Prof. Lipumba na mbio za Urais

Prof. Lipumba na mbio za Urais

DCONSCIOUS

JF-Expert Member
Joined
Oct 4, 2010
Posts
1,269
Reaction score
473
Tuikiwa tunaelekea kumpata mgombea wa urais kwa tiketi ya UKAWA naomba niongee machache juu ya kile kinacho endelea ndani ya UKAWA .Kikubwa ni nachotaka kuzungumza ni juu ya Prof lipumba na chama chake kuiga yale yanayo fanywa na vyama vingine bila kuangalia madhara yake au muendelezo wake. Ngoja niwakumbushe kidogo mwaka 2012 pale chama cha demokrasia na maendeleo chadema kilipo kua kina endeleza operation yake ya M4C yaani Movement for Change, mikoa ya kusini ndipo chama cha wananchi CUF walikasirika na kuhisi wamevamiwa kwenye ngome yao hali iliyo wapelekea na wao kuzindua operation yao waliyo ipa jina la Vision for change (V4C). Nilifurahishwa sana na operation ya CUF niliamini chama kimezinduka kutoka usingizini. Lakini nilishituka hasa baada ya kupata taarifa kutoka ndani ya chama hicho kwamba lengo lilikua kuwajibu chadema walio vamia kile wanacho kiita ngome yao . Hivyo operation ya CUF ililenge mkoa wa Arusha waliio amini ni ngome ya Chadema.Baada ya hapo wakarudi Mtwara na Lindi na ndipo operation yao ilipo fia.Sina tatizo sana na mipango ile ya CUF. Lakini pia naamini umoja wa katiba ya wananchi (UKAWA) ulilenga kufuta tofauti zilizo kuwepo kati ya vyama vikubwa vya upinzani. Nakuvifanya viwe imara zaidi kupambana na CCM .Nimeshituka zaidi baada ya kusikia kua Prof Lipumba anataka kutangaza nia kama walivyo fanya wagombea wa ccm yaani kwa mbwembwe nyingi . Huku akijua kua UKAWA hawajampitisha mgombea wa nafasi hiyo. Lengo kubwa ni kuwaaminisha wanachama wa CUF kua yeye ni bora zaidi ya wengine ndani ya UKAWA hivyo hakuna anae stahili kupitishwa zaidi yake.Inawezekama ikawa kweli yeye akawa bora zaidi ya wegine. Lakini je njia anayo tumia ni si sahihi. Wote tunajua kua prof Lipumba ni mtaaramu wa uchumi. Hivyo anataka kutumia hicho kama kigezo cha kuteuliwa na UKAWA. Inawezekana kikawa nikigezo lakini kwa siasa za Tanzania kigezo cha utaaram wa uhumi kinatosha kumfanya awe Rais?. Hajiulizi kwamba kwanini pamoja na uprofesa wake lakini amegombea urais kalibia mala nne, lakini zote ameshidwa na kura zinazidi kupungua. Hivi ni muujiza gani anao utegemea utakao mfanya mwaka huu ashinde, ikiwa chama chake kimeishia kufanya mikutano Lindi, Mtwara na Tabora tu? Hata mikoa ya pwani tuliyo aminishwa kua ni ngome yao kama Tanga wamshindwa kabisa kujijenga.Chama kina majimbo mawili tu huku bara, lakini prof anataka agombee yeye. Kwa harakati zipi walizo zifanya na chama chake mpaka tuamini ataweza kushinda na kuwauza wagombea wa ukawa?. Wenzenu chadema wakiwa wana zunguka nchi nzima kujenga chama chao, nyinyi mnabaki ofisini kutoa matamko alfu mnataka . mgombea wenu apitishwe kugombea urais. Toka uchaguzi wa mwaka 2010 Profesa hajawai kanyaga mkoa wowote wa nyanda za juu kusini au kanda ya ziwa kwa ajiri ya kujenga chama lakini leo anataka apewe nafasi. Nakumbuka siku David Kafulila alipo pendekeza Dr Slaa awe mgombea wa UKAWA hao hao CUF walikuja juu na kudai amevunja taratibu . https://www.jamiiforums.com/jukwaa-...igawa-ukawa-zinazofanywa-na-wana-ukawa-9.html. lakini cha ajabu wanashindwa kumlaani prof lipumba anae fanya yaleyale waliyo kua wanamlaumu kafulila aliye toa maoni yake tu.
 
