Prof. Mbele na hoja zake: Amfagilia JK

huyu ni professa, mwendekeza tumbo! Wasomi wa namna hii ni wanafiki wanachosema ktk siasa ni tofauti na nini wanafundisha watu madarasani. hizo point alizozitoa yeye, ukiandika esay kwenye term paper yake unafeli takuuliza substance ziko wapi? mbona hoja hafifu? Mambo ya REDET hayo, wanaboa
 
Hamna lolote la maana la kumsadia mtz wa kawaida aliloliandika na bado siamini kama uchambuzi huu kuhusu JK umetoka kwa Profesa wa elimu ya magharibi;Kwa haraka haraka ukisoma utahisi labda umetoka kwa Professor wa miti shamba!

Nilichokiona hapo Professor Mbele likely kama anataka kurudi TZ na sasa anaanza kujijengea mazingira ya ajira hasa akikumbuka yaliyompata comrade mwenzake Baregu!
 
Prof. Mbele!

Uchambuzi wako ni dhaifu, ni vizuri umesema ni uonavyo wewe lakini naweza kusema ubora wa JK umeupima kwa kigezo kimoja tu ambayo ni safari za nje, kwamba watanzania walioko nje hawajatumia vizuri fursa alizo-create JK well huko ndiko kushindwa kwenyewe kwanini hawazitumia?? ina maana hawazioni? kama hawazioni something is wrong with JK ambaye alitaka fursa hizo watu waone ..wa-revist hiyo strategy...

Pili, Ubora wa JK umepungua kwasababu ya ukubwa wa serikali yake, mawaziri chini ya kiwango katika kusimamia na kubuni miradi mbalimbali ultimately yeye mwenyewe ni weak

Tatu, anajipendekeza sana kwa jamii fulani fulani hapa home amewapa vyeo dezo dezo lakini hawaishi kulia lia na kuhitaji kupendelewa zaidi, ameshindwa kuwakemea wanaoleta waraka feki na kugawa jamii pamoja na kwamba wamejazwa serikalini katika teuzi zake..shame on them!

Nne, utekelezaji hafifu wa kazi za serikali (hapa naongelea ofisi ya PM ni very slow nafikiri ameezeka huyu mtoto wa mkulima akili iko slow kufuatilia shughuli za serikali hakuna tena mabadiliko au ubunifu ni mambo yaleyale tumechoka!

Tano, Usimamizi mbovu wa rasimali za umma kila wizara kuanzia samaki, madini, ardhi atcl,trl bandari, TRA...etc mambo shaghalabaghala hakuna innovations walau mtanzania akajivunia

Upimaji wa ubora wa JK uzingatie vitu vyote siyo hoja moja tu Prof. Mbele...
 
Huyu mtu anaheshima zake kuwa sana katika chuo huku America na pia ni mzuri sana katika English sana

Mkuu kuheshimika America does not make his judgement right. We see things on the ground, Yeye yuko America huko sisi tuko Tanzania tunajionea yanayoendelea hapa, uzuri kwenye english hauna maana ya uwezo mkubwa wa kuona yale wengine hawaoni. I can guess that we probably can see what he can't, and may be he as seen what we have not. Angetuambia ni nini hicho ambacho hatujakiona may be tungemwelewa.
 
Huyu mtu anaheshima zake kuwa sana katika chuo huku America na pia ni mzuri sana katika English sana


So akijua kiingereza sana inatosha apewe heshima? Nani utakayempa nafasi ya kukaa katika kundi la waozungumza english 24hrs in a year asiongee kiingereza kizuri?

Prof Mbele namweshimu sana, lakini naona aotusema tuna majadiliano ya kichama yeye amejiwekaje totauti na hilo?

Naomba Prof atueleze nini hicho kizuri JK alichokianzisha nje ya nchi, maana nasi tuko huko huko hatujaona chochote...au ni kwa kuwa hatujakutana na SElebrities as JK crosed over from Tr and Tobago to meet them in the US?

