Mdau
JF-Expert Member
- Mar 29, 2008
- 1,789
- 470
Wadau,nimekua nikimfuatilia kwa karibu sana mheshimiwa huyu,ambae ni mwenyekiti wa Taifa wa CUF, na mgombea urais mara 4 kwa tiketi ya chama chake....nafahamu kwamba kila mtu kajaliwa umbo lake na mwenyezi Mungu, lakini ni wazi kwamba kama mtu unapita kwenye misukosuko na shida nyingi,basi aghalabu afya huyumba...afya ya chama cha CUF haipo sawa, nguvu iliyokua nayo miaka ya nyuma kama chama ngangari na cha pili kwa umaarufu zimepungua au zimeisha kabisa...mojawapo ya watu ambao dhoruba hii huwapata moja kwa moja ni wahusika wa karibu katika kuendesha shughuli za chama...wote ni mashahidi jinsi TLP inavyomnyong'onyeza mzee wetu wa Kiraracha...Tofauti ninayoiona kwa CUF ni kwamba,wakati chama anachokiongoza Prof Lipumba kikizidi kuporomoka kwa umaarufu,yeye anazidi kunenepa na kunawiri haswa...wengine husema kunenepa ni kuridhika,hata ukila mawe..JE,PROF LIPUMBA ANARIDHIKA NA AFYA YA CHAMA CHAKE KAMA MWENYEKITI????