Prof. Kitila Mkumbo: Serikali inavuruga vyuo vikuu

Prof. Kitila Mkumbo: Serikali inavuruga vyuo vikuu

kitila simwamini hata punje ya haradani.

alikuwepo na kusifia mengi.....eti leo nimkosoaji.....hivi ana huruma na vyuo au ......
 
Duh! Wanajf mbona mnagawa dozi kubwa kwa prof mchanga? Si mtamuovadozi?
Nami wacha nimkong'ote na kikokoto cha kichwa. Ninyi maprof wa kibongo hakuna hata dakika moja mliwahi kufikiri juu ya watanzania waliojitolea jasho lao kuwasomesha. Ni aibu kujiita maprof kwani hakuna msaada wowote wa mawazo wala nini mliotupa huku chini zaidi ya kujinadi tu. Oneni sasa mnavyojidhalilisha huko mlikopangiwa sijui uwaziri na ukatibu wa wizara. Hakuna mchango wowote mnaoutoa huko.
Acheni siasa fundisheni wataalamu wa kesho.
 
Wasomi wenyewe makanjanja. Yeye kama mmoja wao wamezidi kupiga mdomo tu. Atuambie enzi za kikwe.. ambapo waliweza kutukana, kuandamana , kufanya mikutano tena bila bugdha walifanya nini na elimu zao za juu kuisaidia nchi hii?!
Ulitegemea wafanye nini?
Mijadala huwajenga washiriki, wakiwemo wanachuo, uwezo wa kuchambua masuala mbali mbali. Hili ni muhimu. Mijadala isilinganishwe na kilimo cha nyanya au kahawa.
Taifa lisilokuwa na watu wenye fikira mbadala na wachambuzi ni mfu(walking corpse).
 
Lisu ana uwezo wa kumpiga msasa huyo??? Jadili hoja cyo kila mda siasa tuu

Kwanini asiweze?Mtu aliyepewa Uprofessor na wanasiasa?Anaweza na ameweza period hakuna siasa hapo,ni facts
 
Akizungumza Dar es Salaam leo katika Mhadhara wa III wa Kavazi la Mwalimu Nyerere, Prof. Kitila Mkumbo ameilaumu serikali kwa tabia yake ya kuingilia na kuvuruga shughuli za Vyuo Vikuu nchini hata kufikia hatua ya kuzuia vyuo kuajiri na kupandisha vyeo watumishi wao.

Ameshangaa pia kuwa midahalo ya kisomi katika vyuo vikuu siku hizi inahitaji vibali vya polisi na mingi kama siyo yote inazuiliwa na wakuu wa vyuo wenyewe kwa kushirikiana na polisi na wakuu wengine wa vyombo vya dola...amesema hili ni janga la wazi na anashangaa kuwa Maprofesa katika vyuo vikuu wako kimya!

Mada iliyokuwa ikijadiliwa ni "Umuhimu wa Elimu ya Juu katika Maendeleo Afrika"

Hongera Prof Kitila.

Ushauri wa bure kwako Prof: Achana na ushiriki katika vyama vya siasa, wewe zingatia taaluma yako na uwe msifuji/mkosoaji kitaaluma mwenendo wa serikali. Hapo utafaidi na taaluma yako itaonekana na kufaidia wengi Tanzania na Afrika.
 
Mambo ya kisomi unawauliza Ngumbaru, wasomi wenyewe wamechanganyikiwa kupita kiasi, wanafuga ng'ombe!!
Kuna Mkuu Mmoja Aliwahi Kusema Humu, " Tunahangaika Kunyoosha Vivuli Vya Miti Wakati Iliyopinda Ni Miti Yenyewe".
Tutawalaumu Wasomi Wetu, Tutakejeli Elimu Zao Lakini Bado Haya Yote Ni Matokeo Tu Na Wala Sio Chanzo.
Cha Muhimu Kujiuliza Ni Je, Mifumo Yetu Ya Elimu Inasaidia Kutatua Changamoto Zetu Kama Taifa? Je, Wasomi Wanaotokana Na Mfumo/Mifumo Hiyo Wana Ujasiri Wa Kusimamia Na Kutekeleza Yale Yote Yenye Manufaa Na Tija Kwa Taifa?
 
Akizungumza Dar es Salaam leo katika Mhadhara wa III wa Kavazi la Mwalimu Nyerere, Prof. Kitila Mkumbo ameilaumu serikali kwa tabia yake ya kuingilia na kuvuruga shughuli za Vyuo Vikuu nchini hata kufikia hatua ya kuzuia vyuo kuajiri na kupandisha vyeo watumishi wao.

Ameshangaa pia kuwa midahalo ya kisomi katika vyuo vikuu siku hizi inahitaji vibali vya polisi na mingi kama siyo yote inazuiliwa na wakuu wa vyuo wenyewe kwa kushirikiana na polisi na wakuu wengine wa vyombo vya dola...amesema hili ni janga la wazi na anashangaa kuwa Maprofesa katika vyuo vikuu wako kimya!

Mada iliyokuwa ikijadiliwa ni "Umuhimu wa Elimu ya Juu katika Maendeleo Afrika"
Kama maprofesa wenyewe ni kama yy na Lipumba, ni bora hiyo midahalo ikawa banned forever...... its a wastage of time and resources
 
Usimpe hongera bila sababu. Vyuo vikuu si ndivyo vinaongozwa na wastaafu? Hawa si ndo juzi hapa wameambiwa warudishe pesa za wizi? Yeye mkumbo amefanya nini kuzuia huyo VC wake ambaye kaigeuza UD kuwa kama sekondari?

Binafsi naiomba serikali iongeze mkono vyuo vikuu. Hao wanaojiita maprofesa wamegeuka kuwa ni waalimu wa kufundisha wizi tu. Pesa za tuition wanajengea bar za pombe na mahoteli wakati facilities za vyuo ziko taaban!
Mh!!! Hayo ya kutumia fedha za taasisi kujengea Bar na Mahoteli sinayo taarifa. Wastaafu ni ceremonial figure tu. Waendeshaji/Watendaji si wastaafu natumai.
 
Just
Mh!!! Hayo ya kutumia fedha za taasisi kujengea Bar na Mahoteli sinayo taarifa. Wastaafu ni ceremonial figure tu. Waendeshaji/Watendaji si wastaafu natumai.
recently nimemuona VC wa UD akieleza mafanikio ya chuo chake, which to me was another rubbish on the display.
VC at the age of almost over 70 claiming to develop the university by counting the huge number of graduates instead of their quality.
 
Back
Top Bottom