DuaZaMama
JF-Expert Member
- Jun 2, 2025
- 1,882
- 4,131
Mwanamajumuiya wa Afrika kutoka Kenya, Prof. Patrick Lumumba, amesema hatua za awali alizoziona kutoka kwa Rais wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassana ikiwamo kumuelekeza Mkurugenzi wa Mashtaka (DPP) kupitia mashauri ya vijana mbalimbali waliokamatwa kutokana na maandamano yaliyoambatana na vurugu Oktoba 29, 2025, kwa lengo la kuyafuta ni dalili za mabadiliko chanya lakini akasisitiza kuwa juhudi hizo hazijatosha kurejesha utulivu wa kisiasa Tanzania.
Akizungumza na Diamond TV ya Zambia, Prof. Lumumba ambaye pia ni mwanasheria na mwandishi wa vitabu amesema hatua muhimu zaidi inayotakiwa ni kuachiwa kwa kiongozi wa upinzani nchini Tanzania Tundu Lissu, ambaye anakabiliwa na tuhuma za uhaini. “Ningependa kuona jambo kubwa zaidi…ningependa kuona Tundu Lissu akiachiwa,” amesema akisisitiza kuwa kuachiwa kwake kutafungua njia ya maridhiano ya kitaifa.
Lumumba ameongeza kuwa Rais Samia ana nafasi ya kihistoria kurejesha imani ya wananchi kwa kuanzisha mchakato mpana wa maridhiano ikiwamo kuwaachia huru wote waliokamatwa kutokana na sababu za kisiasa, kuunda tume huru ya kuchunguza yaliyotokea wakati wa uchaguzi ikiwezekana kwa kushirikisha wataalamu kutoka Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) na Jumuiya ya Afrika Mashariki, kuitisha mkutano wa kitaifa utakaojumuisha vyama vyote vya siasa, asasi za kiraia, viongozi wa dini na wadau wengine muhimu kuzungumzia hatima na mustakabali wa taifa.
Akizungumza na Diamond TV ya Zambia, Prof. Lumumba ambaye pia ni mwanasheria na mwandishi wa vitabu amesema hatua muhimu zaidi inayotakiwa ni kuachiwa kwa kiongozi wa upinzani nchini Tanzania Tundu Lissu, ambaye anakabiliwa na tuhuma za uhaini. “Ningependa kuona jambo kubwa zaidi…ningependa kuona Tundu Lissu akiachiwa,” amesema akisisitiza kuwa kuachiwa kwake kutafungua njia ya maridhiano ya kitaifa.
Lumumba ameongeza kuwa Rais Samia ana nafasi ya kihistoria kurejesha imani ya wananchi kwa kuanzisha mchakato mpana wa maridhiano ikiwamo kuwaachia huru wote waliokamatwa kutokana na sababu za kisiasa, kuunda tume huru ya kuchunguza yaliyotokea wakati wa uchaguzi ikiwezekana kwa kushirikisha wataalamu kutoka Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) na Jumuiya ya Afrika Mashariki, kuitisha mkutano wa kitaifa utakaojumuisha vyama vyote vya siasa, asasi za kiraia, viongozi wa dini na wadau wengine muhimu kuzungumzia hatima na mustakabali wa taifa.