JK has done nothing to be praised. Since he came into power, UMASKINI UMEONYESHA MAKUCHA, RUSHWA KUBWA ZIMETAWALA KWA KUWA HAWEZI KUMYOOSHEA KIDOLE ALIEMSUPPORT, YUKO NA VIHIYO KWENYE CABINET HATHUBUTU KUWAULIZA DIGREE ZAO WAMEPATA WAPI...ETC

Laiti kama JK angetekeleza walao machache aliyoyataja kwenye ile speech yake ya kusisimua "aliyoisoma" bungeni in first days.....ila hatukutarajia kubwa maana alisoma speech iliyoandokwa na waandishi wazuri na sio comitment...

Prof Mbele, utazaraulika sana..acha kabisa...politcs sio game yako....wewe fundisha vijanaaaa
 
Huyu ni mpuuzi tu kama wengine tuliwahi kuwasikia.

Sasa badala kuchukua fursa hiyo kuelezea 'ubora wa JK' anaelezea suala la watz walio nje wanavyoshindwa kuwekeza..Hawa ndio wasomi wa kitanzania..Phew!
 
Maoni yake...nanyi si mna yenu? Critics, critics! Ni huyu JK akitoka madarakani mtaanza kumsifia kama mfanyavyo kwa Mkapa sasa. Kwani enzi za ukandamizaji wa Mkapa watu mlikuwa mnaponda mpaka wengine mkafutiwa uraia.

Prof anayohaki ya kusema aonanvyo yeye, kitendo cha baadhi yenu kuanza kumponda si cha uungwana. Wengine mkiulizwa umelifanyia nini taifa, utasema nimelipigia mayowe pale JF! JK si mbaya kama wengi wa JF members wanavyo muelezea. Kumbuka wote tunaowajibu wakulifanyia taifa kitu, si rais pekee, japo yeye ni kiongozi.
"Huyu ni mpuuzi tu kama wengine tuliwahi kuwasikia."-Maneno kama haya aliyosema Abdulhalim hapo juu si ya kiungwana hata kidogo.
 
hivi kumbe ni prof wa kiingereza, basi ni vizuri akaendelea na na kuchambua na kuandika mada kuhusu hiyo lugha, maana kwa u-prof wake naona yuko too shalow kuongelea mambo mengine ya kijamii, kama siasa? ingwa ma-prof wengine ingwa wanaweza kuwa sio wa fani inayo jadiliwa lakini kutokana na kuwa na background nzuri au tuseme upeo utakuta ujengaji hoja wao ni mzuri, huyu inafaa nimpe mtoto wangu amfundishe kiingereza.
 
Huyo prof. nadhani ameanza mbio za october 2010 huko jimboni kwao,na kaona hapo ndio pa kuanzia.
 
Kuwajumlisha wapinzani katika tume kama ile ya kuchunguza mikataba au tuhuma za kashfa ni ishara ya kuwa Rais Kikwete anatambua kuwa suala la maslahi ya Taifa ni suala la wote, si la chama tawala tu.

......Mbona JK hajumuishi wapinzani katika TUME YA UCHAGUZI?
 
Namtetea Profesa Joseph Mbele

Niliona humu ukumbini yametundikwa mawazo ya Profesa Mbele. “ Wengi Waanza Kuona Ubora Wa JK”. Yalikuwa ni maoni binafsi ya Profesa Mbele. Wengi wamechangia na wanaendelea kuchangia. Nami nitachangia pia. Nimepata bahati ya kukutana na kuongea na Profesa Mbele kwa simu na ana kwa ana . Ni pale aliporudi nyumbani Tanzania mwaka jana.

Naweza kusema nimemfahamu Profesa Mbele kupitia maandiko yake kwa maana ya makala zake anazozituma KWANZA JAMII na pia nilipoongea nae na kumsikia anavyoelezea mitazamo yake juu ya masuala mbali mbali ya nchi aliyozaliwa, Tanzania. Kwamba Profesa Mbele ni mtaalamu wa lugha ya Kiingereza haina maana hana anachokijua kuhusiana na nchi yake Tanzania na ulimwengu kwa ujumla.

