki ya miaka 50,000,000", "miamba ya miaka 400,000,000,000",

Karibu kila kitabu na kila chombo cha Habari kinaripoti namba hizo!

Sasa Biblia inayoonyesha binadamu wa kwanza alikuwepo miaka 6000 tu iliyopita si inaonekana kituko!

View attachment 2646106

Wakristo walioshindwa kukana imani yao ilibidi waanze kuisoma biblia upya wajaribu kupatanisha hizo gunduzi na kweli zilizoandikwa kwenye biblia,

ndomana kuna wakristo wanaamini nadharia ya mageuzi, wanaona simulizi la Adam na Hawa ni fumbo na sio tukio halisi, wanaamini zile siku za uumbaji sio siku halisi bali ni mfano wa mamilioni ya miaka.

Lakini UKWELI ni kuwa njia zinazotumika kupima umri wa wa vitu vya zamani (Radiometric dating), vikiwemo mabaki ya viumbe hai, mawe na miamba, zote zinathibitisha dunia hii ni changa ya miaka elfu kadhaa tu, wala sio zee ya mabilioni ya miaka! Wala hakuna mabaki yenye umri mkubwa kiasi hicho!

Tuanze somo la jinsi ya kupima umri wa historia; tutaanza na Radiocarbon.

Kwanza kila kitu kimetengezwa na atomi (atoms), kama matofali yanavyotengeneza nyumba.

Kama ambavyo matofali yanatengenezwa na maji, mchanga na saruji, Atomi nazo zinatengenzwa na protons, neutrons na electrons.

Protons na neutrons zinakaa kwenye kiini. Electrons zinazunguka kiini.

View attachment 2646061

Idadi protons kwenye kiini ndo kinatokeza umbo tofauti (elements) lenye sifa za kipekee tofauti na maumbo mengine, Mfano sodium in protons 11, Oxygen ina 8, Nitrogen ina 7 n.k.

Idadi ya protons kwa kila element Huwa haibadiliki, na kwa kawaida idadi ya protons na neurons ni sawa kwa kila atomi.

Lakini kuna elements nyingine ambapo unakuta atomi zake tofauti zina idadi tofauti ya neutrons, lakini idadi ya protons ni ileile (Isotopes).

Mfano Carbon yenye protons 6 inaweza ikawa na neutrons 6, 7 au 8 (yaani Carbon 12, Carbon 13 na Carbon 14 respectively).

View attachment 2646065

Baadhi ya hizi isotopes huwa hazijatulia, zinajikuta zinatoa mionzi hadi zinabadilika kuwa element nyingine (radioactive decay).

Mfano Carbon-12 na Carbon-13 zimetulia. Lakini Carbon-14 haijatulia, itaanza kutoa mionzi mwishowe neutron moja inabadilika inakuwa proton, hivyo na umbo (element) linabadilika inakuwa Nitrogen-14.

Kuhesabu umri kutumia Carbon-14

Carbon-14 hupatikana duniani kutoka kwenye jua. Miale ya jua inakuja spidi na neutrons zake, inapiga anga letu lililojaa Nitrogen, Nitrogen ikiungana na hizo neutrons inatengeneza Carbon-14.

Carbon-14 na Carbon-12 zinaungana na Oxygen kutengeneza Carbon Dioxide inayotumiwa na mimea. Kwahiyo vyakula tunavyokula na hewa tunayopumua vina Carbon-14 na Carbon-12.

Viumbe hai vyote kwenye miili yao kuna uwiano wa C-14 na C-12 sawa na uwiano uliopo kwenye hewa (ambao kwa sasa ni C-14 moja kwa C-12 trillion moja).

View attachment 2646070

Kiumbe hai kikifa, kinaacha kupokea C-14 (kupitia chakula na hewa).

Na kwakuwa C-14 haijatulia (inageuka kuwa N-14), kadri muda unavyoenda itaendelea kupungua kwenye mwili.

