Usanii wa pea za epa kwenye usanii wa filamu. Kazi ipo.Wasanii wetu wa bongo movie wamekua na majina makubwa huku wengi wao wakiwa na hali mbaya kiuchumi.Wengi wamekua wakiitupia lawama kampuni ya muhindi ya Steps kuwa ndio inayowanyonya wasanii.Msanii Batuli alikiri kuwa filamu hazilipi,na ili msanii aweze kijikimu inabidi kutafuta pedeshee la kumuweka mjini.Wasanii wa kiume kama Dr Cheni wako vizuri kiuchumi kwa sababu wanajituma kufanya shughuli nyingine nje ya uigizaji.
Sasa hivi kuna hii kampuni mpya iliyotoa filamu ya Lulu ya Folish age iitwayo Proin.Hawa jamaa wanaonekana kwa kila namna wana lengo la kuimeza Steps.Mpaka dakika hii tayari imeshasaini mikataba na wasanii wakubwa wa filamu akiwamo Lulu na Steve Nyerere na wengine wengi.
Ni vizuri Steps akapata mpinzani,maana upinzani unaweza kuwasaidia vijana waliojikita katika sanaa.Ni vyema wasanii wetu wakafaidi matunda ya vipaji nyao.Inasikitisha kuona dada zetu wakiuza miili yao kwa wazee wa rika la baba zao ilimradi wajikimu na maisha wakati wana majina na vipaji vinavyoweza kuwapa maisha mazuri.
Nimefurahi kuona Proin wakileta upinzani kwa STEPS lakini hofu yangu ni je hawa PROIN wana nia ya kuwakomboa wasanii wetu au lengo lao ni kuendeleza unyonyaji.
Wasanii kwa vile PROIN bado ni changa na inawanyenyekea ili muende upande wao ningewashauri na nyie kutumia hii fursa kuonesha thamani yenu katika kusaini mikataba itakayowanufaisha.
Tuwaunge mkono kwani wanapojitokeza wapinzani wengi ndio msanii atakaponufaika, Ila cha msingi na wasanii nao wacheze vema kwenye upande wao...waje na kazi zinazoeleweka na sio madudu.
Usanii wa pea za epa kwenye usanii wa filamu. Kazi ipo.
Jamaa wa proin wanaangalia pesa hawana haja na puchi za wasanii wa bongo movie wanalipa vizuri sana ila kwa installment ili kuweza kuwa manage wasanii wao wasifulie kwa steps mtu unapeleka movie baada ya six month ndo unaeza kupewa hela yako tena robo robo...
Kama hawana haja ya papuchi mbona JR ambaye ni mmoja wa ma CEO anagonga Lulu au hali papuchi anakula 0713?acheni promo za kishamba nao hawana tofauti na Steps
Kama ni Proin ya pale Mikocheni karibu kwa JK, basi Steps wajiandae...jamaa biashara wanaifahamu...Steps bado itakimbiza kwa miaka Kama sita ijayo... Neither proin nor 5effects has the capability of pulling steps down....
Steps bado itakimbiza kwa miaka Kama sita ijayo... Neither proin nor 5effects has the capability of pulling steps down....
Kama ni Proin ya pale Mikocheni karibu kwa JK, basi Steps wajiandae...jamaa biashara wanaifahamu...
mmesahau changamoto moja ambayo imekuwa ikiisumbua tasnia ya filamu ambayo ni wizi wa kazi za wasanii.....mheshimiwa mkulu naskia washamlilia sana khs hili suala ila km kawaida ya ccm wamepuuuzia kbsa
Kuzuia wizi wa kazi za wasanii ni zaidi ya kumlilia Rais... kwanza wao wenyewe wala hawaonekani kama kweli wapo tayari wao kama wao kupambana na uharamia... wengi ubishoo umewazidi! Hebu fanya kufikiria, endapo kungekuwa na Msama kama 20 tu hapa wangekuwa wamezuia wizi kwa kiasi gani kinyume chake, namuona Msama peke yake ndie anaepambana kwa vitendo huku wengine wakikalia kulia lia tu!mmesahau changamoto moja ambayo imekuwa ikiisumbua tasnia ya filamu ambayo ni wizi wa kazi za wasanii.....mheshimiwa mkulu naskia washamlilia sana khs hili suala ila km kawaida ya ccm wamepuuuzia kbsa
Kuzuia wizi wa kazi za wasanii ni zaidi ya kumlilia Rais... kwanza wao wenyewe wala hawaonekani kama kweli wapo tayari wao kama wao kupambana na uharamia... wengi ubishoo umewazidi! Hebu fanya kufikiria, endapo kungekuwa na Msama kama 20 tu hapa wangekuwa wamezuia wizi kwa kiasi gani kinyume chake, namuona Msama peke yake ndie anaepambana kwa vitendo huku wengine wakikalia kulia lia tu!