Ni dhahiri kuna wanaotishika wanaposikia mtu anaitwa ‘ Profesa fulani’. Na kuna anayejisikia raha anaporudi nyumbani na kumwambia mumewe au mkewe; “ Kuna jamaa kule JF anaitwa Profesa Mbele, kaja na hoja zake za kipumbavu, nimempa maneno yake, mpuuzi mkubwa!”

Aliyempa Profesa Mbele ‘maneno yake’ huenda ana hitaji la kupunguza hasira zake, msongo wake wa mawazo. Kama hilo linamsaidia ni jambo la heri. Lakini bahati mbaya si wengi wako kama Profesa Mbele. Yeye atasoma na atalifahamu hilo, wala hutamwona akirudi na kujibu kwa hasira.

Ukikutana na Profesa Mbele huwezi kumsikia akitamka neno ‘Profesa’. Kwa Profesa Mbele ‘ sina hata ya kujisikia kuwa mimi ni sawa na ‘Mwalimu wa Zamu’ Shule ya Sekondari Changanyikeni. Profesa Mbele hana makuu. Ni mwalimu na bado ana kiu ya kujifunza. Anajiamini. Si mwanachama wa chama cha siasa hapa Tanzania. Anaipenda Tanzania na anajisikia huru kuchangia fikra zake. Hana sababu za kuficha jina lake. Na katika hilo, Profesa Mbele na mimi tuna mitazamo sawa. Binafsi sioni tatizo kuandika maoni yangu. Naandika kwa uhuru . Sina chama na sina sababu ya kuficha jina langu kwa fikra zangu ninazozitoa hadharani. Mwenye kuzipinga, ruksa, azipinge kwa hoja, ni muhimu. Na mengine niandikayo yaweza kuwa ya kipuuzi, najua, maana mimi si malaika. Kuna watakayekubaliana na hoja zangu, na kuna watakaosema; “ Sasa mshenzi huyu atakiona cha mtema kuni”. Watanishambulia mimi binafsi hata kwa matusi ya nguoni. Nimeshazoea. Ukichagua mchezo wa masumbwi, usiogope ngumi za usoni!

Tujitahidi kujenga mazoea ya kuikabili hoja inayowasilishwa na si kumkabili mwasilisha hoja. Mathalan, Profesa Mbele yeye kwa mtazamo wake anaona kuwa JK ameonyesha ubora kama kiongozi. Ni mtazamo wake. Wengine tuje na mitazamo yetu kwa kupinga au kuunga mkono hoja zake. Si busara kuanza kumvamia Profesa Mbele na kwa kutumia lugha zisizo za kiungwana . Na wanaofanya hivyo baadhi yao ni waoga kwa vile hawatumii hata majina yao halisi.

Daima tupiganie ‘ Neno huru’. Uhuru wa kila mmoja wetu kutoa maoni yake. Tujiadhari tusije tukatumia majukwaa haya kukandamiza fikra huru. Si kwa bastola na pingu, bali kwa kalamu zetu. Tujiulize; ni Maprofesa wangapi wa Kitanzania wanaojitokeza kwa majina yao kuchangia fikra zao katika majukwaa ya wazi ya kijamii?

Na kama asememavyo Profesa Mbele Mwenyewe; “ Kuona mazuri ya JK kama kiongozi, kwa upande wangu, si sawa na kuipigia debe CCM. Tangu CCM ianze, nimekuwa nikiishutumu kwa namna mbali mbali, tena kimaandishi, ili kila mtu asome. Nimechapisha hata kitabu, wiki chache zilizopita, ambamo nimeendelea kuishutumu CCM.

Tatizo la waTanzania wengi ni ufinyu wa mawazo. Kwa vile wamezama mno katika siasa za vyama, wanayachukulia masuala kwa mtazamo wa kichama. Ukisema hivi, wanaangalia unaunga mkono chama gani. Ukisema vile, wanaangalia kwa mtazamo wa chama fulani. Ukweli ni kuwa mimi si mwanachama wa chama chochote. Nina uhuru wa kusema chochote ninachofikiri, hata kama kinawaudhi watu wa chama fulani. Shauri lao na siasa zao za ufinyu na ukandamizaji wa fikra kwa maslahi ya chama.
” Profesa Mbele.

