johnthebaptist
JF-Expert Member
- May 27, 2014
- 84,036
- 142,129
Waziri wa Uchumi Prof Kitila Mkumbo anesema yeye ni Professional na Mbunge anayewakilisha wapiga kura laki 4 Ubungo hivyo ni vema aaminiwe
Prof Kitila amesema DP World watapewa Malengo na Vigezo vyetu wakishindwa watatimuliwa.
---
"Zamani serikali ilikuwa ni mmiliki wa kila kitu, miaka ya 90's serikali ikafanya mabadiliko makubwa ya kisera na kuingia katika uchumi wa soko. Uchumi wa soko maana yake ni kwamba unakaribisha sekta binafsi kushiriki kufanya shughuli za kiuchumi"
"Hata ukienda kwenye uwanja wa ndege mfano KIA aua Mwalimu Nyerere jijini Dar es Salaam, wanaoshughulikia mizigo kwa maana ya kupakua na kupakia mizigo sio serikali ni sekta binafsi, ukienda uwanja wa ndege wa Mwalimu Julius Nyerere kazi hiyo inafanywa na Swissport, lakini suala la ulinzi na usalama linafanywa na serikali, utawakuta jeshi letu, polisi, uhamiaji. Na kwenye bandari ni hivyo hivyo"
"Tunapoteza biashara kwa sababu ya miundombinu ya bandari ni hafifu. Tunahitaji uwekezaji ili bandari yetu ipate uwezo wa kutoa huduma. tunahitaji uwekezaji mkubwa wa bandari ili fedha zingine zikafanye shughuli nyingine kama kujenga barabara, hospitali na mambo mengine. Kwa busara Serikali ya Chama cha Mapinduzi ikamuita mwekezaji.
"Wanauliza kwanini tusiwekeze wenyewe kwenye bandari? Bajeti yote ya Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi ni trilioni 5; hii ndiyo inayojenga barabara, SGR na mambo mengine. Kupanga ni kuchagua, uchukue bajeti hii nzima, zaidi ya nusu upeleke kwenye bandari au umuite mwekezaji aje awekeze?"
Ibara ya 22 inazungumzia marekebisho ya mkataba; mkataba unarekebishika. Sisi kama Serikali tumepokea maoni ya wananchi wengi; yapo maoni ya maana na yasiyo ya maana. Tutayachambua; yale maoni ambayo ni ya maana tutayafanyia kazi na tutakwenda nayo kwenye mitakaba ya miradi"
"Mwekezaji huyu (DP World) tutampa mkataba, maeneo, muda, malengo na vigezo mahususi. Tutampima, akishindwa tutamuondoa mchana kweupe."
"Mtu yeyote anayewaambia kwamba; Serikali yenu ya Chama Cha Mapinduzi imeuza bandari, mtu huyo anawaambieni jambo la kipumbavu. Wengine wanasema tumeuza nchi; nchi ni ardhi na watu wake. Waulizeni kama tumeuza nchi na wao wameuzwa kwa nani?"
"Tumemchagua (DP WORLD) kwa sababu ana faida za ziada, kama vile amewekeza bandari kavu Rwanda na DRC hivyo tukimpa yeye hapa mizigo ya Rwanda na DRC tumeikamata"
"Serikali baada ya kuona haja ya uwekezaji kwenye bandari ilikaribisha maombi na mapendekezo kutoka kwenye makampuni mbalimbali duniani yenye uwezo wa kuwekeza na kuendesha bandari; zilijitokeza saba ikiwemo na hii DP World, sio kweli kwamba ilikuwepo kampuni moja" Prof.
''Mimi ni mbunge, nawakilisha wapigakura zaidi ya laki 4 Jimbo la Ubungo; nina dhamana ya Waziri- Ofisi ya Rais Mipango na Uwekezaji; na pia ni msomi - Profesa niliyesoma kwa kodi zenu, siwezi kuja hapa kuwaambia jambo lisilo na maana (mkataba wa ushirikiano kati ya Tanzania na Dubai kuhusu Uwekezaji Bandarin) ''
Source Jambo TV
Prof Kitila amesema DP World watapewa Malengo na Vigezo vyetu wakishindwa watatimuliwa.