Tuikiwa tunaelekea kumpata mgombea wa urais kwa tiketi ya UKAWA naomba niongee machache juu ya kile kinacho endelea ndani ya UKAWA .Kikubwa ni nachotaka kuzungumza ni juu ya Prof lipumba na chama chake kuiga yale yanayo fanywa na vyama vingine bila kuangalia madhara yake au muendelezo wake. Ngoja niwakumbushe kidogo mwaka 2012 pale chama cha demokrasia na maendeleo chadema kilipo kua kina endeleza operation yake ya M4C yaani Movement for Change, mikoa ya kusini ndipo chama cha wananchi CUF walikasirika na kuhisi wamevamiwa kwenye ngome yao hali iliyo wapelekea na wao kuzindua operation yao waliyo ipa jina la Vision for change (V4C). Nilifurahishwa sana na operation ya CUF niliamini chama kimezinduka kutoka usingizini. Lakini nilishituka hasa baada ya kupata taarifa kutoka ndani ya chama hicho kwamba lengo lilikua kuwajibu chadema walio vamia kile wanacho kiita ngome yao . Hivyo operation ya CUF ililenge mkoa wa Arusha waliio amini ni ngome ya Chadema.Baada ya hapo wakarudi Mtwara na Lindi na ndipo operation yao ilipo fia.Sina tatizo sana na mipango ile ya CUF. Lakini pia naamini umoja wa katiba ya wananchi (UKAWA) ulilenga kufuta tofauti zilizo kuwepo kati ya vyama vikubwa vya upinzani. Nakuvifanya viwe imara zaidi kupambana na CCM .Nimeshituka zaidi baada ya kusikia kua Prof Lipumba anataka kutangaza nia kama walivyo fanya wagombea wa ccm yaani kwa mbwembwe nyingi . Huku akijua kua UKAWA hawajampitisha mgombea wa nafasi hiyo. Lengo kubwa ni kuwaaminisha wanachama wa CUF kua yeye ni bora zaidi ya wengine ndani ya UKAWA hivyo hakuna anae stahili kupitishwa zaidi yake.Inawezekama ikawa kweli yeye akawa bora zaidi ya wegine. Lakini je njia anayo tumia ni si sahihi. Wote tunajua kua prof Lipumba ni mtaaramu wa uchumi. Hivyo anataka kutumia hicho kama kigezo cha kuteuliwa na UKAWA. Inawezekana kikawa nikigezo lakini kwa siasa za Tanzania kigezo cha utaaram wa uhumi kinatosha kumfanya awe Rais?. Hajiulizi kwamba kwanini pamoja na uprofesa wake lakini amegombea urais kalibia mala nne, lakini zote ameshidwa na kura zinazidi kupungua. Hivi ni muujiza gani anao utegemea utakao mfanya mwaka huu ashinde, ikiwa chama chake kimeishia kufanya mikutano Lindi, Mtwara na Tabora tu? Hata mikoa ya pwani tuliyo aminishwa kua ni ngome yao kama Tanga wamshindwa kabisa kujijenga.Chama kina majimbo mawili tu huku bara, lakini prof anataka agombee yeye. Kwa harakati zipi walizo zifanya na chama chake mpaka tuamini ataweza kushinda na kuwauza wagombea wa ukawa?. Wenzenu chadema wakiwa wana zunguka nchi nzima kujenga chama chao, nyinyi mnabaki ofisini kutoa matamko alfu mnataka . mgombea wenu apitishwe kugombea urais. Toka uchaguzi wa mwaka 2010 Profesa hajawai kanyaga mkoa wowote wa nyanda za juu kusini au kanda ya ziwa kwa ajiri ya kujenga chama lakini leo anataka apewe nafasi. Nakumbuka siku David Kafulila alipo pendekeza Dr Slaa awe mgombea wa UKAWA hao hao CUF walikuja juu na kudai amevunja taratibu . https://www.jamiiforums.com/jukwaa-...igawa-ukawa-zinazofanywa-na-wana-ukawa-9.html. lakini cha ajabu wanashindwa kumlaani prof lipumba anae fanya yaleyale waliyo kua wanamlaumu kafulila aliye toa maoni yake tu.

Mwache Lipumba Atangaze Nia, lakini pale ukawa watakapoamua kumpitisha Mtu mwingine Na siyo Lipumba, Tunamuomba Lipumba awe Tayari kumuunga Mkono, Na kama Ukawa Watahamua Kumpitisha Lipumba Basi Wanachama wenza wote wa Ukawa Wawe Tayari kumuunga Mkono. Chezea Ukawa wewe .Lumpumba Endelea na juhudi zako ili CCM waje kujichanganya wenyewe.
 
Mwenyewe nimeona Kupitia ITV jamaa kaamua kutoka kama cuf na si UKAWA,kwa staili hii kapotea
 
Huku tanganyika wapo Lindi na Mtwara tu alfu wanataka kuwania urais.
 
Prof Lipumba ni prof kama alivyo magembe na maji marefu.Kila mwaka staili ile ile hamna ubunifu kabisa.Cuf baada ya kupanda inashuka.Ndio maana anakurupuka kama magamba bora Maalim Seif
 
Prof Lipumba ndiye mwenye sifa hakuna ukawa zaidi ya Lipumba, hatutafuti kiongozi wa kiroho, tunatafuta kiongozi wa nchi.
 
