Prof. Muhongo: Nitatumbua majipu tofauti na wengine

Prof. Muhongo: Nitatumbua majipu tofauti na wengine

.."Itanichukua miaka 100 kutumbua majibu kama wafanyavyo viongozi wenzangu...mimi utumbuaji wangu ni kuhakikisha huduma bora zinawafikia wananchi... - Prof. Muhongo

Anaweza kuwa na point kidogo hapa. Kudeal na ''individuals'' badala ya kujaribu ku-overhaul system yote hakutaleta tija iliyokusudiwa.
 
Tangu mpango wa tumbua majipu uanze naweza kuona tija kwa yale ya TRA na TPA. Lakini majipu ya kulazimisha na kuokoteza kwa tochi ni kupoteza muda na kutojua dira hasa ni nini. Dira kwa bandarini na TRA iko clear katika kukusanya mapato!
Mkuu,
Hata Muhimbili Hospital, Uhamiaji na kadhalika haujaona tija!
 
Nitatumbua majipu tofauti na wengine- Prof. Muhongo
Friday, February 19 2016, 0 : 0
WAZIRI wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo, amesema kazi ya kutumbua majibu inayofanywa na viongozi
wenzake serikalini, itakuwa tofauti na ile ambayo ataifanya yeye kwa kuhakikisha huduma zinawafikia wananchi.

Prof. Muhongo aliyasema hayo Dar es Salaam jana wakati akizungumza na waandishi wa habari baada ya kufungua Mkutano Mkuu wa Wawekezaji wa Nishati ya Umeme nchini.

Alisema kila mtu anastahili yake ya kufanya kazi ambapo hamu ya wananchi ni kuona Wizara yake ikitumbua majibu kama wafanyavyo viongozi wenzake lakini yeye atatumbua majipu hayo kwa staili tofauti.

"Itanichukua miaka 100 kutumbua majibu kama wafanyavyo viongozi wenzangu...mimi utumbuaji wangu ni kuhakikisha huduma bora zinawafikia wananchi.

"Mtendaji mzuri si lazima aonekane sana katika vyombo vya habari, Watanzania tunapaswa kuwa makini katika hili, lazima
viongozi wawe waangalifu tunapovitumia vyombo vya habari, jambo la msingi ni kutoa huduma," alisema.

Aliongeza kuwa, atahakikisha mikataba mipya ambayo Wizara itaingia na wawekezaji, haitakuwa na makosa na ile ya zamani, itaanza kupitiwa upya.

Prof. Muhongo alisema mikataba ambayo wameikuta ni mingi ambapo kwa mujibu wa taratibu kisheria, ipo mikataba ambayo wataipitia na kuirekebisha, mingine haitawezekana kutokana na kuheshimu mikataba hiyo.

Akizungumzia tozo za kampuni kutokana na sera mpya ya umeme, alisema Shirika la Umeme nchini (TANESCO) halitazalisha umeme pekee bali litashindana na kampuni nyingine katika uzalishaji.

"Sera mpya inasema, mtu kuzalisha umeme si lazima auziwe na TANESCO, hivi sasa kampuni zinazozalisha umeme zinaruhusiwa kumuuzia mtu yeyote bila kupitia TANESCO," alisema.

Aliongeza kuwa, TANESCO mpya itapata washindani katika uzalishaji umeme na usambazaji ili kuhakikisha Watanzania wanapata umeme kwa bei nafuu na kuwafikia kwa urahisi.

Alisema hadi sasa Watanzania asilimia 40 wanapata umeme ambapo Tanzania ikiwa nchi ya kipato cha kati, huduma hizo lazima isambae kwa asilimia 75 ambapo mpango huo utafanikiwa kutokana na kasi iliyopo katika Mradi wa Kusambaza Umeme Vijijini (REA).