Kwakuwa C-12 haibadiliki, na ndani ya mwili wa kiumbe kuna uwiano unaojulikana wa C-12 na C-14, tunaweza kujua kiasi cha C-14 kilichopotea kwenye mwili kwa kuhesabu kiasi cha C-12 kilichopo.

Wanatumia kifaa hicho kwenye picha kinaitwa Accelerator Mass Spectrometer (AMS) kinachopima uwiano wa Carbon hizi mbili.

View attachment 2646073

Sasa ili kupima umri, kwanza tujue hii C-14 inabadilika kwa kiwango/spidi gani.

Wanatumia half-life, yaani muda ambao inachukua kwa nusu ya idadi atomi iliyo kwenye Sampuli kupotea.

(Note: Kila umbo (element) ina half-life yake ambayo ni constant, na haitegemei idadi ya atomi kwenye sampuli ya kuanzia).

Half life ya C-14 ni miaka 5730.

Yaani nikichukua kopo nifungie humo idadi fulani ya C-14 pekeyake, baada ya miaka 5730 nitakuta nusu ya C-14 imebadilika imekuwa N-14. Baada ya miaka mingine 5730 nusu iliyobaki itabaki nusu yake tena (1 -> 1/2 -> 1/4 -> 1>8...n.k).

View attachment 2646079

Kwahiyo tayari tunakua tunajua:

- idadi ya C-12 iliyopo kwenye sampuli ya mwili uliokufa ambayo haibadiliki

- ratio ya C-12 na C-14 kwenye kiumbe hai, ambayo ni C-14 moja kwa C-12 trillion moja

- half life ya C-14, ambayo inafanya ratio ya C-12 na C-14 izidi kupungua, hivyo kadri ratio ilivyo ndogo ndo kadri muda mrefu ulivyopita baada ya kiumbe kufa.

Hivyo tunaweza kupima ni kiasi gani cha C-14 kilikuwepo kabla kiumbe hakijafa, hivyo kujua pia kilikuwa hai wakati gani uliopita.

Dhana moja muhimu

Kuna dhana moja (assumption) inayotumiwa kwenye haya mahesabu, ambayo ni kuwa uwiano wa C-14 na C-12 kwenye dunia ulikuwa sawa miaka yote.

Kama hii ni kweli, mahesabu yote ya umri kupitia kifaa cha AMS kilichotajwa huko juu, yanakuwa sahihi hadi takriban miaka 80,000 tu kwakuwa vyombo wanavyotumia watafiti kupima C-14 havina uwezo wa kutambua uwepo kiwango kidogo cha C-14 kilichobaki baada ya miaka hiyo.

Pia, kama dhana hiyo ya uwiano wa C-12 na C-14 sio kweli, basi mahesabu yote ya umri yanakuwa yamekosewa.

Ni jambo gani linaloweza kufanya uwiano wa C-14 na C-12 ubadilike?

Kama uwiano wa wa utengenezaji wa C-14 kwenye anga haulingani na kutolewa kwake (removal) hasa kupitia kupotea (decay), ratio ya C-12 na C-14 haiwezi kuwa sawa, hivyo kufanya ishindikane kutambua kiwango cha C-14 kilichokuwepo wakati kiumbe kimekufa.

Aliyegundua hii njia ya kupima umri kutumia C-14 (Dr. Willard Libby) ali assume uwiano huu wa utengenezaji na utolewaji wa C-14 kuwa sawa, na alitoa dhana hiyo kutoka kwenye dhana ya mageuzi, inayodhania kuwa dunia ina mabilioni ya miaka.

Dhana kwenye ulimwengu wa sayansi ni muhimu. Kama dhana ya kuanzia imekosewa, basi mahesabu yote yanayofuata hata kama ni sahihi bado yanatoa hitimisho lisilo sahihi.

Kwenye kazi zake huyo Dr. Libby alitambua kuwa uwiano wa utengenezaji na utolewaji wa C-14 sio sawa. Na hilo ilimsumbua kwasababu kama kweli dunia ina mabilioni ya miaka, umeshapita muda mrefu hivyo kunapasw kuwa na uwiano.