Nawasilisha.

Maggid

‘ Mwalimu Wa Zamu’.
Tembelea: http://mjengwa.blogspot.com
 
Sasa wewe kwanini uwe proxy wake?? Kwanini usimlete mwenyewe humu JF na kujibu hoja??
 
Nina uhuru wa kusema chochote ninachofikiri, hata kama kinawaudhi watu wa chama fulani. Shauri lao na siasa zao za ufinyu na ukandamizaji wa fikra kwa maslahi ya chama.”

Ni uhuru huo huo unaotumiwa na wanaoipinga hoja yako!
 
Ndio Maprofessor wa TZ walivyo...list is full with their "big" Cvs. Lakini bado najiuliza, mbona sioni mchango wao katika kulinasua Taifa huku tuliko? Well, Rais anajukumu zito la kuivusha nchi kwenda eneo salama. Uzuri wa Rais kwa nchi maskini kama yetu sio ukarimu na uwezo wake wa kuzunguka dunia hii akiomba kusaidiwa. Lini atatuonyesha kwamba dawa ya kuondokana na adha ya umaskini ni kufanya kazi kwa bidii na kuondoa dhana ya kwamba hatuwezi kufanya lolote bila msaada wa kina mjomba ambao hawaaminiki?
 
Tatizo ni kuwa ameenda kutafuta Milioni 20 ambazo tunazipata kwa masharti na masimango kibao na kaacha kufanya kazi nzito na kukusanya hizo milioni 20 hapahapa Tanzania.

Umatonya ni too much na mtu anayekaa na kusifia umatonya kwa kweli ni kichekesho. Toa sadaka ameni, na bahati mbaya watoa sadaka wenyewe hata dini hawaamini. Wao hapendwi mtu ila pesa.

Huyu Jk si aliwahi kusema hajui ni kwa nini TZ ni maskini!

Aliambiwa bajeti ya nchi ina pesa za wafadhili zaidi ya 40%, unatafuta msaada ili ifikie kiasi gani? Hakuwa na jibu.

Jamaa ni mpenzi wa kuzunguka tu na ninaamini hata alipokuwa hana madaraka, lazima alikuwa hatulii nyumbani.
 
Namtetea Profesa Joseph Mbele

Niliona humu ukumbini yametundikwa mawazo ya Profesa Mbele. " Wengi Waanza Kuona Ubora Wa JK". Yalikuwa ni maoni binafsi ya Profesa Mbele. Wengi wamechangia na wanaendelea kuchangia. Nami nitachangia pia. Nimepata bahati ya kukutana na kuongea na Profesa Mbele kwa simu na ana kwa ana . Ni pale aliporudi nyumbani Tanzania mwaka jana.

Naweza kusema nimemfahamu Profesa Mbele kupitia maandiko yake kwa maana ya makala zake anazozituma KWANZA JAMII na pia nilipoongea nae na kumsikia anavyoelezea mitazamo yake juu ya masuala mbali mbali ya nchi aliyozaliwa, Tanzania. Kwamba Profesa Mbele ni mtaalamu wa lugha ya Kiingereza haina maana hana anachokijua kuhusiana na nchi yake Tanzania na ulimwengu kwa ujumla.

Ni dhahiri kuna wanaotishika wanaposikia mtu anaitwa ' Profesa fulani'. Na kuna anayejisikia raha anaporudi nyumbani na kumwambia mumewe au mkewe; " Kuna jamaa kule JF anaitwa Profesa Mbele, kaja na hoja zake za kipumbavu, nimempa maneno yake, mpuuzi mkubwa!"

Aliyempa Profesa Mbele ‘maneno yake' huenda ana hitaji la kupunguza hasira zake, msongo wake wa mawazo. Kama hilo linamsaidia ni jambo la heri. Lakini bahati mbaya si wengi wako kama Profesa Mbele. Yeye atasoma na atalifahamu hilo, wala hutamwona akirudi na kujibu kwa hasira.

