Prof. Safari kweli upo CHADEMA?

Prof. Safari kweli upo CHADEMA?

Rockcity native

JF-Expert Member
Joined
Dec 31, 2012
Posts
2,174
Reaction score
1,460
Habari za weekend wana JF,

Nina swali moja kwa Prof Safari, hivi mbona simwoni katika majukwaa ya M4C au katika harakati yoyote ile ya CHADEMA? Mara ya mwisho kumsikia ilikua katika hekaheka ya uchaguzi mdogo wa Igunga aliposimamia kidete suala la DC kuvuliwa hijabu hapo kidogo alisikika akitetea chama. Lakini toka mda huo sijamwona kwenye harakati yoyote.

Au kuja kwake CHADEMA ilikua nguvu ya soda kumkomoa Lipumba?

MAJIBU toka CHADEMA:
Mkuu,

Prof. Safari yupo, na mbali ya kuwa mwanachama mwandamizi, ni mjumbe wa Kamati Kuu ya CHADEMA, mmoja wa wanasheria waandamizi wa CHADEMA ambao wamekuwa wakifanya kazi usiku na mchana kupambana na hila chafu za CCM kuvuruga nchi na kuumiza wananchi kwa kutumia mhimili wa mahakama na baadhi ya watumishi wasiokuwa waaminifu wanaoamua kutumikia maslahi ya CCM badala ya maadili yao kwa kutafsiri sheria na kutenda haki.

Ameshiriki katika kutoa ushauri na kushiriki moja kwa moja katika kesi nyingi ambazo ama chama kimefungua au kimefunguliwa kwa viongozi wake kushtakiwa.

Ni mtu anayetumika na amekubali kutoa uwezo na uzoefu wake katika masuala ya kisheria, kisiasa, kijamii na pia kitaaluma, kila anapohitajika kufanya hivyo, kwa ajili ya Watanzania. Anashiriki vikao ambavyo ndivyo vinaamua hiyo M4C. Maana yake yeye na wenzake katika CC, anayo nafasi ya kutoa mchango wa operesheni kufanyika au kutofanyika!

Ni mmoja kati ya wanasheria watakaotambuliwa na chama kama umma utakavyojulishwa karibuni.

Tunasonga mbele kwenda kuwatumikia Watanzania katika nyanja zote, ikiwemo huu utumishi bora na uliotukuka wa akina Prof. Safari na wenzake wengi tu na hapa naweza kuwataja kwa uchache sana sana (maana wako wengi kuanzia ngazi ya taifa mpaka vitongojini na mitaani), Mabere Nyaucho Marando, Method Kimomogolo, Mbogoro, Tundu Lissu, Amani Mwaipaja na watu wengine wenye dhamana mbalimbali ndani na nje ya chama.

Rockcity, nikuulize swali poti wangu, nani aliyesababisha leo hii Peter Kafumu, si mbunge wa Igunga, hata kabla hajatimiza mwaka mmoja bungeni?

Makene
 
ni profesa, inaonekana wala humjui kwahiyo hata akiwepo kwy m4c huwezi kumtambua sababu humjui. yupo na kazi yake anayofanya ni kubwa kama wanaofanya m4c, kasimamia kesi za msingi na hatimaye ameibuka kidedea, kama ya Igunga, ya uloleulole dhidi ya bulembo n.k.
 
Ni suala la majukumu we bwegee,,
wataalam ka prof safari huwa wapo katika kamati ya ufundi.
Sio zile kamati zenu za kwenda kwa kalumanzila...hapana kisomi zaidi.
Gamba mkubwa.
 
huyu ni mshauri (consultant) ndani ya chama na mshauri huwa haonekani majukwaani mara nyingi utakavyo!!!!!
 
Yeye anashughurikia mambo ya kisheria zaidi, kama unakumbuka kesi ya Dr Kafumu, yeye ndiye alikuwa wakili wa Kashidye wa CDM
 
Yupo, utamuona siku Chama kitakapoenda kutoa msimamo kuhusu katiba ya nchi.
 
Kama unashida naye anzisha kesi inayohusu CHADEMA utamuona tu. Afu kwanini akili zunu zinalengalenga? Acha "perepere" kafanye kazi. Au nenda msikitini au kanisani usali badala ya kushindia perepere.
 