Mwenyewe alipiga mahesabu akaona kuwa kama dunia ilianza bila C-14 yoyote kwenye anga, ilipaswa kuchukua miaka 30,000 tu ili kutokee uwiano sawa Kati ya utengenezaji na utolewaji wa C-14.

Dr. Libby aliamua kupuuza tatizo hili kwenye mahesabu yake akasema itakuwa kuna kosa flani kwenye majaribio (experiments) lakini lazima uwiano uwe sawa.

Lakini ni KWELI kuwa uwiano wa C-14 na C-12 hauko constant kwasababu kuna C-14 nyingi zaidi zinazotengenezwa kuliko zinazopotea, wala sio kosa la experiment.

Inajulikana kuwa kiwango mahususi cha utengenezwaji wa C-14 (Specific Production Rate (SPR)) ni atomi 18.8 za C-14 kwa kila gramu moja ya Carbon kwa dakika moja.

Na kiwango mahususi cha utolewaji wa C-14 (The Specific Decay Rate (SDR)) ni kinajulikana, ni atomi 16.1 za C-14 kwa kila gramu moja ya Carbon kwa dakika moja.

Hii inamaanisha nini?

Inamaanisha kuwa, kama inachukua miaka 30,000 tu ili kufikia uwiano sawa wa utengenezaji na utolewaji na C-14 na bado hakuna uwiano, basi inawezekana dunia haina umri mkubwa kama wanamageuzi wanavyodhani.

Shamba la sumaku la Dunia (Earth's Magnetic Field)

Dunia imezungukwa na shamba la sumaku linalolinda dunia na mionzi hatari kutoka angani. Shamba hili linazidi kuishiwa nguvu.

View attachment 2646127

Kadri shamba hili linavyozidi kuwa na nguvu, ndivyo kiwango cha miale ya jua inayoingia duniani inapungua. Hivyo zamani wakati lilikuwa na nguvu zaidi, kulikuwa na kiwango kidogo cha utengenezwaji wa C-14 kuliko sasa.

Wachora historia ya shamba la sumaku la Dunia wanakubaliana na nadharia ya mwanafizikia anayetetea uumbaji Thomas Barnes kuwa nguvu ya shamba la sumaku la Dunia yetu imekuwa ikipungua nguvu miaka yote, hivyo haliwezi kuwa na zaidi ya miaka 10,000.

Leo hii, nguvu ya shamba la sumaku la Dunia imepungua kwa asilimia 10 toka mwaka 1845 ambapo mtaalam wa hisabati
Carl Friedrich Gauss alianza kulifwatilia.

Kama kiwango cha utengenezwaji wa C-14 ulikuwa mdogo hapo zamani, basi mahesabu yetu ya sasa yatadhani kuwa kuna kiwango kingi cha C-14 kimepotea kuliko kiwango halisi kilichopotea, hivyo kutoa umri mkubwa zaidi wa sampuli kuliko umri halisi.

Gharika la Noah

Gharika la Noah lingekuwa na matokeo gani kwenye kiwango cha Carbon?

View attachment 2646128

Gharika lingezika kiwango kikubwa sana cha wanyama na mimea hivyo kutengeneza nishati za ardhini kama mafuta na makaa ya mawe.

Kiwango cha nishati hizo zinazotokana na mabaki ya viumbe hai kilichopo leo, kinaashiria kulikuwa na idadi kubwa sana ya mimea kabla ya gharika.

Yaani kabla ya gharika, kulikuwa na kiasi cha Carbon ndani ya mimea na viumbe hai mara 500 zaidi ya ilivyo leo. Kimahesabu, hali hiyo ilipunguza zaidi kiwango cha C-14 na kupunguza zaidi uwiano wa C-12 na C-14.

Kikundi cha watafiti kilichoitwa Radioisotopes and the Age of The Earth (RATE) kilitumwa na mashirika yanayotetea sayansi ya uumbaji mwaka 1997 kufanya utafiti uliodumu miaka nane na kugharimu zaidi ya dollar milioni mbili.

