natamani ningekuwa rais ningeifanya zenj mkoa na hao vimbelembele kama jusa ningewarudisha kwao uaharabuni, hawa ndio wanaotududisha nyuima. Tanahitaji raisi mbabe ndio tuendelee. La sivyo hatutafika mahali. Huyu jussa ni ni mtu hatari na si mzalendo kabisa ni mamluki
kosa ni kubwa sana Zanzibar(mkoa) kuipa hazi ya nchi matokeo yake ndizo hizi chokochoko, yani watu million moja na robo wanatusumbua hivyo, nasikia kichefuchefu kuona Jussa anaendekezwa sana , watu kama hawa ni kuwakata kilimilimi
Kilichoombwa ni bahari kuu ya kimataifa sio eneo la Zanzibar JUSSA FIKILI KABLA YA KUSEMA
waelezee hao majuha wasojua kutambua, hapo umepiga ikulu kwenyewe! kilichoombwa hawakijui na wanacholalamika sijui kimetokea wapi!? poor barubaru &co.
Kumbuka vile vile Znz ni nchi kamili yenye mamlaka kamili na hilo limebainishwa katika katiba ya Znz.
Nadhani hapa mtamuonea bure tu huyu mama. Hakuna nchi mbili au mataifa mawili. Kuna nchi moja tu nayo inaitwa Tanzania. Prof. Tibaijuka anatumikia Jamhuri ya Muungano wa TAnzania. Na kinyume na wanasiasa wa CUF wanavyojaribu kushawishi, uamuzi huo ulipewa baraka na serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar ndio maana Waziri toka kwenye serikali hiyo naye alikuwepo UN wakati wa kupeleka ombi hilo. Lakini vile vile kwa wanaofahamu mchakato wa mambo haya wanajua kabisa kuwa maamuzi haya ya kimataifa toka chini ngazi za wataalamu hadi inapofikia ngazi ya mawaziri serikali zote mbili hushirikiana vizuri sana.
Kuongeza eneo la bahari haiongezi eneo la bahari ya Tanganyika! Linaonekana eneo la bahari ya Tanzania ambayo Zanzibar ni sehemu yake. Kwa hiyo labda kama kuna sababu nyingine. Sioni mahali popote ambapo pana msingi wa kuliuliza Baraza la Wawakilishi juu ya hili kwani suala la eneo la Muungano ni eneo zima la Tanzania. Hakuna bahari ya Zanzibar!
Kama wapo watu wa CUF au wengine wanaoamini kitendo hiki kiko nje ya madaraka ya serikali ya Muungano; wafungue kesi ya Kikatiba kukipinga na kukizuia. Of course, I know no one will.
Kilichoombwa ni bahari kuu ya kimataifa sio eneo la Zanzibar JUSSA FIKILI KABLA YA KUSEMA
Barubaru na wenzake wanashangaza kwani wanajua kuwa Waziri Aboud kama sikosei naye yuo kwenye msafara wa NY; hao CUF na CCM najua ni kitu kimoja nilitegemea wawe wanajua kila kitu kuliko kuja kupayuka majukwaani kana kwamba kinachofanyika ni siri. Nadhani Jusa ni mtu hatari sana na serikali ya JMT im-mulike na tochi mchana kabla giza halijaingia
Naomba nikuweke sawa kidogo kwani kuna mambo umeyasahau kidogo.
Tanganyika na Znz zimeungana kimkataba na sio kikatiba. Kuna mambo yamo katika mkataba huo nayo ndio mambo ya muungano. Suala la ardhi na makazi si suala la Muungano na ndio maana Znz kuna waziri wa wizara hiyo na Bara yupo.
Kumbuka kuwa Mamlaka ya Tibaijuka mwisho wake ni Chumbe akiwa Znz hana mamlaka yoyote ukilinganisha na waziri wa mambo ya nje au mambo ya ndani. hawa wana malka kote kote.
Kumbuka vile vile Znz ni nchi kamili yenye mamlaka kamili na hilo limebainishwa katika katiba ya Znz. Kwa msingi huo Katiba hiyo hiyo imeanisha eneo la Znz kiufasaha kabisa. sasa kwa ombi hilo la Tibaijuka ni lazima katiba ya Znz itabidi ibadilike kwa kuongeza eneo la milki yake au kupunguza miliki yake na hapo ili kubadilisha kipengele hicho cha katiba lazima BLW litahusika vilivyo kwani wao ndio wtunzi wa sheria za Znz na mambo yote yaliyo nje ya muungano.
Kumbuka kuwa katika Picha walopiga kule UN wakti wanawakilisha alikuweo Tibaijuka, balozi wa Tz katika UN, Mbunge wa Mafia na Katibu wa wizara kutoka Znz. Kwa mantiki hiyo inaonekana wazi Prof Tibaijuka alipata baraka zote za Bunge la Muungano dio maana akachukua muwakilishi wa Bunge.
