Egwugu
JF-Expert Member
- Mar 16, 2011
- 17,558
- 8,551
Mama popote pale ulipo.
Kwanza nikukumbushe ya kuwa katika somo la kiingereza hakuna msingi wa hii lugha zaidi ya kitu kinaitwa tense. Nakumbuka hii niliambiwa toka nikiwa darasa la sita mwaka 1997 na nilipoingia form one nikayaona. Kipindi hicho tulikuwa majirani na seminari moja ndogo (std5-7) na mara nyingi tulikutana nao hasa kwenye kushindana kuongea a.k.a debate na mara nyingi walitupa shida. Shida haswa ilitokea kwasababu wenzetu waliivishwa vizuri katika kuelewa msingi wa lugha ya kiingereza (tense).
Tukaendelea kukomaa na msingi wa kiingereza (structure) tukiwa O-Level huku tukijitutumua. Mungu si Athumani huko tukatoka na kuingia A-Level na huko HGL yangu ikaendelea kujengeka chini ya topic mpya kabisa ya Syntax. Nikiri wazi, hii ni topic mama katika maandalizi adhimu ya kuelekea kuifaulu hii lugha. Mtu akiiweza vizuri hii topic hutoweza kumsumbua sana lakini hata pale atakapokuwa ni wazi utaelewa anamudu hii lugha walau kwa kuiandika make kuongea ni majaaliwa kidogo na wepesi wa ulimi wa mhusika.
Sasa leo tunayaona, mliamua kuifumua elimu kwa kuanza na kuunganisha masomo ya sayansi O-Level, mkatoka hapo mkafuta biashara na kilimo na mkaenda Advance mkaondoa baadhi ya topic katika baadhi ya masomo hasa zile zilizoonekana kuwa tatizo. Kwenye hesabu mliondoa baadhi ya vipengele na katika kiingereza mkaondoa Syntax na sasa mnafundisha vitu vya juu juu tu na kuchora kadi za mialiko. Hivi kadi ndo mmeona jambo la maana sana? Kwa sababu hamna tense pale, lakini mnafundisha kuandika makala na kuripoti habari. Sasa huyu amabaye amekosa structure huko O-Level na Syntax huko A-Level hiyo ripoti anaenda kuiandikaje? Anaendaje kuandika makala?
Lakini huyu mtu kesho mnataka asimame aongee mbele ya watu, huyu mtu anaanzaje? Kama haitoshi, tunawaona wanaotoka vyuoni, nikiri wazi mie nakutana nayo sana haya matatizo. Kuna watu wako mpaka vyuoni wanaandika research zao na wengine tayari tunao huku mtaani makazini lakini wanashindwa hata kukokotoa sentensi moja ya maana katika Syntax yake sahihi. Akikuletea kazi yake umsaidie kuedit unaweza kushangaa unatakiwa kuedit kila neno juu ya neno ukurusa wa kwanza hadi ule wa mwisho, na mbaya kuliko unakuta huyu mtu anasoma hata masomo hayo hayo ya lugha huko chuo kama vile linguistics n.k. Kuna mda unajiuliza hivi kama hii ndio hari sawa, inakuwaje wakienda huko makazini kwao? Vipi huku maofisini?
Kwanza nikukumbushe ya kuwa katika somo la kiingereza hakuna msingi wa hii lugha zaidi ya kitu kinaitwa tense. Nakumbuka hii niliambiwa toka nikiwa darasa la sita mwaka 1997 na nilipoingia form one nikayaona. Kipindi hicho tulikuwa majirani na seminari moja ndogo (std5-7) na mara nyingi tulikutana nao hasa kwenye kushindana kuongea a.k.a debate na mara nyingi walitupa shida. Shida haswa ilitokea kwasababu wenzetu waliivishwa vizuri katika kuelewa msingi wa lugha ya kiingereza (tense).
Tukaendelea kukomaa na msingi wa kiingereza (structure) tukiwa O-Level huku tukijitutumua. Mungu si Athumani huko tukatoka na kuingia A-Level na huko HGL yangu ikaendelea kujengeka chini ya topic mpya kabisa ya Syntax. Nikiri wazi, hii ni topic mama katika maandalizi adhimu ya kuelekea kuifaulu hii lugha. Mtu akiiweza vizuri hii topic hutoweza kumsumbua sana lakini hata pale atakapokuwa ni wazi utaelewa anamudu hii lugha walau kwa kuiandika make kuongea ni majaaliwa kidogo na wepesi wa ulimi wa mhusika.
Sasa leo tunayaona, mliamua kuifumua elimu kwa kuanza na kuunganisha masomo ya sayansi O-Level, mkatoka hapo mkafuta biashara na kilimo na mkaenda Advance mkaondoa baadhi ya topic katika baadhi ya masomo hasa zile zilizoonekana kuwa tatizo. Kwenye hesabu mliondoa baadhi ya vipengele na katika kiingereza mkaondoa Syntax na sasa mnafundisha vitu vya juu juu tu na kuchora kadi za mialiko. Hivi kadi ndo mmeona jambo la maana sana? Kwa sababu hamna tense pale, lakini mnafundisha kuandika makala na kuripoti habari. Sasa huyu amabaye amekosa structure huko O-Level na Syntax huko A-Level hiyo ripoti anaenda kuiandikaje? Anaendaje kuandika makala?
Lakini huyu mtu kesho mnataka asimame aongee mbele ya watu, huyu mtu anaanzaje? Kama haitoshi, tunawaona wanaotoka vyuoni, nikiri wazi mie nakutana nayo sana haya matatizo. Kuna watu wako mpaka vyuoni wanaandika research zao na wengine tayari tunao huku mtaani makazini lakini wanashindwa hata kukokotoa sentensi moja ya maana katika Syntax yake sahihi. Akikuletea kazi yake umsaidie kuedit unaweza kushangaa unatakiwa kuedit kila neno juu ya neno ukurusa wa kwanza hadi ule wa mwisho, na mbaya kuliko unakuta huyu mtu anasoma hata masomo hayo hayo ya lugha huko chuo kama vile linguistics n.k. Kuna mda unajiuliza hivi kama hii ndio hari sawa, inakuwaje wakienda huko makazini kwao? Vipi huku maofisini?