Kilitumwa kutafuta data zinazopuuzwa au kufichwa na wanasayansi wanamageuzi na mahesabu yao.

Walifuatilia nadharia na taratibu zinazotumika kupima mawe, miamba na mabaki ya viumbe.

View attachment 2646110

Waligundua mengi ikiwemo:

1) Kuna C-14 kwenye mabaki ya viumbe ambayo kiumri hayakupaswa kuwa na C-14.

Kwamfano kuna njia wanamageuzi wanatumia kupima umri wa mabaki ya viumbe kwa kupima umri wa miamba ambamo mabaki hayo yamepatikana.

Mfano kuna sampuli ya mabaki ya mbao yalichukuliwa kwenye safu tofauti za miamba iliyopimwa na kukutwa na umri kati ya miaka 40,000,000 na 250,000,000, kwahiyo wanahitimisha kuwa na hizo mbao zina umri huo.

Lakini hata kwa kutumia njia yao ya C-14, walikuta sampuli hizo zina kiasi cha C-14 ambacho kinatoa umri wa mabaki hayo kuwa ni kati ya miaka 30,000 na 45,000 tu.

Watafiti wa RATE walipitia majarida ya wanazuoni waliotafiti kutumia C-14 na kukuta sampuli kibao (zaidi ya 40) za aina hiyo, yani sampuli za viumbe hai wanaodaiwa kuishi mamilioni ya miaka iliyopita lakini wana kiwango cha C-14 kingi badala ya kutokuwa nayo kabisa.

Watafiti wa RATE pia walichukua sampuli 10 za makaa ya mawe kutoka kwenye safu kadhaa za makaa ya mawe ambazo wanamageuzi walizipima na kudai ni za zamani sana (kuanzia miaka 65,000,000 hadi miaka 540,000,000). Walichukua tahadhari zote kuhakikisha haziwi contaminated.

Sampuli zote hizo zilikutwa na viwango vya kupimika vizuri kabisa vya C-14.

Ni jambo la kushangaza kwakuwa half-life ya Carbon ni fupi (miaka 5730) kwahiyo hakupaswi kuwa na kiwango cha kupimika cha C-14 baada ya miaka 100,000.

Kwa kutumia hesabu zao hizo hizo za C-14, sampuli zote kutoka safu zote za makaa ya mawe kuanzia ya miaka milioni 65 hadi miaka milioni 540, zote zilikutwa na takribani miaka 50,000 tu.

Ukitumia mahesabu ya halisi zaidi ukizingatia uwiano wa C-12 na C-14 kabla ya gharika la Noah, umri unapatikana kuwa ni miaka 5,000 tu.

Matokeo haya yanaonyesha umri wa safu zote za miamba ya chokaa haizidi miaka 100,000 (kwasababu ya uwepo wa C-14), na inaweza kuwa ndogo zaidi.

2) Ugunduzi mwingine wa kikundi cha RATE ni kiwango cha C-14 kinachopatika kwenye Almasi (Diamond).

View attachment 2646102

Wanasayansi wa kidunia kupitia njia nyingine za kupima umri (ambazo tutaona baadae pia nazo zinadhihirisha umri mdogo wa Dunia), walisema Almasi zina miaka mamilioni hadi mabilioni.

Watafiti wa RATE walichukua sampuli 12 za Almasi na zote zilikutwa na C-14 ingawa kwa kiasi kidogo kuliko sampuli za viumbe.

Hili limethiitishwa na watafiti wengine pia tofauti n RATE, kuwa Almasi zina C-14.

Huu ni uthibitisho tosha kuwa Makaa ya mawe na Almasi havina umri wa mabilioni ya miaka kama wanamageuzi wanavyodai.

Wazo la kuwa "wakati wa sasa ndio funguo ya kujua wakati uliopita" linawaletea shida wanaoamini kuwa dunia ni ya mabilioni ya miaka.

