Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais- Mipango na Uwekezaji, Profesa Kitila Mkumbo amesema Tanzania imeendelea kupiga hatua katika mapambano dhidi ya rushwa na ufisadi, jambo linalothibitishwa na takwimu za kimataifa.
Akizungumza katika Jukwaa la Cafetalk lililofanyika Jumamosi, Prof. Kitila amesema kwa mujibu wa vipimo vya Transparency International, Tanzania inashika nafasi ya pili katika Afrika Mashariki kwa juhudi za kupambana na rushwa, ikitanguliwa na Rwanda. Aidha, katika bara la Afrika lenye nchi 54, Tanzania inashika nafasi ya 14
“Kwa vipimo vya Transparency International vinavyopima mwenendo wa rushwa duniani, Tanzania ni ya pili kwa Afrika Mashariki kwenye kupambana na rushwa, tumebaki nyuma ya Rwanda pekee. Ndani ya Afrika, sisi ni wa 14. Hii inaonesha tumekuwa tukipiga hatua kubwa katika mapambano dhidi ya rushwa na ufisadi,” amesema Prof. Kitila alipokuwa akijibu swali lililoulizwa na mtangazaji Charles William kuhusu mtazamo wa Watanzania wa kipato cha chini wanaoamini umasikini wao unasababishwa na rushwa na uzembe.
Katika mjadala huo uliojadili mada: “Je, Serikali ya Awamu ya Sita Imeweza Kugusa Maisha ya Watanzania?”, Prof. Kitila amesema ili kuendelea na mapambano hayo, katika Ilani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) ya mwaka 2025/30 kuna kipengele cha utawala bora chenye lengo la kuimarisha na kudumisha mapambano dhidi ya rushwa, ufisadi, uzembe na wizi
Amesisitiza kuwa Serikali ya Awamu ya Sita imejiwekea dhamira ya dhati na imechukua hatua madhubuti katika kudhibiti vitendo vya rushwa na ufisadi, ili kuhakikisha rasilimali za taifa zinawanufaisha Watanzania wote
Akizungumza katika Jukwaa la Cafetalk lililofanyika Jumamosi, Prof. Kitila amesema kwa mujibu wa vipimo vya Transparency International, Tanzania inashika nafasi ya pili katika Afrika Mashariki kwa juhudi za kupambana na rushwa, ikitanguliwa na Rwanda. Aidha, katika bara la Afrika lenye nchi 54, Tanzania inashika nafasi ya 14
“Kwa vipimo vya Transparency International vinavyopima mwenendo wa rushwa duniani, Tanzania ni ya pili kwa Afrika Mashariki kwenye kupambana na rushwa, tumebaki nyuma ya Rwanda pekee. Ndani ya Afrika, sisi ni wa 14. Hii inaonesha tumekuwa tukipiga hatua kubwa katika mapambano dhidi ya rushwa na ufisadi,” amesema Prof. Kitila alipokuwa akijibu swali lililoulizwa na mtangazaji Charles William kuhusu mtazamo wa Watanzania wa kipato cha chini wanaoamini umasikini wao unasababishwa na rushwa na uzembe.
Katika mjadala huo uliojadili mada: “Je, Serikali ya Awamu ya Sita Imeweza Kugusa Maisha ya Watanzania?”, Prof. Kitila amesema ili kuendelea na mapambano hayo, katika Ilani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) ya mwaka 2025/30 kuna kipengele cha utawala bora chenye lengo la kuimarisha na kudumisha mapambano dhidi ya rushwa, ufisadi, uzembe na wizi
Amesisitiza kuwa Serikali ya Awamu ya Sita imejiwekea dhamira ya dhati na imechukua hatua madhubuti katika kudhibiti vitendo vya rushwa na ufisadi, ili kuhakikisha rasilimali za taifa zinawanufaisha Watanzania wote