Profesa huyu anastahili pongezi za dhati

Profesa huyu anastahili pongezi za dhati

Maneno haya kina Msalani wayapeleke Lumumba labda yale mabilioni ya uswizi yangerudi na kuwekezwa huko kwa hao mafisadi ajira zingeongezeka.
Mkuu Manyerere, asante!. Kwanza nakuu mkono pongezi zako kwa Prof. Ngoma, na kuungana na wito watu, watu wenye uwezo, wakumbuke makwao, wawekeze makwao na kuinua makwao kama CRS ya kurudisha kile kidogo with appreciation!.

Bila kujali sources of fund, tunachoangalia hapa ni "The end justifies the means!", ila mimi naomba niende a bit deeper zaidi katika "the motive behind" ziara yako kuzuru kijiji hicho!. Kama ulikuwepo hapo kwa safari zako nyingine, na ikatokea tuu ukauona huo mjengo, ukahamasika na kuutumia ku inspire na wengine, then its very fine!.

Lakini kama ulifanya "facility visit", kwa lengo hilo tuu, whoever facilitated that "visit kutembelea maendeleo ya enero hilo", might have "motive behind" with a good intention "watu" waone maendeleo ya "see what this man is doing for us!", hive mbunge wa eneo hilo ni nani vile?!, ili na mimi nimlobby a sponsored tour, atutembeze atuonyeshe amefanya mini, vinginevyo 2015...

Hongera zake Prof. Ngoma!.
Asante.
Pasco
 
Hongera Wachaga ,sasa kilichobaki ni kuchukua nchi basi kilimanjaro itakuwa kama "london

Ngoma ni majina ya Wapare na Mwanga ni maeneo ya Wapare. Au unamaanisha na Wapare pia ni Wachagga kwa kua wanatoka mkoa wa Kilimanjaro???
Heko watu wa Kilimanjaro
 
Wiki hii nimefika Mwanga mkoani Kilimanjaro.

Nimedhuru vijiji kadhaa kama Mgagao, Ngulu, Lembeni na Kwakoa.

Hapo kwakoa nimekuta kitu cha hamasa sana.

Kuna jengo kubwa mno la kisasa linajengwa na Profesa Ngoma.

Ni hospitali, chuo na kwa shughuli nyingine. Kwakoa ndipo alipozaliwa Profesa huyu, hakika mradi huu ni wa mfano kwa wasomi kukumbuka kuwekeza kwao.

Profesa ngoma si wa kujikweza, lakini nadhani anastahili pongezi nyingi akingali hai.

Wasomi wakifanya mambo makubwa ya aina hii bila shaka vijana wengi watapenda kuishi vijijini.

Naomba wanahabari wazuru kwakoa wajionee fahari hii ya mtanzania huyu.

Bila shaka itakuwa hospitali ya Cancer (Kwakoa Cancer Institute Hospital KCIH)maana mashine kibao za kuchoma mionzi ameziiba sana kwa kujifanya ni write-off.
 
Pasco, ziara yangu inahusu migogoro ya ardhi. Ilitokea tu nilipofika hapo nikaona hilo jengo. Nikajibiwa kuwa ni kazi ya huyo msomi. Hakika nikawa sina jingine, isipokuwa kumpongeza na kuwapa hamasa watanzania wasomi wengine kufanya mambo makubwa kama haya Kwa hiyo hiku kitu nilikutana nacho tu kwa "bahati mbaya'.
Mkuu Manyerere Jackton, asante. Kama ni hivyo nakuunga mkono, big up sana kwa Prof. Ngoma!. Nilidhani hii ni moja ya zile "facility trips" kuwapeleka waandishi mahali ili sio waende tuu kuandika habari za maendeleo, bali waandike ili "watu" waone, 2015 kieleweke!.

Thanks.
Pasco.
 
Wiki hii nimefika Mwanga mkoani Kilimanjaro. Nimedhuru vijiji kadhaa kama Mgagao, Ngulu, Lembeni na Kwakoa. Hapo kwakoa nimekuta kitu cha hamasa sana. Kuna jengo kubwa mno la kisasa linajengwa na Profesa Ngoma.

Ni hospitali, chuo na kwa shughuli nyingine. Kwakoa ndipo alipozaliwa Profesa huyu, hakika mradi huu ni wa mfano kwa wasomi kukumbuka kuwekeza kwao. Profesa ngoma si wa kujikweza, lakini nadhani anastahili pongezi nyingi akingali hai. Wasomi wakifanya mambo makubwa ya aina hii bila shaka vijana wengi watapenda kuishi vijijini.

Naomba wanahabari wazuru kwakoa wajionee fahari hii ya mtanzania huyu.