Sasa upande wa BLW hawakuwa na taarifa zozote ongezeka hilo officially na aliku husishwa kwa lolote lile kitu ambacho Jussa amehoji. Ikumbukwe kuwa maombi haya yakifanikiwa lazima BLW litahusishwa katika kupitisha sheria za ongezeko la eneo la miliki la Znz.
sasa labda tujiulize.
Je Znz itaongezewa kiasi gani katika hicho kilicho ombwa? hilo ni suala ambalo limegubikwa na utata mkubwa na alijabainishwa katika mkataba au mbi hilo.
Lakini pia lazima ufahamu kuwa Tz na Znz zote zinaongozwa na Rules of Law. Na mihimili yote mikuu inajipambanua yaani Serikali, Bunge na Mahakama bila kuingilia katika utendaji kazi wake. Kila muhimili unajitegemea.
Limeanza baraza la wawakilishi kuhoji Serikali ya Znz kisha uzi utafuata. Kwani majibu ya Serikali ndio yatatoa mwangaza kwa sakata hilo. Lakin all in all Tibaijuka lazima ajiuzuru hapo.
Kwani mtiririko wa jambo hili unakuwa sawa kabisa na ule wa Tz kujiunga na OIC.
Hivi Zanzibar inatambuliwa UN kama nchi? Hivi UN waweza pokea ombi toka kwa mwanachama ambaye si nchi akiishtaki nchi? Zanzibar kwenda kupinga UN wataenda kama nani hadi UN wawasikilize? Hivi CUF wanajua wanachoongea? Hivi UN wanafikiri ni Jimbo la Wawi ambako mwana CUF yeyote aweza enda na kusema lolote.CUF hata wakienda UN nobody will listen to them after all CUF is not a UN member.
Naona kama unajichanganya mwenyewe. Unaposema Tanzania iliwakilishwa ....... na Zanzibar haikuwakilishwa ......, Una maana gani? Unataka kutuambia Zanzibar si sehemu ya Tanzania?Waziri Moh'd Abood hakuwepo kwa mujibu wa picha aliyokuwepo kwene blog ya Issa Michuzi. Yule mweupe uliyemuona ni mbunge wa Mafia naye aliwakilisha Bunge la Muungano. Suala mbona hakukuwa na mwakilishi toka Baraza la wawakilishi?
Kumbuka kuwa katika Rules of Law kuna mihimili mikuu mitatu katika nchi nayo ni Bunge, Makahakama na Serikali. Tanzania iliwakilishwa na Mihimili ya Bunge na Serikali na Znz iliwakilishwa na Serikali na BLW halikuwakilishwa na kutojulishwa kuhusu suala hili.
Na at the end of the day BLW watahisishwa katika kubadili kipengele cha Katiba hususan kila cha eneo la miliki.
Ndio maana wawakilishi wmeuliza hilo kwanini wao hawakujulishwa kuhusu ombi hilo wakti linagusa muungano. Na suala la ardhi ni jambo ambalo haliko katika mambo ya muungano?
Kuna siri hapo ambayo Tibaijuka ameificha nayo lazima ijulikane na kubainishwa.
Tusubiri tu majibu ya Serikali.
Mamlaka ya JMT ni kamili. Eneo la jamhuri ya Muungano ni eneo zima la bara na visiwani. Hakuna eneo lolote la 'nchi ya Zanzibar' ambalo si eneo la JMT. Kama lipo niambie. Katiba ya ZNZ inaweza kusema lolote lakini ikipingana na ile ya Muungano vipengele vyake ni batili. Zanzibar ni nchi kwa Wazanzibari tu; siyo nchi inayotambulika mahal popote duniani. Kuwa na jeshi, mahakama, na rais (mihimili mitatu ya dola) hakuifanyi ZNZ kuwa nchi vinginevyo miye ningetamba niko "nchi" ya Michigan! Kuongeza eneo la bahari kutakuwa na manufaa kwa Zanzibar na kwa Tanzania nzima. Wananchi wa ZNZ yawapasa wafurahi na kuunga mkono uamuzi huu wa serikali ya JMT.
Unahangaika bure ndugu yangu kuwafahamisha na kuwapa maana wakati hawajuwi neno lenyewe muungano. Kwao wao Tanzania ni Tanganyika na Tanganyika ni Tanzania wala hawjuwi kuwa kuna kitu Zanzibar.
Kwao wao matusi na kejeli ndio wanachokijuwa na utakuwa mwenzao kama utakuwa unaweza kufanya kama wao tu.
Nadhani wewe unachotaka kuelezea ama kushawishi hapa ni upupu mtupu.Tanzania ni muungano wa Zanzibar na Tanganyika sasa waziri wa Tanzania anapokuwa hana mamlaka Zanzibar kwa sababu Zanzibar ni nchi,hoja yako inakosa mwelekeo.