Kuhusu upunguzaji bei ya umeme, Prof. Muhongo alisema Serikali imewapa jukumu la TANESCO, Baraza la Ushauri la Watumiaji wa Huduma za Maji na Nishati (EWURA), waone uwezekano wa kupunguza bei ya umeme.

"Watanzania wavumilie, kazi ya kupiga hesabu inaendelea iweze kuletwa wizarani nasi tutawaeleza maana upunguzaji bei hauwezi kufanyika kwenye jukwaa, lazima kuwepo hesabu," alisema.

Alisema tathmini inaonesha hali ya umeme nchini imeimarika ambapo TANESCO wamejitahidi na wanazidi kuimarisha upatikanaji umeme wa uhakika.
Yeye awe wazi tu, kama anaona hakubaliani na mizuka ya wenzake basi aachie tu ngazi. Kwanza ameshafuta msg aliomtumia Mama Chuwa wa WMA kwenye sent items yake??
 
Wewe ambaye siyo kipofu soma hapa kiduchu...

WAZIRI wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo, amesema kazi ya kutumbua majibu inayofanywa na viongozi
wenzake serikalini, itakuwa tofauti na ile ambayo ataifanya yeye kwa kuhakikisha huduma zinawafikia wananchi.

Prof. Muhongo aliyasema hayo Dar es Salaam jana wakati akizungumza na waandishi wa habari baada ya kufungua Mkutano Mkuu wa Wawekezaji wa Nishati ya Umeme nchini.

Alisema kila mtu anastahili yake ya kufanya kazi ambapo hamu ya wananchi ni kuona Wizara yake ikitumbua majibu kama wafanyavyo viongozi wenzake lakini yeye atatumbua majipu hayo kwa staili tofauti.

"Itanichukua miaka 100 kutumbua majibu kama wafanyavyo viongozi wenzangu...mimi utumbuaji wangu ni kuhakikisha huduma bora zinawafikia wananchi.
"Mtendaji mzuri si lazima aonekane sana katika vyombo vya habari, Watanzania tunapaswa kuwa makini katika hili, lazima
viongozi wawe waangalifu tunapovitumia vyombo vya habari, jambo la msingi ni kutoa huduma," alisema.


Ndio maana nikasema utakuwa na ukipofu uliosababishwa na ukada wa ufisiem.
 
Majipu yalioko wizara hiyo ni makubwa na sugu. Si ya saizi ya kutumbuliwa na waziri. Haya ni ya Majaliwa na Magufuli tu, kama yalivyo TRA na TPA. Wee imagine IPTL, ESCRAW, RICHMOND, DOWANS, TANESCO, EWURA, REILA etc
 
Kwa sekta ya madini ndiko balaa zaidi. Madini yanaondolewa vile ni takataka zinazotukera kukaa nazo. Huko kuna makampuni kama BARIC, BUZWAGI, NYAMHONGO, KIWIRA, MERELANI, MTWARA GAS, SONGOSONGO etc Upotevu wa mapato ktk sekta hii ni zaidi ya Shs trion moja kwa mwezi! Ndiyo rais wetu anasema Tanzania inapaswa kuwa 'a donor country' na siyo nchi ya kulilia tu misaada twa kijingajinga kama twa MCC nk.
 
"Itanichukua miaka 100 kutumbua majibu kama wafanyavyo viongozi wenzangu...mimi utumbuaji wangu ni kuhakikisha huduma bora zinawafikia wananchi.
"Mtendaji mzuri si lazima aonekane sana katika vyombo vya habari, Watanzania tunapaswa kuwa makini katika hili, lazima
viongozi wawe waangalifu tunapovitumia vyombo vya habari, jambo la msingi ni kutoa huduma," alisema.


