. Kwa maelezo yake amesema kuanzia Mei 2012 mtu yeyote atayeomba kuunganishwa na Tanesco kupata umeme, anatakiwa kupatiwa huduma hiyo ndani ya mwezi mmoja].
Kama kuanzia mwezi Mei 2012, basi tayari mwezi na ushee umeshapita. Tunataka ripoti ya utekelezaji maana Juni inakatika angalau tujue wangapi katika mwezi Mei wamehudumiwa kwa kufuata agizo la waziri. Wala hakuna haja ya kusubiri miezi tisa kama anavyopendekeza rafiki yangu. Agizo la serikali makini linatekelezeka na linatekelezwa kama lilivyotolewa na la kwake ndani ya mwezi mmoja kuanzia Mei. Hii ni Juni nayo inayoyoma! Ripoti Prof?
Kinyume cha hapo ni longolongo ileile tuliyoizoea kutoka serikali ileile inayoongozwa na chama kilekile. Tusutegemee mabadiliko. LOL!