Ukikutana na Profesa Mbele huwezi kumsikia akitamka neno ‘Profesa'. Kwa Profesa Mbele ' sina hata ya kujisikia kuwa mimi ni sawa na ‘Mwalimu wa Zamu' Shule ya Sekondari Changanyikeni. Profesa Mbele hana makuu. Ni mwalimu na bado ana kiu ya kujifunza. Anajiamini. Si mwanachama wa chama cha siasa hapa Tanzania. Anaipenda Tanzania na anajisikia huru kuchangia fikra zake. Hana sababu za kuficha jina lake. Na katika hilo, Profesa Mbele na mimi tuna mitazamo sawa. Binafsi sioni tatizo kuandika maoni yangu. Naandika kwa uhuru . Sina chama na sina sababu ya kuficha jina langu kwa fikra zangu ninazozitoa hadharani. Mwenye kuzipinga, ruksa, azipinge kwa hoja, ni muhimu. Na mengine niandikayo yaweza kuwa ya kipuuzi, najua, maana mimi si malaika. Kuna watakayekubaliana na hoja zangu, na kuna watakaosema; " Sasa mshenzi huyu atakiona cha mtema kuni". Watanishambulia mimi binafsi hata kwa matusi ya nguoni. Nimeshazoea. Ukichagua mchezo wa masumbwi, usiogope ngumi za usoni!

Tujitahidi kujenga mazoea ya kuikabili hoja inayowasilishwa na si kumkabili mwasilisha hoja. Mathalan, Profesa Mbele yeye kwa mtazamo wake anaona kuwa JK ameonyesha ubora kama kiongozi. Ni mtazamo wake. Wengine tuje na mitazamo yetu kwa kupinga au kuunga mkono hoja zake. Si busara kuanza kumvamia Profesa Mbele na kwa kutumia lugha zisizo za kiungwana . Na wanaofanya hivyo baadhi yao ni waoga kwa vile hawatumii hata majina yao halisi.

Daima tupiganie ' Neno huru'. Uhuru wa kila mmoja wetu kutoa maoni yake. Tujiadhari tusije tukatumia majukwaa haya kukandamiza fikra huru. Si kwa bastola na pingu, bali kwa kalamu zetu. Tujiulize; ni Maprofesa wangapi wa Kitanzania wanaojitokeza kwa majina yao kuchangia fikra zao katika majukwaa ya wazi ya kijamii?

Na kama asememavyo Profesa Mbele Mwenyewe; " Kuona mazuri ya JK kama kiongozi, kwa upande wangu, si sawa na kuipigia debe CCM. Tangu CCM ianze, nimekuwa nikiishutumu kwa namna mbali mbali, tena kimaandishi, ili kila mtu asome. Nimechapisha hata kitabu, wiki chache zilizopita, ambamo nimeendelea kuishutumu CCM.

Tatizo la waTanzania wengi ni ufinyu wa mawazo. Kwa vile wamezama mno katika siasa za vyama, wanayachukulia masuala kwa mtazamo wa kichama. Ukisema hivi, wanaangalia unaunga mkono chama gani. Ukisema vile, wanaangalia kwa mtazamo wa chama fulani. Ukweli ni kuwa mimi si mwanachama wa chama chochote. Nina uhuru wa kusema chochote ninachofikiri, hata kama kinawaudhi watu wa chama fulani. Shauri lao na siasa zao za ufinyu na ukandamizaji wa fikra kwa maslahi ya chama.
" Profesa Mbele.

Nawasilisha.

Maggid

' Mwalimu Wa Zamu'.
Tembelea: http://mjengwa.blogspot.com

Ndugu Maggid,

Awali niliposoma kichwa cha habari kuwa unamtetea Profesa Mbele nilidhani utakwenda moja kwa moja kwenye hoja iliyofanya baadhi ya wana-JF wapingane nae in the first place.Lakini kwa bahati mbaya,au makusudi,umeamua kukumbatia utamaduni wa kuangalia haiba ya mtu badala ya hoja husika.