Prof Lipumba ndiye mwenye sifa hakuna ukawa zaidi ya Lipumba, hatutafuti kiongozi wa kiroho, tunatafuta kiongozi wa nchi.
Kuna uhusiano gani kati ya ajali za mabasi na mikutano ya Zitto, ? Leo kaanza na ajali huko Singida
 
Prof Lipumba ndiye mwenye sifa hakuna ukawa zaidi ya Lipumba, hatutafuti kiongozi wa kiroho, tunatafuta kiongozi wa nchi.
Amegombea mara 4 hizo sifa watanzania wangeisha ziona
 
Kutangaza nia siyo tatizo labda wasiwasi wangu ni huko kuiga kwa maccm make nakumbuka tuliawhi kuambiwa kuwa chama chake tayari kimempitisha kama mgombea wa chama hicho ili baadae ashindanishwe na wengine ndani ya UKAWA lakin cha ajabu anataka kutangaza tena, hapo nina mashaka makubwa
 
Tuikiwa tunaelekea kumpata mgombea wa urais kwa tiketi ya UKAWA naomba niongee machache juu ya Prof lipumba anataka agombee yeye. Toka uchaguzi wa mwaka 2010 Profesa hajawai kanyaga mkoa wowote kwa ajiri ya kujenga chama lakini leo anataka apewe nafasi.
Mkuu DCONSCIOUS, kwanza nakupa pole kwa ujinga wako, wewe ni mjinga, na nakuomba usichukulie kuwa nimekutukana bali mjinga ni mtu asiyejua, akiisha julishwa ujinga ukimtoka, anakuwa sio mjinga tena kwa sababu ameufuta huo ujinga wake!.

Mtu kuwa mjinga kwa kutokujua sio kosa, bali kosa ni kama mjinga huyo ataelimishwa na kuendelea kuumbatia ujinga huo!.

Ujinga hapa ni kwa wana UKAWA, kutoelimishwa kuhusu upatikanaji wa mgombea wa pamoja wa urais kwa tiketi ya UKAWA.

Vyama vyote vinne vinavyounda UKAWA viko huru kuendesha mchakato wake wa ndani kumpata mgombea wake wa urais wa Zanzibar na Muungano. Chama cha CUF kimeishauzindua mchakato wake wa ndani na tayari kimeisha mtangaza Maalim Seif ndio mgombea wake urais wa Zanzibar na soon kitazindua huku bara kwa kumtangaza Prof. Lipumba kuwa mgombea wake wa urais bara.

Chadema nacho kiko huru kutangaza mgombea wake wa urais Zanzibar na Bara. NCCR nageuzi nao pia wako huru kutangaza wagombea wao vivyo hivyo kwa NLD.

Kisha UKAWA sasa itakutana na kuwachuja hao wagombea wote kutoka vyama vyote vinavyounda UKAWA na kuibuka na mgombea mmoja mmoja kwa urais wa Zanzibar na wa Muungano kwa tiketi ya UKAWA. Mgombea huyo sasa ndio atakuwa mgombea wa UKAWA na sio lazima ndio lazima awe Prof. Lipumba, anaweza hata kuwa ni James Mbatia au hata Emanuel Makaidi!.

Kwangu tatizo sio CUF kumtangaza Prof. Lipumba kuwa mgombea wake, bali ni watu ambao hawana shughuli nyingine yoyote ambapo siasa wao wameifanya ndio ajira yao ya kudumu, hivyo hata kugombea urais, mtu anakuwa ni mgombea wa kudumu, amaishakataliwa mara 4, na bado anataka tena mara ya 5!, mtu kama huyo asipopitishwa yeye na haku hajawahi kujaribu hata jimbo lolote, atafanya nini?!.

Kwa siasa za Bongo, Prof. Lipumba hana uwezo wa kuchagulika kuiingiza UKAWA Ikulu, ila ni haki yake kuchaguliwa kuwa mgombea wa CUF ila safari yake itaishia kwenye kumpata mgombea wa pamoja mwenye uwezo wa kuchagulika kuiingiza UKAWA Ikulu!.

Naamini kwa hili, utakuwa umeelimika na kuacha ujinga!.

Wito kwa viongozi wa UKAWA, elimisheni watu wenu kuwatoa ujinga ili waijue process ya kuelekea kumpata mgombea wa pamoja!.

Pasco
 
Cuf wameachiwa Zanzibar coz wanakubalika, Rais wa Tz hawezi kutoka Cuf tena coz umoja unakosa maana. Na hata makamu wa Rais busara itumike sana asiwe chama kimoja na Rais. Lipumba ana haki ya kutangaza japo hekima ni muhimu sana ktk hili. Jana niliona vazi la Cuf kama Chadema vile nkafurahi
 
maoni yangu. UKAWA waende na combination ifuatayo. urais wa zanzibar agombee maalim seif sharif hamadi, urais wa tanzania agombee dr. slaa. na wafuatao wagombee ubunge. lipumba,mbowe,makaidi na james mbatia..
 