Prof Safari ni jembe la kweli ndani ya chama,na uelewe sio lazima ukiwa mwana chadema uwe mwanasiasa wa jukwaani.
 
Habari za weekend wana jf,
Nina swali moja kwa Prof Safari, hivi mbona simwoni katika majukwaa ya M4C au katika harakati yoyote ile ya CHADEMA? Mara ya mwisho kumsikia ilikua katika hekaheka ya uchaguzi mdogo wa Igunga aliposimamia kidete suala la DC kuvuliwa hijabu hapo kidogo alisikika akitetea chama. Lakini toka mda huo sijamwona kwenye harakati yoyote.

Au kuja kwake CHADEMA ilikua nguvu ya soda kumkomoa Lipumba?

Mkuu,

Prof. Safari yupo, na mbali ya kuwa mwanachama mwandamizi, ni mjumbe wa Kamati Kuu ya CHADEMA, mmoja wa wanasheria waandamizi wa CHADEMA ambao wamekuwa wakifanya kazi usiku na mchana kupambana na hila chafu za CCM kuvuruga nchi na kuumiza wananchi kwa kutumia mhimili wa mahakama na baadhi ya watumishi wasiokuwa waaminifu wanaoamua kutumikia maslahi ya CCM badala ya maadili yao kwa kutafsiri sheria na kutenda haki.

Ameshiriki katika kutoa ushauri na kushiriki moja kwa moja katika kesi nyingi ambazo ama chama kimefungua au kimefunguliwa kwa viongozi wake kushtakiwa.

Ni mtu anayetumika na amekubali kutoa uwezo na uzoefu wake katika masuala ya kisheria, kisiasa, kijamii na pia kitaaluma, kila anapohitajika kufanya hivyo, kwa ajili ya Watanzania. Anashiriki vikao ambavyo ndivyo vinaamua hiyo M4C. Maana yake yeye na wenzake katika CC, anayo nafasi ya kutoa mchango wa operesheni kufanyika au kutofanyika!

Ni mmoja kati ya wanasheria watakaotambuliwa na chama kama umma utakavyojulishwa karibuni.

Tunasonga mbele kwenda kuwatumikia Watanzania katika nyanja zote, ikiwemo huu utumishi bora na uliotukuka wa akina Prof. Safari na wenzake wengi tu na hapa naweza kuwataja kwa uchache sana sana (maana wako wengi kuanzia ngazi ya taifa mpaka vitongojini na mitaani), Mabere Nyaucho Marando, Method Kimomogolo, Mbogoro, Tundu Lissu, Amani Mwaipaja na watu wengine wenye dhamana mbalimbali ndani na nje ya chama.

Rockcity, nikuulize swali poti wangu, nani aliyesababisha leo hii Peter Kafumu, si mbunge wa Igunga, hata kabla hajatimiza mwaka mmoja bungeni?

Makene
 
Mkuu, usiwe na wasiwasi, kamanda yupo na moiganaji mzuri tu. Unajua, siyo wote wente talanta ya kukaa na kuongea majukwaani!
 
Nafkiri siasa za ccm zimekuzoesha vibaya,sikila mwanasiasa lazima a pande jukwaani.wengine ni strategist wapo ofisini kuandaa mikakati ya chama huku wengine wakiwa facilitators.just division of labour.
 
Big up kaka makene kwa ufafanuzi mzuri nafikiri sasa ndugu yetu Rockcity native atakua ameelewa kwanini gwiji la sheria na lugha adhimu Pro Safari haonekani mara kwa mara kwenye siasa za majukwaani.
 
Unajua wadau nini? Unapoanza kumsaka nyoka lazima uanze kwenye miguu yako kumwangalia...

Mnaposema nifanye utafiti mwafikiri ntaanzia wapi kama si hapa JF? JF ndo mahala pekee pa kujua jamaa yuko wapi na anafanya nini sio kukurupuka wajameni
 
Bila kusahau pia Prof.Safari ni mbobezi katika lugha yetu ya Kiswahili!!
 
Back
Top Bottom