Naomba pia kutokubaliana nawe katika hoja yako kuwa "tatizo la Watanzania wengi ni ufinyu wa mawazo".Hivi una takwimu zozote za kusapoti hitimisho hilo?Ufinyu huo ni pale wanapokosolewa akina Profesa mbele pekee au kwenye kila suala?Hivi hapa Jamii Forums,michango ya maana inayotolewa pale inawekwa na wageni au Watanzania hao "wengi wenye ufinyu wa mawazo"?Na pengine la muhimu zaidi,inakuwaje akina Mjengwa na Profesa Mbele ambao ni Watanzania wenzetu hawako kwenye kundi hilo la wenye ufinyu wa mawazo?

Unatetea uhuru wa Profesa Mbele kutoa mawazo yake halafu wakati huohuo unakwaza uhuru wa wasioafikiana na mtizamo wake.Naamini kabisa kuwa laiti Profesa Mbele angeungwa mkono usingekuja na hitimisho la "dharau" kuwa Watanzania wengi wana ufinyu wa mawazo.

Pengine kabla ya kukimbilia kumtetea "rafiki yako Profesa Mbele" ungefanya utafiti mdogo tu kwanini kumejitokeza upinzani kwenye hoja yake kuhusu JK.Kukurahishia,ukweli ni kwamba hoja yake sio tu unpopular bali ilikosa hoja za msingi zinazotarajiwa kutoka kwa mwanazuoni kama yeye.Hapa JF kuna baadhi ya wana-forums wanaotoa hoja za ajabu kabisa lakini mara nyingi zinaishia kupuuzwa na wachache.Sababu ya kupuuzwa huko au kupingwa na wachache ni ukweli kuwa wana-forums hawajua uwezo wa akili na kiuchambuzi wa mwandishi husika.Ila kwa Profesa Mbele,sote tunafahamu kuwa ni mwanazuoni aliyebobea,na tuna matarajio makubwa kutoka kwake.

Wana-JF waliohoji usomi wa Profesa Mbele walikuwa na haki na uhuru wa kufanya hivyo kama ilivyokuwa kwa Profesa Mbele kutoa hoja yake hiyo unpopular.Tukienda mbele zaidi ya suala la haki na uhuru,ni dhahiri kuwa laiti hoja ya Profesa ingeendana na hali halisi basi kusingekuwa na ukosoaji uliojitokeza.

Na wakati unawakosoa wakosoaji wa Profesa Mbele unasahau kuwa Profesa nae ni mahiri wa kuwakosoa Watanzania wenzake kuhusu "uvivu wa kufikiri" au "ufinyu wa mawazo" (angalau wewe umesema "Watanzania wengi" badala ya kusema "Watanzania" ikimaanisha "wote").Uhuru ni sawa na barabara yenye pande mbili: heshimu uhuru wangu,nami niheshimu wako.

Mwisho,mnapoamua kuweka mawazo yenu hadharani msitarajie kuungwa mkono pekee.Hata kama mawazo yenu yangekuwa sahihi kila wakati bado kungewepo uwezekano wa baadhi ya wasomaji kutoafikiana nanyi.Ndio wanasayansi wa jamii wanachoita point of view.Atakayeafikiana nanyi atawaunga mkono na hata kuwapongeza,atakaetofautiana nanyi atawapinga au kuwakosoa.Hilo la kujadili mtu badala ya hoja si mwafaka lakini si la ajabu kwa vile hata waandishi mahiri kama wewe Mjengwa umeangukia kwenye mtego huohuo wa kuwashutumu watu (Watanzania wengi wenye ufinyu wa mawazo) badala ya kuangalia mantiki ya hoja zao.Na badala ya kuangalia kwanini "wenye ufinyu wa mawazo" wamempinga Profesa mbele,mwenzetu unatuletea habari za haiba ya Profesa Mbele!
 
Namtetea Profesa Joseph Mbele

Niliona humu ukumbini yametundikwa mawazo ya Profesa Mbele. " Wengi Waanza Kuona Ubora Wa JK". Yalikuwa ni maoni binafsi ya Profesa Mbele. Wengi wamechangia na wanaendelea kuchangia. Nami nitachangia pia. Nimepata bahati ya kukutana na kuongea na Profesa Mbele kwa simu na ana kwa ana . Ni pale aliporudi nyumbani Tanzania mwaka jana.

