muongozaji
JF-Expert Member
- Oct 9, 2009
- 1,386
- 1,002
Hilo ni kweli kabisa, ukiona kiongozi wa Kizungu anakuja Afrika ujue kuna sababu maalumu na kwa kuwa sisi tuna IQ ndogo Wazungu wanasema IQ ya Kusini mwa Sahara ni 70 wkt ile ya Dunia nje ya kwetu inaanzia 90 kuendelea (hii ni kulingana na hao Wazungu tunaowaabudu hivyo usinihukumu)!
Kilichomleta Netanyahu Afrika ndicho kile kile kilichomleta Kim wa Korea Kaskazini na ndicho kilichomleta Park wa Korea Kusini Afrika pia, hawa wote wanahitaji mtu wa kuwaunga mkono kwenye mambo yao huko UN, sasa kwa kuwa Dunia nje na Afrika watu wanajitambua sehemu pekee ya wao kupata kura za bure ni Afrika kwetu (Kusini mwa Sahara) hakuna kingine, wanazuga kuja na Wafanyabiashara lkn ajenda ndiyo hiyo wanataka kura za Afrika huko UN, sasa Israeli (hasa utawala wa Netanyahu) unabanwa na Dunia nzima kuhusu uonevu wanaowafanyia Wapalestina hata Ulaya wanasapoti Palestianian State mpaka Obama mwenyewe sasa wanahitaji (Isreali) mtu wa kuwasapoti huko UN ni nani huyo?
Ndiyo maana nampenda na kumkubali Raisi wangu Magufuli, hana mpango na hao takataka na wala kwanza hajaenda kwenye upuuzi wao!!
Long live raisi Magufuli!
Umetoa ufafanuzi sahihi kabisa. Kuna vitu ambavyo watu wengi wa chini ya jangwa la Sahara hawavielewi hasa pale inapokuja aspect ya foreign policy na diplomacy ya nchi za hawa wenzetu. Nimeona hata kwenye hii thread kuna watu wanaleta ubishi bila kuelewa kile wanachokibishania kwa undani/usahihi.