Hizi kazi zinauzwa mitaani mwetu... kwa Dar es salaam karibu kila kitu cha daladala kunauzwa kaz fake za wasanii na ndio vituo hivyo hivyo ndivyo vinatumika na hao hao wasanii! Kuna siku kwenye mtandao mmoja wa kijamii tulikuwa na mjadala mkubwa sana wa suala hili! Wakati ule, baadhi yao walikuwa wanaridhishwa kutokana na utendaji wa COSOTA pamoja na TRA katika kuzuia suala hili! Mleta mada, Producer na Director mmoja maarufu, nikamweleza wazi kwamba hamjui mnachoongea! Nikawauliza, ikiwa kweli mathalani, kazi kutoka Nigeria huwa zinapata kibali COSOTA kuonesha kwamba zimetoka mikono salama ambako zililipiwa kodi (huko zilikotoka) na hivyo sio one of the pirated materials zinazokuja ku-create competition na kazi za nyumbani, COSOTA wanatumia vigezo gani kujiridhisha kwamba kazi hizo ziliriripiwa kodi huko zilikotoka!!! Hakuna cha maana alichoongea zaidi ya kuendelea kuendelea kuongea kile ilichoonesha wazi kwamba hakifahamu! Kwa hasira, akaamua kuni-block ingawaje ametuma tena request baada ya hasira zake kumwisha!
Aina ya mikataba yenyewe haiwafanyi Crew Members kuwa na uchungu na kazi zinazouzwa mitaani! Chukulia Hollywood kwa mfano, tumwache mwigizaji ambae ndie anauza filamu... hata mwandishi wa script, si kwamba akishalipwa chake tu ndo basi tena, bye for good! Wapo wenye mikataba ambayo inasema wazi kabisa kwamba, pamoja na kuwa tayari umeshalipwa, Box Office ikifika kiasi fulani, utapewa bonus ya kiasi fulani! Sasa kibongo bongo, assume umeandika script ukalipwa sh. laki tano... hapo hata kama filamu itaingiza sh. bilioni tano, wewe huna chako... laki tano yako ulishalipwa! Sasa katika mazingira kama hayo usitarajie kwamba wasanii watakuwa na uchungu na kazi zinazouzwa kama njugu mitaani... chao walishalipwa na ndo imeshatoka hiyo!
Mifano ni mingi lakini linapokuja suala la wizi wa kazi za wasanii; kuna matatizo pande zote mbili! Mambo ambayo zamani niliwahikuwaeleza ndiyo yale yale ambayo kwa sasa ndiyo yanatokea!
Suala la sheria, ni kweli kuna tatizo kubwa sana katika hilo na ukiangalia vizuri, kuna mengine zaidi yanatakiwa kufanyika pamoja na hayo masuala ya sheria!mkuu kiukweli umeandika point ila umesahau suala la wizi wa kazi za wasanii ni suala la kisheria zaid na hpo role ya serikal ndyo inapokuwa kubwa zaid kuliko ya wasanii wenyewe, leo hii msama anajitahidi kuwakamata hawa wezi lkn wanapofikishwa kwny vyombo vya sheria hawapewi adhabu kali ya kuwafanya waogope kurudia tena kwa hyo inakuwa km kazi bure ,nilishawahi kumsikia kikwete akilalamika khs hili suala na akaahidi kuwasaidia lkn mpk sasa ni kimya .....ki ukweli hii vita ni ngumu sana bila ya msaada wa serikali
uwiz wa kazi za wasanii, wasanii wenyewe hawaathiriki ndio maana wanachukulia poa.
msanii akitengeneza film anakwenda peleka master cd steps entertaimentt, anapewa chake mfn ml20 au mln50. steps anagonga kopi hata akiuza mln100 ni juu yake kwani anakuwa hati milki, msanii anakuwa hana chake.
huko mtaani wajasiriliamali nao wanafanya yao kupiga fake kopi, hapo muhindi inakuwa inakula kwake na sio msanii. msanii habari yake kwisha.