Naweza kusema nimemfahamu Profesa Mbele kupitia maandiko yake kwa maana ya makala zake anazozituma KWANZA JAMII na pia nilipoongea nae na kumsikia anavyoelezea mitazamo yake juu ya masuala mbali mbali ya nchi aliyozaliwa, Tanzania. Kwamba Profesa Mbele ni mtaalamu wa lugha ya Kiingereza haina maana hana anachokijua kuhusiana na nchi yake Tanzania na ulimwengu kwa ujumla.

Ni dhahiri kuna wanaotishika wanaposikia mtu anaitwa ' Profesa fulani'. Na kuna anayejisikia raha anaporudi nyumbani na kumwambia mumewe au mkewe; " Kuna jamaa kule JF anaitwa Profesa Mbele, kaja na hoja zake za kipumbavu, nimempa maneno yake, mpuuzi mkubwa!"

Aliyempa Profesa Mbele ‘maneno yake' huenda ana hitaji la kupunguza hasira zake, msongo wake wa mawazo. Kama hilo linamsaidia ni jambo la heri. Lakini bahati mbaya si wengi wako kama Profesa Mbele. Yeye atasoma na atalifahamu hilo, wala hutamwona akirudi na kujibu kwa hasira.

Ukikutana na Profesa Mbele huwezi kumsikia akitamka neno ‘Profesa'. Kwa Profesa Mbele ' sina hata ya kujisikia kuwa mimi ni sawa na ‘Mwalimu wa Zamu' Shule ya Sekondari Changanyikeni. Profesa Mbele hana makuu. Ni mwalimu na bado ana kiu ya kujifunza. Anajiamini. Si mwanachama wa chama cha siasa hapa Tanzania. Anaipenda Tanzania na anajisikia huru kuchangia fikra zake. Hana sababu za kuficha jina lake. Na katika hilo, Profesa Mbele na mimi tuna mitazamo sawa. Binafsi sioni tatizo kuandika maoni yangu. Naandika kwa uhuru . Sina chama na sina sababu ya kuficha jina langu kwa fikra zangu ninazozitoa hadharani. Mwenye kuzipinga, ruksa, azipinge kwa hoja, ni muhimu. Na mengine niandikayo yaweza kuwa ya kipuuzi, najua, maana mimi si malaika. Kuna watakayekubaliana na hoja zangu, na kuna watakaosema; " Sasa mshenzi huyu atakiona cha mtema kuni". Watanishambulia mimi binafsi hata kwa matusi ya nguoni. Nimeshazoea. Ukichagua mchezo wa masumbwi, usiogope ngumi za usoni!

Tujitahidi kujenga mazoea ya kuikabili hoja inayowasilishwa na si kumkabili mwasilisha hoja. Mathalan, Profesa Mbele yeye kwa mtazamo wake anaona kuwa JK ameonyesha ubora kama kiongozi. Ni mtazamo wake. Wengine tuje na mitazamo yetu kwa kupinga au kuunga mkono hoja zake. Si busara kuanza kumvamia Profesa Mbele na kwa kutumia lugha zisizo za kiungwana . Na wanaofanya hivyo baadhi yao ni waoga kwa vile hawatumii hata majina yao halisi.

Daima tupiganie ' Neno huru'. Uhuru wa kila mmoja wetu kutoa maoni yake. Tujiadhari tusije tukatumia majukwaa haya kukandamiza fikra huru. Si kwa bastola na pingu, bali kwa kalamu zetu. Tujiulize; ni Maprofesa wangapi wa Kitanzania wanaojitokeza kwa majina yao kuchangia fikra zao katika majukwaa ya wazi ya kijamii?