Huwa najiuliza hivi watu kama ninyi na hao kina Jusa mnasiri gani dhidi ya wananchi! .Mtazamo wangu wananchi wanahitaji huduma bora za jamii na usalama wa maisha yao .Ila wote mnaoleta hizi chokochoko ni waroho wa madaraka, badala ya kuishauri na kuikosoa serikali kuweka uwiano wa matumizi ya rasilimali kwa manufaa ya wananchi,ninyi mpo majukwaani mkidai Zanzibar ni nchi.Mnachokitaka hakitakaa mkipate kwa sababu wengi wenu hamjui mnachohitaji.
Halafu ningewashauri wewe na hao wapiga debe wenzako kina Jusa kipindi hichi cha kubadili katiba ndio muafaka kuweza kuweka mambo sawa kwa yale yote mnayoona ni kikwazo.Ila kutokana na kuwa mna ajenda zenu za siri mnatanguliza matakwa yenu binafsi badala ya matakwa ya wananchi.
Hiyo ardhi /bahari inayoongezwa ni ya Tanganyika ama Tanzania! kwanza hiyo Tanganyika haipo sasa sijui kinachowapandisha majukwaani na kupaza sauti kama vile nyie sio watanzania.Wapemba wanaofanya biashara Kariakoo na kusaidia ndugu zao walioko Zanzibar isingekuwa huu muungano unafikiri mambo yangekuwaje! .Nadhani ni vyema kuleta hoja zenye/zilizofanyiwa utafiti na sio kutoa hoja kutokana na hulka za mrengo wa kivyama.
Nimelipenda hilo neno. Rarely huwa linatumika kuelezea hisia kali mtu alizonazo. Ila kwa kumwambia Prof ajiuzuru ni kumuonea. She did not go there as Prof Tibaijuka trust me
Hao ndio wajukuu wa Sultani wamewambukiza mpaka wamatumbi nao wameingia kwenye kukana bidii za kukombooa Nchi yao,iliyokombolewa kwa mkono wa Okello mmatumbi mwenzao.Wanzanzibar shida sana, najua tuliovijana sasa hivi kuna siku isiyo na jina uko mbele ya safari wakisha toka kwenye utwala hawa wazee wanaongangania Muuungano tutawapa Ultumatum kuchagua wawe watanzania Zanzibar iwe Mkoa au Tuwaache wakaishi wanavyotaka.Na wale watakaao amua kuwa Watanzania watabaki Tanzania wtakao amua kuwa Wanzanzibar kwaheri hivyo hivyo kwa Wamatumbi walio Zanzibar wakitaka kuwa Wanzaibar hay wachague wakiataka kuludi Tanzania karibu waachane na Uzanzibar.
Hakika Watu hawa hawatachukua muda watanyukana tu,sasa hivi wanataka hayo kwa sababu ya msukumo wa kuapata nafasi za utukufu wa madaraka na si vinginevyo.Nje ya tamaa hiyo hakuan la msingi mpemba ni mpemba na munguja ni munguja tena HAWAPENDANI KAMA NINI.
Sasa hivi hii ni tamaa za viongozi aina ya JUSSA wakisaidiwa na WAFITISHINAJI ambao hapo zamani walionekana ndio wanaitakia mema Tanzania kupitia CCM walipopata PESA NA POWER kwa njia haramu sasa wanawachezesha viongozi wetu SINDIMBA kwa mapigo ya KIPEMBA.Wanajua sasa kuwa tayari Bara kumeshanuka na wakati wowote chaweza kutokea cha kutokea sasa lililopo kwa sasa ni kuengineer mchezo mchafu wa Zanzibar kuwa Nchi kisha wakimbilie huko kujificha chini ya kivuli cha undungu wa kufanana rangi.
lazima mjue Zanzibar ni nchi kamili yenye mamlaka kamili kwa mujibu wa sharia za Znz. Na Muungano wanalijua hilo.
Watu wengine sijui wanafikiri kwa kutumia masuburi? umeambiwa mchakato huu ulianza mwaka 2007. Prof. Tibaijuka amekuwa waziri tangia 2010. Pili hili jambo liweze kwenda UN lazima liliridhiwe na baraza la mawaziri, ambalo mwenyekiti wake ni Rais JK na rais wa Zanzibar ni member kama waziri asiye na wizara maalumu.
Kwa mukhutada huo kwanini Tibaijuka ajiuzuru na siyo JK au Shein aliyeshindwa kuitetea ZNZ kwenye kikao cha baraza la mawaziri?!
Acha masaburi bana! OIC na EPZ wapi na wapi, I guess baada ya hapa utaifananisha EPZ na Vatican?
Muungano upi huo unaongelea? Muungano wa Tangayika na Zanzibar? Kama ndiyo hivyo basi Prof Tibaijuka ni Waziri wa Ardhi na Makazi wa Tanganyika na Zanzibar (i.e. Muungano)
Acha masaburi bana!
Ni sawa ulivyosema kuwa Zanzibar ni nchi kamili kwa sharia za Zanzibar sio za UN.Ni kweli hata muungano tunalijua.Ukienda UN unatakiwa uende na faili la sheria za UN huendi na faili la sharia za Zanzibar faili la sharia za Zanzibar mwisho wake ni bandari ya Zanzibar.