Kesho uandike kama mwandishi wa habari ninaona tu prifesa ngoma. Hivi hujui mtu anatambuliwa kwa angalau majina mawili?. Sasa ngoma ni jina la ukooo. Na ngoma maprofesa wapo wengi huyu profesa ngoma wako anajina moja tuu?
 
Hata kama ni ufadhili, ametumia akili na utu kwa kutambua kuwa vijijini nako wana haki ya kusogezewa huduma muhimu kama hizo. Lakini kubwa ni kwamba profesa amerejesha fadhila kwa ndugu na jamaa waliohangaika kumsokesha. Matunda ya usomi wake kayajeresha nyumbani. Hili ni jambo la kuigwa na wengi wetu.

mkuu kuna thread huko habari na hoja mchanganyiko una hamasisha watu kujichukulia sheria mkononi,.... umetia aibu sana, hilo neno kwa red hapo hukutumia ...
 
Hongera kwa msomi huyu....
Uwekezaji wa aina hii ndo unaleta chachu ya maendeleo. Wazawa ni kila kitu...
 
Wiki hii nimefika Mwanga mkoani Kilimanjaro. Nimedhuru vijiji kadhaa kama Mgagao, Ngulu, Lembeni na Kwakoa. Hapo kwakoa nimekuta kitu cha hamasa sana. Kuna jengo kubwa mno la kisasa linajengwa na Profesa Ngoma.

Ni hospitali, chuo na kwa shughuli nyingine. Kwakoa ndipo alipozaliwa Profesa huyu, hakika mradi huu ni wa mfano kwa wasomi kukumbuka kuwekeza kwao. Profesa ngoma si wa kujikweza, lakini nadhani anastahili pongezi nyingi akingali hai. Wasomi wakifanya mambo makubwa ya aina hii bila shaka vijana wengi watapenda kuishi vijijini.

Naomba wanahabari wazuru kwakoa wajionee fahari hii ya mtanzania huyu.

Safi sana profesa. Sio kama Nkapa wetu kahama kwao kaenda kuwekeza Ushoto. Na akifumba macho mmzike huko huko sio kuanza kutuleta usumbufu huku Ntwara. Kwanza huku mikusanyiko imepigwa marufuku ili wenye gesi wastarehe
 
Kama aliandikia pepa kwa ajili ya hapo kwao na hisani ya watu wamarekani wakaona hivyo hongera zake Prof kama aliandikia pepa kwa Tanzania nzima na kwao kuna hospitali za kutosha si sahihi maana kuna maeneo hayana kabisa.Nawaona wengi wampongezao hawataki kujua fedha zimetoka wapi ila ndo hawo hawo wanaomlaumu Rais kwa kujenga bandari Bagamoyo.WaTanzania tuache ubinafsi.
 
Kama aliandikia pepa kwa ajili ya hapo kwao na hisani ya watu wamarekani wakaona hivyo hongera zake Prof kama aliandikia pepa kwa Tanzania nzima na kwao kuna hospitali za kutosha si sahihi maana kuna maeneo hayana kabisa.Nawaona wengi wampongezao hawataki kujua fedha zimetoka wapi ila ndo hawo hawo wanaomlaumu Rais kwa kujenga bandari Bagamoyo.WaTanzania tuache ubinafsi.

Charity begins at home yeye kafanya kwa nafasi yake kukumbuka nyumbani ila wengine wakipata hawakumbuki vile vile huwezi kuandika ya Tanzania nzima yeye alikuwa na malengo ya huko atokako na sio nchi nzima
 
Hata kama ni ufadhili, ametumia akili na utu kwa kutambua kuwa vijijini nako wana haki ya kusogezewa huduma muhimu kama hizo. Lakini kubwa ni kwamba profesa amerejesha fadhila kwa ndugu na jamaa waliohangaika kumsokesha. Matunda ya usomi wake kayajeresha nyumbani. Hili ni jambo la kuigwa na wengi wetu.

Ukiona mwandishi wa afrika anampa sifa mwafrika mwenzake ujue hapo si bure kuna kitu kapewa au kaahidiwa!..tunawajua nyinyi na njaa zenu za kujiendekeza!..kila mwandishi ana kambi yake na wewe naona ushaanza kujichagulia kambi! Huna haja ya kujitetea hayo ndo maisha yenu waandishi njaa
 
Kalagabaho, mimi si wale wa kutoa sifa mtu akiwa keshakufa. Kama mwananchi kafanya jambo jema tumsifu akiwa hai. Ni upuuzi kudhani haya yanasemwa kwa sababu ya bahasha. Nimesema wazi kwamba hiki kitu nimekiona, nikahamasika nikiwa kwenye masuala mengine kabisa ya wafugaji na wakulima. Tusiwe na fikra chovu za kudhani kila jema linalostahili sifa, lazima wa kusifu awe kapewa bahasha au ana ajenda ya mwaka 2015. Lets be serious!
 
Back
Top Bottom