Ndio maana nikasema utakuwa na ukipofu uliosababishwa na ukada wa ufisiem.
huyu pro hizi kauli zake zitampoza
utatoaje huduma bora huku mkiwa na mikataba ya kinyonyaji
utatoaje huduma bora huku watu
iptl wakitunyonya kupitia rugemarila na seth
ajitathmim huyu professor
 
huyu pro hizi kauli zake zitampoza
utatoaje huduma bora huku mkiwa na mikataba ya kinyonyaji
utatoaje huduma bora huku watu
iptl wakitunyonya kupitia rugemarila na seth
ajitathmim huyu professor
Kweli kabisa mkuu umetoa point za maana Sana.

kwanza Prof mkweli mwenyewe ni jipu. Je unategemea atatumbuaje majipu wakati yeye mwenyewe ni part of it. Ni sawa na kukata tawi uliloliegemea unategemea nini?!!
 
Naamin profesa akurupuki kama nyumbu wa ufipa walivyokurupuka kumpokea mamviii


unamtetea baba yako nini, maana hata yeye mwenyewe ni jipu, sasa uhalali wa kutumbua majipu mengine unatoka wapi. Ashukuru tu kwa kuwa nchi hii ni inaongozwa kiujanjaujanja mngeshamsahau kitambo
 
unamtetea baba yako nini, maana hata yeye mwenyewe ni jipu, sasa uhalali wa kutumbua majipu mengine unatoka wapi. Ashukuru tu kwa kuwa nchi hii ni inaongozwa kiujanjaujanja mngeshamsahau kitambo
Hilo ndio tatizo la vijana wa lumumba wamefungiwa kwenye kachumba na kufungwa akili kwa b7. Kama sikosei watakuwa wanaumwa ule ugonjwa wa ufisiem(kuweka akili tumboni na kufikiri kwa makalio).
 
Hizi bei zilizopo si kwasababu ya deni la serikali au? Bei tuliyokua tunalipa kabla ya serikali kukataa kulipa deni lake na kuwaambia tanesco waongeze tozo za umeme ilikua ni sh 80 kwa unit. Sasa wapige mahesabu ya nn? Kama deni limeshaisha basi warudishe bei za zamani. Haina haja ya kigugumizi hapo. Huu mzigo wa umeme mm naelekea kielemewa maana hali imekua ngumu



Kweli mkuuu umeme ni ghali alafu hauna uhakika kabisa
 
unamtetea baba yako nini, maana hata yeye mwenyewe ni jipu, sasa uhalali wa kutumbua majipu mengine unatoka wapi. Ashukuru tu kwa kuwa nchi hii ni inaongozwa kiujanjaujanja mngeshamsahau kitambo
Hivi ni nani siyo jipu, kama haki ikifuatwa? Nani hana kasoro?!

Sent from my G630-U10 using JamiiForums mobile app
 
Nimejaribu kusoma huu uzi zaidi ya mara 10 sijaona sehemu yoyote alipopinga zaidi ya kusema kila mmoja na style yake ya utumbuaji majipu.

Read between the line.
 
Tangia huyu Prof atume ile meseji kwa lile jipu ata simuelewi tena. Of course maybe tumvumilie sababu tunahitaji ujuzi wake ila otherwise huyu jamaa bado anawaza bado yupo kule kule kwenye business as usual.
 
Anaweza kuwa na point kidogo hapa. Kudeal na ''individuals'' badala ya kujaribu ku-overhaul system yote hakutaleta tija iliyokusudiwa.

Kutumbua majipu lengo lake ni kurejesha nidhamu kazini. Ukiangalia kila kitu kulikuwa hakiendi sababu kuu ni kukosekana kwa discipline kwenye shughuli zote.

Ata uwe na system zuri kiasi gani kama inasimamiwa na watu waovu hakuna jipya utafanya. Angalia mfano wa Kenya na walivyokimbilia kubadili system badala ya mindset wanalilia kupata kiongozi dizain ya Magufuli.
 
Hii nchi inahitaji uzalendo zaidi na sio porojo za siasa kwenye media, Prof anaweza kuwa na ni dhati lakn atashindwa kwa kuwa wananchi wenyewe hawajajitambua
 
Back
Top Bottom