Program Note: Mahojiano na Mhe. Sofiia Simba

Mzee Mwanakijiji

Platinum Member
Mar 10, 2006
33,475
39,988
460%3E_1507880.jpg


Mojawapo ya chaguzi ambazo zimekuwa na mvuto wa muda mrefu ndani ya CCM ni ule uliofanyika mwishoni mwa juma lililopita ambapo Mwenyekiti mpya wa Jumuiya ya Wanawake wa CCM (T) alipatikana.

Mshindi huyo si mwingine bali Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Mhe. Sofia Simba. Safari ya ushindi wake ilikuwa ni safari ambayo wachache wako tayari kuipitia. Ilikuwa ni safari ambayo unapofika mwisho inabidi ujiuliza ulianzaje safari hiyo.

Hivyo KLHN ilipata nafasi ya kuzungumza naye kwa kirefu kuhusu ushindi wake huo na hasa kutupa mwanga kuhusu kile kilichokuwa kinaendelea kati yake na mpinzani wake katika uchaguzi Mhe. Janeti Kahama.

Pamoja na hayo tumemuuliza maswali ya kutaka kujua kama kweli Rais Kikwete ndiye aliyemtaka agombee na kama ni kweli hotuba ya Rais Kikwete kwenye ufunguzi wa uchaguzi ilikuwa ni ya kumpa mkono wa baraka ili achaguliwe. Pamoja na hayo tulitaka kujua zaidi kuhusu UWCCM utakuwaje chini ya uongozi wake?

Kwa maoni au mawazo tuandikie mhariri@klhnews.com


BONYEZA HAPA KUSIKILIZA
 
Back
Top Bottom