Prof. Kitila Mkumbo: Serikali inavuruga vyuo vikuu

Prof. Kitila Mkumbo: Serikali inavuruga vyuo vikuu

Ki Mun

JF-Expert Member
Joined
Oct 6, 2014
Posts
3,442
Reaction score
4,389
Akizungumza Dar es Salaam leo katika Mhadhara wa III wa Kavazi la Mwalimu Nyerere, Prof. Kitila Mkumbo ameilaumu serikali kwa tabia yake ya kuingilia na kuvuruga shughuli za Vyuo Vikuu nchini hata kufikia hatua ya kuzuia vyuo kuajiri na kupandisha vyeo watumishi wao.

Ameshangaa pia kuwa midahalo ya kisomi katika vyuo vikuu siku hizi inahitaji vibali vya polisi na mingi kama siyo yote inazuiliwa na wakuu wa vyuo wenyewe kwa kushirikiana na polisi na wakuu wengine wa vyombo vya dola...amesema hili ni janga la wazi na anashangaa kuwa Maprofesa katika vyuo vikuu wako kimya!

Mada iliyokuwa ikijadiliwa ni "Umuhimu wa Elimu ya Juu katika Maendeleo Afrika"
 
Naam. Kitila anawasilisha jambo la msingi sana. Taasisi za Elimu ya Juu hasa za umma zinapaswa kujitathmini upya endapo kweli zataka kumuenzi Mwalimu kwa vitendo.

Hongera Prof. Kitila.
 
Wasomi wenyewe makanjanja. Yeye kama mmoja wao wamezidi kupiga mdomo tu. Atuambie enzi za kikwe.. ambapo waliweza kutukana, kuandamana , kufanya mikutano tena bila bugdha walifanya nini na elimu zao za juu kuisaidia nchi hii?!
 
Naam. Kitila anawasilisha jambo la msingi sana. Taasisi za Elimu ya Juu hasa za umma zinapaswa kujitathmini upya endapo kweli zataka kumuenzi Mwalimu kwa vitendo.

Hongera Prof. Kitila.
Hivi huyu naye ni profesa wa UDSM? Mbona amejibu kiporojo na blahblah tu. Hana facts. Darasani anafundishaje?
 
Unamwambia nani wakati uko kwenye system?Kwani hamjui nyie wasomi ndiyo hamna michango kwa jamii yetu?Ninyi ni wasomi lakini ni wasanii wa siasa.
 
Naam. Kitila anawasilisha jambo la msingi sana. Taasisi za Elimu ya Juu hasa za umma zinapaswa kujitathmini upya endapo kweli zataka kumuenzi Mwalimu kwa vitendo.

Hongera Prof. Kitila.
Usimpe hongera bila sababu. Vyuo vikuu si ndivyo vinaongozwa na wastaafu? Hawa si ndo juzi hapa wameambiwa warudishe pesa za wizi? Yeye mkumbo amefanya nini kuzuia huyo VC wake ambaye kaigeuza UD kuwa kama sekondari?

Binafsi naiomba serikali iongeze mkono vyuo vikuu. Hao wanaojiita maprofesa wamegeuka kuwa ni waalimu wa kufundisha wizi tu. Pesa za tuition wanajengea bar za pombe na mahoteli wakati facilities za vyuo ziko taaban!
 
Wasomi wenyewe makanjanja. Yeye kama mmoja wao wamezidi kupiga mdomo tu. Atuambie enzi za kikwe.. ambapo waliweza kutukana, kuandamana , kufanya mikutano tena bila bugdha walifanya nini na elimu zao za juu kuisaidia nchi hii?!
Haya mambo ya elimu ya juu waachie wanaoweza kuchangia vizuri. Mbona mada na hoja za kiplopaganda na kisiasa zipo nyingi tu na unaweza kuchangia huko!
 
Haya mambo ya elimu ya juu waachie wanaoweza kuchangia vizuri. Mbona mada na hoja za kiplopaganda na kisiasa zipo nyingi tu na unaweza kuchangia huko!
Hivi huku jf hata wasomi vilaza wanajiita wana elimu ya juu?!, "kiplopaganda" dah nouma!!!! halafu huku jf watu hawajaweka cv zao wewe pimbi. Bado nakosoa wasomi wa kibongo sana,... Obama ni prof wa katiba na sheria but still the man is titled Mr Obama. We need to see what the elite is doing in accordance to his /her level of education bwana mdogo
 
Safi.Magufuli kaza huko chuo kikuu mpaka waisome namba.
 
Kama Wasomi wenyewe ndio nyinyi akina Mkumbo, Bana kwanini F IV polisi wasiwapige ban? Twambie wewe kama Professor una chapisho lolote katika journal kama Nature, Lancet etc. Vimachapisho vyako vyote ni journal of UDSM tena kazi za wanafunzi wa first degree na Masters. Poor Mkumbo!
 
yaan mtu unasema kuwa kitila kaongea pumba et kisa siasa,jamani muwe na akili muda mwingine mtu akiongea jambo la maana mpeni sifa zake siasa baadae!!
 
Unamwambia nani wakati uko kwenye system?Kwani hamjui nyie wasomi ndiyo hamna michango kwa jamii yetu?Ninyi ni wasomi lakini ni wasanii wa siasa.
huyu kitila si ndio alikacha kugombea urais ACT kwa Zitto, halafu ndio yeye alikuwa CHADEMA?
 
Hongera prof mzindue huyu mama ndalichako
 
Back
Top Bottom