Namna mbadala ya kusoma data za C-14 tofauti na wanamageuzi wanavyodai ni kuwa: kulitokea gharika dunia nzima ambayo ndo imetengeneza safu za miamba na mabaki ya viumbe hai ambao sampuli zao zote bado zina C-14.

View attachment 2646113


View attachment 2646130

(Nimekuwa nikikusanya uthibitisho wa gharika. Very interesting. Uthibitisho ulio wazi kabisa kila mahali lakini ndo hivyo wanatafuta kila namna kutafuta interpretation ya ajabu ya data mradi wakwepe kutaja gharika la Noah. Wengine wanakubali kulikuwa na gharika Dunia nzima lakini sio ya kwenye biblia 😂)

Wakristo wasiogope Carbon 14, Carbon 14 iko upande wetu kutetea Dunia changa kabisa ya miaka elfu kadhaa tu iliyopita.

2 Petro 3:8

Lakini wapendwa msisahau neno hili, kwamba kwa Bwana, siku moja ni kama miaka elfu, na miaka elfu ni kama siku moja.

Methali 3:5,6

Mtumaini BWANA kwa moyo wako wote, wala usizitegemee akili zako mwenyewe. Katika njia zako zote mkiri yeye, naye atanyoosha mapito yako.


Makala kwa hisani ya Answers in Genesis.

Next time: Kuhusu njia wanazotumia kupima miamba kuwa mabilioni ya miaka (radioisotope dating na isochron dating) ambazo kiuhalisia TUMEPIGWA pia, na ukweli ni kinyume kabisa.
Ujue kwamba DUNIA enzi hizo ilikuwa inamaanisha baadhi ya maeneo ya Mashariki ya Kati na sio dunia jinsi tuijuavyo leo.

Biblia ni contextual sio factual na inatumia lugha ya kimwili kuongelea mambo ya kiroho.
 
unabisha tafiti za sayansi hiyo Jf ,simu,magari,ndege,matibabu na n.k ungeyaona wapi

Hujui kilichoandikwa ni matokeo ya tafiti hizo hizo za sayansi? Did you even read the article?

Plus Carbon-14 inahusianaje na "jf, magari, ndege, simu na matibabu"?

Ndomana ma layman tunapigwa maana ni ili mradi atokee mtu na cheti chake kinachoheshimiwa basi chochote atakachotangaza tunabeba. Lakini kama tulivyoona kwa Dr. Libby aliyebuni Hesabu za Carbon-14, hawa wanasayansi are not infallible. And their works need to be checked especially by Creation scientists.

Kadri navyofanya uchunguzi nagundua Science proves God and not the other way round. Do not be deceived.

He is the greatest Mathematician, Programmer, Scientist, Artist!!

Psalms 111:2

Great are the works of the LORD, studied by all who delight in them. Full of splendor and majesty is his work, and his righteousness endures forever
 
Ujue kwamba DUNIA enzi hizo ilikuwa inamaanisha baadhi ya maeneo ya Mashariki ya Kati na sio dunia jinsi tuijuavyo leo.

Biblia ni contextual sio factual na inatumia lugha ya kimwili kuongelea mambo ya kiroho.
"Enzi hizo" maana yake nini? Toa neno original la Kigiriki/Kiebrania/Aramaic lililotumiwa kwenye kifungu gani kisha utuonyeshe watfsiri wametafsirije.

By the way, jambo hili linahusiana nini na Carbon-14?
 
I think it would be rather childish to assume that 6000 species that entered the ark evolved into a billion species present on earth today for only 6000 years
I think its not childish yo can just observe the demographic trends of the human species can answer it all
from year 2021 to 2022 there was an increase in no of people by 0.88% which is about 70,206,291 people in just one year now multiply that no by just 1000 years you get over 70 billion people and that is just for human species only which is not much efficient in reproduction rate.... assume those species that undergo asexual reproduction, the number might be unimaginable yet very real..
 
Back
Top Bottom