Profesa Jay machozi jasho na damu

ukwaju_wa_ kitambo

Senior Member
Joined
Sep 15, 2024
Posts
155
Reaction score
182
PROFESSOR JAY -MACHOZI,JASHO NA DAMU

VERSE..1

Nashukuru Macho yangu mawili hayana upofu/ na mdomo upo wazi kukemea mambo maovu/ siku inapofika naona Heri ya jana/ maisha ya wabongo yanakuwa kama ya wanyama/ hiki ninachosema kila jicho linaona/ nina futa chozi la mnyonge kilio cha kila kona/ damu ya mtanzania naona sasa inavuja/ na hali ya hatari kwa kasi nayo inakuja/ ni macho mangapi yanatazama hospital Kina mama wanajifungua kwenye mazingira ya hatari/ utu unatutoka inapotokea Ajali/ majeruhi wana uwawa watu waibe mali/ nafuta jasho la mlala hoi chozi la mnyonge/ na ililia damu ya zanzibar wote tuombe/ jasho linashamili kwenye Uso wa mlala hoi/ na sauti inakauka kwenye koo la Turn boy..

CHORUS..

Tunaishi kama hakuna kesho/
Amani kwa yatima,kina mama, watoto wenye mateso
Machozi ,jasho na damu kwa watanzania /
Ya wote tuwe pamoja tu sali kwa nia/

Tunauwana kama hakuna kesho/
Amani kwa machinga ,wana Apolo,masela wenye mateso/
Machozi,jasho na Damu kwa watanzania /
Na mungu atasikia tusali kwa nia...

VERSE..2..

Msalamba wa dhiki bado una muelemea / mtanzania halisi hana pa kuengemea/ najaribu kuishika vizuri fimbo ya mnyonge/ nwendo wa miguu mitatu na anapiga moyo konde/ mkutano wa Beijing ungefanyika kijijini/ labda na bibi yangu nae angekuwepo ku ndini/ misaada haipati inaishia mijini/ tajiri anaongezewa ni vipi kwa masikini/ ninasema kwa Uchungu wengine wananicheka/kwenye kambi ya lahana ujue wewe mateka/ siasa ya kiBongo imeanza kunuka Damu/ndugu watanzania wana uwana kwa zamu/ nani ataizoa damu inayo mwangika / nyerere alitabiri ya kwamba tuta adhirika/ siasa sio mchezo kama karata tatu/ jazba inapo panda ina ng'oa nyoyo za watu/ mishale na mikuki imetawala kilosa/ nachali na wachaka wauwa bila makosa/wote walikufa mungu walaze pema/ rehemu marehemu wapate safari njema/ futa machozi yangu msanii ya hati miliki/ kila nikijivuta naona si thaminiki / upendo unatoweka ngiza ndio linatanda/ unyama ufedhuli mututu juu ya Anga/ msio penda Amani toeni na roho yangu/ mnao nyonya watu sikia kilio changu/ mnaotaka haki guseni na hoja zangu/ wote wenye mateso shikeni mkono wangu...

CHORUS..

Tunaishi kama hakuna kesho/
Amani kwa yatima,kina mama, watoto wenye mateso
Machozi ,jasho na damu kwa watanzania /
Ya wote tuwe pamoja tu sali kwa nia/

Tunauwana kama hakuna kesho/
Amani kwa machinga ,wana Apolo,masela wenye mateso/
Machozi,jasho na Damu kwa watanzania /
Na mungu atasikia tusali kwa nia...

VERSE..3.

Kila nikinyamaza naji sikia kusema / kuishikiana mitutu wa Bongo bado mapema/ sijawahi kuona mimi masikio yakizindi kichwa/ ila sasa kwa mbali naanza kuifuta picha/ naota nusu nusu masuala mengi ya vita/ nafikiri kwa kina ni nani ata athirika/ mtoto wa kigongo masomoni London/ au bibi na Babu wanao lima shambani / hatua kwa hatua nadhani huo ndio mwendo/
Mambo yanavyo kwenda hakuna cha uzalendo/ naona hata vibaka Msheli wanajishuku/ ni bora kuiba mabilioni kuliko kuku/ kibaka na mla rushwa nani angeuke mfano/ jasho la mahabusu halimo kwenye mikingamo/ watu wanapofanya maovu bila vificho / ndipo napo gundua Dunia yafika mwisho/ jasho la mlala hoi lazindi kuchuluzuka/ na upande wa pili vigongo wananuka Rushwa/ nakuta kundi la watoto wengi kwenye mitaa/ nauliza wanachofanya wanadai wana ngaga njaa/ tufumbe macho tusadiki tumuombe Allah / serikali imelala na haya si masihara/ wengi wana acha shule wengi wana kuwa malaya/ wengi wanakuwa wezi na wengi wanapata miwaya/ ni nani atairisha yatima kwenye mitaa/ nani atakae zuia Ukimwi unao zagaa/ nani atazuia vita na baa la njaa / eeh Mwenyezi mungu epusha hili balaa..

CHORUS..

Tunaishi kama hakuna kesho/
Amani kwa yatima,kina mama, watoto wenye mateso
Machozi ,jasho na damu kwa watanzania /
Ya wote tuwe pamoja tu sali kwa nia/

Tunauwana kama hakuna kesho/
Amani kwa machinga ,wana Apolo,masela wenye mateso/
Machozi,jasho na Damu kwa watanzania /
Na mungu atasikia tusali kwa nia...

Ukwaju wa kitambo

0767 542 202
 

Similar Discussions

Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…