Prof Muhongo songambele Kazi hii haina mfano

Prof Muhongo songambele Kazi hii haina mfano

Asenga wa Pakaya

JF-Expert Member
Joined
Jul 13, 2012
Posts
260
Reaction score
61
Hongera Wizara ya nishati na madini
Hongera Prof Muhongo kwa usimamizi mzuri

UJENZI WA BOMBA LETU CHINI YA BAHARI UMEKAMILIKA:

Ujenzi wa bomba la umbali wa km 5 chini ya Bahari kutoka Mnazi Bay hadi Kilindi (6 km nchi kavu kutoka Madimba patakapojengwa Processing Plant) umekamilika.

Ujenzi wa umbali wa km 25 kutoka Kisiwanii Songo Songo hadi Somanga Fungu nao umekamilika.

"Kampuni ya CCP 601 Off Shore ya China ndiyo imekamilisha kazi hizi. Nimetembelea meli (barge) iliyotumika kutandaza bomba chini ya Bahari."
S Muhongo.waziri

Kidumu.
 
Ndugu Asenga wa Pakaya nakubaliana na mtazamo wako kwa hili. Kwa kweli Prof. Muhongo na timu nzima ya Wizara wanastahili pongezi kwa usimamizi makini. Kumbe nchi hii tukiamua na kupata viongozi makini tunaweza.
 
jembe letu, hakika wapinzani hapendi hili kwa sababu watakosa cha kuongea 2015 wakati umeme utakuwa unang`ara vijijini na mjini kwa bei ndogo, tanzania yangu nakupenda, prof. Goooooooooooooooooooooooooooooooooooooooooooooooooooooooooooooo
 
kuwa fair kabisa kama mtanzania kuna mawaziri wachahce ambao wanafanya kazi .... Prof muhongo, Dr. Magufuli na Dr. Mwakyembe .... I wish wangekua wanapata budget kamili kukamilisha mipango yao

wengine wanasafiria nyota za wenzao au bora liende tu!
 
jembe letu, hakika wapinzani hapendi hili kwa sababu watakosa cha kuongea 2015 wakati umeme utakuwa unang`ara vijijini na mjini kwa bei ndogo, tanzania yangu nakupenda, prof. Goooooooooooooooooooooooooooooooooooooooooooooooooooooooooooooo

Waziri Prof. Muhongo anadhamira nzuri ya kuhakikisha kuwa sekta ndogo ya nishati inachangia maendeleo ya Tanzania na Watanzania. Zinaweza zikaweko kasoro lakini tunazingatia dhamira yake. Chapa kazi Prof. Sisi tuko nyuma yako.
 
Profesa Muhongo hamumunyi, anachapa kazi na matokeo yake yanaonekana. U-waziri wapewe technocrats na sio wanasiasa ili kazi ifanyike. Hongera Profesa, nchi yako inakushukuru.
 
Sisi huku hatuna umeme kwa siku tatu sasa, akitokea huyo Sospeter Mwongo tunamchapa bakora maana alituambia mgao utakuwa historia wakati anaingia, sasa mwaka umepita. Muhongo ni mtu wa hovyo na janga la kidunia
 
ndio waziri anayeongoza kwa jeuri na majibu ya ovyo wakati kila siku wizara yake inatukatili kwa mgao wa umeme usiotangazwa
 
uzi wa lumumba utaujua tu

Lumumba yamejaa ma Cadaver Tu,,, ndio maana badala ya kusifia kampuni iliyojenga anamsidia mtu aliye ofisini anapigwa kiyoyozi huku anasubiri rushwa na ten percent
 
ndio waziri anayeongoza kwa jeuri na majibu ya ovyo wakati kila siku wizara yake inatukatili kwa mgao wa umeme usiotangazwa

Wewe unaonekana huna cha kusema tafuta jingine , hapo serikali imepiga bao , tunasubiri umeme wa bei poa tu hapa
 
Hakuna binadamu mchapa kazi asiyekumbana na wakatisha tamaa! Ni ukweli usiopingika kuwa Mhongo ni Jembe haijawahi kutokea awamu zote kupata waziri wa nishati mchapa kazi kama Mh; Mhongo, Tofauti ndogondogo ni za kila binadamu! Lakini ukipima katika mizania ya utendaji Muhongo ni Kiboko!! Nakupa big up Uliyeleta hii maada, Wanaotukana achana nao.
 
Mpongeze pia kwa makubaliano mabovu kwenye kugawana mapato ya gesi Kati ya TPDC na statiol
 
Back
Top Bottom