Mkuu DCONSCIOUS, kwanza nakupa pole kwa ujinga wako, wewe ni mjinga, na nakuomba usichukulie kuwa nimekutukana bali mjinga ni mtu asiyejua, akiisha julishwa ujinga ukimtoka, anakuwa sio mjinga tena kwa sababu ameufuta huo ujinga wake!.

Mtu kuwa mjinga kwa kutokujua sio kosa, bali kosa ni kama mjinga huyo ataelimishwa na kuendelea kuumbatia ujinga huo!.

Ujinga hapa ni kwa wana UKAWA, kutoelimishwa kuhusu upatikanaji wa mgombea wa pamoja wa urais kwa tiketi ya UKAWA.

Vyama vyote vinne vinavyounda UKAWA viko huru kuendesha mchakato wake wa ndani kumpata mgombea wake wa urais wa Zanzibar na Muungano. Chama cha CUF kimeishauzindua mchakato wake wa ndani na tayari kimeisha mtangaza Maalim Seif ndio mgombea wake urais wa Zanzibar na soon kitazindua huku bara kwa kumtangaza Prof. Lipumba kuwa mgombea wake wa urais bara.

Chadema nacho kiko huru kutangaza mgombea wake wa urais Zanzibar na Bara. NCCR nageuzi nao pia wako huru kutangaza wagombea wao vivyo hivyo kwa NLD.

Kisha UKAWA sasa itakutana na kuwachuja hao wagombea wote kutoka vyama vyote vinavyounda UKAWA na kuibuka na mgombea mmoja mmoja kwa urais wa Zanzibar na wa Muungano kwa tiketi ya UKAWA. Mgombea huyo sasa ndio atakuwa mgombea wa UKAWA na sio lazima ndio lazima awe Prof. Lipumba, anaweza hata kuwa ni James Mbatia au hata Emanuel Makaidi!.

Kwangu tatizo sio CUF kumtangaza Prof. Lipumba kuwa mgombea wake, bali ni watu ambao hawana shughuli nyingine yoyote ambapo siasa wao wameifanya ndio ajira yao ya kudumu, hivyo hata kugombea urais, mtu anakuwa ni mgombea wa kudumu, amaishakataliwa mara 4, na bado anataka tena mara ya 5!, mtu kama huyo asipopitishwa yeye na haku hajawahi kujaribu hata jimbo lolote, atafanya nini?!.

Kwa siasa za Bongo, Prof. Lipumba hana uwezo wa kuchagulika kuiingiza UKAWA Ikulu, ila ni haki yake kuchaguliwa kuwa mgombea wa CUF ila safari yake itaishia kwenye kumpata mgombea wa pamoja mwenye uwezo wa kuchagulika kuiingiza UKAWA Ikulu!.

Naamini kwa hili, utakuwa umeelimika na kuacha ujinga!.

Wito kwa viongozi wa UKAWA, elimisheni watu wenu kuwatoa ujinga ili waijue process ya kuelekea kumpata mgombea wa pamoja!.

Pasco
Narudia tena, unapokuwa sober ubongo wako unafanya kazi vizuri sana kama unavyodhihirisha hapa. Kwanini usiachane na hizo lager kabisa?
 
Cuf wameachiwa Zanzibar coz wanakubalika, Rais wa Tz hawezi kutoka Cuf tena coz umoja unakosa maana. Na hata makamu wa Rais busara itumike sana asiwe chama kimoja na Rais. Lipumba ana haki ya kutangaza japo hekima ni muhimu sana ktk hili. Jana niliona vazi la Cuf kama Chadema vile nkafurahi
Ndiyo maana Pasco kashauri muelimishwe taratibu za kuwapata wagombea zilivyo, mkiifahamu na katiba ya nchi hamtakuwa na hoja za kijinga kama hizi zenu tena.
 
5 terms mtu anagombea you still claim hiko chama kina demokrasia?something is wrong
 
5 terms mtu anagombea you still claim hiko chama kina demokrasia?something is wrong
Ndiyo misingi ya demokrasia waliyojiwekea. Prof Safari alijaribu kugombea uenyekiti akashambuliwa na kudhalilishwa sana, na kiongozi wa mashambulizi akiwa hamad rashid. rashid huyohuyo naye akafika mahali ikawa kama amesahau misingi waliyojiwekea kwenye chama. Yaliyomkuta hata kwao Pemba anaogopa kukanyaga, eti naye anagombea urais Tanganyika.
 
Back
Top Bottom