Na kama asememavyo Profesa Mbele Mwenyewe; " Kuona mazuri ya JK kama kiongozi, kwa upande wangu, si sawa na kuipigia debe CCM. Tangu CCM ianze, nimekuwa nikiishutumu kwa namna mbali mbali, tena kimaandishi, ili kila mtu asome. Nimechapisha hata kitabu, wiki chache zilizopita, ambamo nimeendelea kuishutumu CCM.

Tatizo la waTanzania wengi ni ufinyu wa mawazo. Kwa vile wamezama mno katika siasa za vyama, wanayachukulia masuala kwa mtazamo wa kichama. Ukisema hivi, wanaangalia unaunga mkono chama gani. Ukisema vile, wanaangalia kwa mtazamo wa chama fulani. Ukweli ni kuwa mimi si mwanachama wa chama chochote. Nina uhuru wa kusema chochote ninachofikiri, hata kama kinawaudhi watu wa chama fulani. Shauri lao na siasa zao za ufinyu na ukandamizaji wa fikra kwa maslahi ya chama." Profesa Mbele.

Nawasilisha.

Maggid

' Mwalimu Wa Zamu'.
Tembelea: http://mjengwa.blogspot.com
Lugha ya kiswahili imeshehena maneno mengi ya Busara ambayo tunajitahidi kuwapatia watoto wetu maarifa wangali wadogo, hivyo wewe na Prof nafikiri mlipitia hizo shule na hili neno dogo tu lakini lenye maana kubwa tu nalo ni "kizuri cha jiuza, kibaya cha jitembeza" Sasa sijui kama nchi ya tanzania inatakiwa ijitembeza kama zuzu au ijituze/tuwekeze kwenye vitu vya muhimu ili tuongeze thamani ya nchi yetu/ubora/uzuri nk na jambo ambalo mimi naona linafaa zaidi ya kwenda wall street nk , ni kuwa na utawala bora, unafuata sheria, kuwekeza kwenye miundo mbinu na nishati , elimu bora sio bora elimu, hivi vingine vitakuja kama utitiri wawe wawekezaji , watalii nk mpaka hata kudengua tutadengua kwamba kwa kuongeza vigezo vya huyu mwenye kumtaka mwari "Tanzania" lakini tukiendelea na vituko vya Richmond, RITEs/TRL, ATCL , waaalimu wa VODA faster , tutawapata wawekezaji wanaokuja na brief case tupu na kuondoka na mamilioni, wakati makazi ya Kalenga nk yanazidi kudidimia.
naama ndimi wako sio Prof lakini hivyo uwezo wangu wa kujieleza na kujadili maada sio kama wa Prof wa New York anaye wafundisha Wamerekani. na kutambulika Dunia Thima

Mwenye macho haambiwi .........tazama maana kesha ona potential za kila mahali ancho hitaji ni vitu vitakavyo wezesha biashara/shughuli zake, ukiona tofauti ya hiyo ujue kuna tatizo.
 
Mkuu Majid,
Huyu ni prof mzima ambaye nilitegemea anapoandika sifa za JK ataziweka ktk maandishi makubwa yaani lugtha ambayo kila mtanzania angeeelewa... lakini nimsomapo anakuwa kama vile anaunganisha hoja. Hakuna mahala amezungumza kwa nguvu ya elimu yake isipokuwa kuchapia chapia kana kwamba tunamsoma Mkandara alosomea madrasa!...

Hivyo unapojitangaza kama Profesa ni muhimu sana ujenge hoja zinazolinganalaa sivyo ndio matokeo yake yanakuwa kama hivi. Nina hakika kabisa kama leo hii mimi nikiamua kumsifia JK nitakuwa na mazito zaidiyenye kuwalenga wananchi na sii kuchapia chapia..
Hii ndio wasiwasi ya wengi ktk uandishi wa mkuu wetu pengine swala la kuandika Kiswahili ndio limemshinda, unajua tena wasomi wetu wazuri sana ktk nyanja walizosomea ukimtoa nje ya darasa umemmaliza!
 
Hiii kweli iliandikwa Na Professor....Leo ni miaka nane Ila andiko linaishi.hebu wapinzani wenzangu , rudin tuedit comment zetu.....
 
Back
Top Bottom