---
"Zamani serikali ilikuwa ni mmiliki wa kila kitu, miaka ya 90's serikali ikafanya mabadiliko makubwa ya kisera na kuingia katika uchumi wa soko. Uchumi wa soko maana yake ni kwamba unakaribisha sekta binafsi kushiriki kufanya shughuli za kiuchumi"
"Hata ukienda kwenye uwanja wa ndege mfano KIA aua Mwalimu Nyerere jijini Dar es Salaam, wanaoshughulikia mizigo kwa maana ya kupakua na kupakia mizigo sio serikali ni sekta binafsi, ukienda uwanja wa ndege wa Mwalimu Julius Nyerere kazi hiyo inafanywa na Swissport, lakini suala la ulinzi na usalama linafanywa na serikali, utawakuta jeshi letu, polisi, uhamiaji. Na kwenye bandari ni hivyo hivyo"
"Tunapoteza biashara kwa sababu ya miundombinu ya bandari ni hafifu. Tunahitaji uwekezaji ili bandari yetu ipate uwezo wa kutoa huduma. tunahitaji uwekezaji mkubwa wa bandari ili fedha zingine zikafanye shughuli nyingine kama kujenga barabara, hospitali na mambo mengine. Kwa busara Serikali ya Chama cha Mapinduzi ikamuita mwekezaji.
"Wanauliza kwanini tusiwekeze wenyewe kwenye bandari? Bajeti yote ya Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi ni trilioni 5; hii ndiyo inayojenga barabara, SGR na mambo mengine. Kupanga ni kuchagua, uchukue bajeti hii nzima, zaidi ya nusu upeleke kwenye bandari au umuite mwekezaji aje awekeze?"
Ibara ya 22 inazungumzia marekebisho ya mkataba; mkataba unarekebishika. Sisi kama Serikali tumepokea maoni ya wananchi wengi; yapo maoni ya maana na yasiyo ya maana. Tutayachambua; yale maoni ambayo ni ya maana tutayafanyia kazi na tutakwenda nayo kwenye mitakaba ya miradi"
"Mwekezaji huyu (DP World) tutampa mkataba, maeneo, muda, malengo na vigezo mahususi. Tutampima, akishindwa tutamuondoa mchana kweupe."
"Mtu yeyote anayewaambia kwamba; Serikali yenu ya Chama Cha Mapinduzi imeuza bandari, mtu huyo anawaambieni jambo la kipumbavu. Wengine wanasema tumeuza nchi; nchi ni ardhi na watu wake. Waulizeni kama tumeuza nchi na wao wameuzwa kwa nani?"
"Tumemchagua (DP WORLD) kwa sababu ana faida za ziada, kama vile amewekeza bandari kavu Rwanda na DRC hivyo tukimpa yeye hapa mizigo ya Rwanda na DRC tumeikamata"
"Serikali baada ya kuona haja ya uwekezaji kwenye bandari ilikaribisha maombi na mapendekezo kutoka kwenye makampuni mbalimbali duniani yenye uwezo wa kuwekeza na kuendesha bandari; zilijitokeza saba ikiwemo na hii DP World, sio kweli kwamba ilikuwepo kampuni moja" Prof.
''Mimi ni mbunge, nawakilisha wapigakura zaidi ya laki 4 Jimbo la Ubungo; nina dhamana ya Waziri- Ofisi ya Rais Mipango na Uwekezaji; na pia ni msomi - Profesa niliyesoma kwa kodi zenu, siwezi kuja hapa kuwaambia jambo lisilo na maana (mkataba wa ushirikiano kati ya Tanzania na Dubai kuhusu Uwekezaji Bandarin) ''
Source Jambo TV