Saint Ivuga
JF-Expert Member
- Aug 21, 2008
- 54,363
- 58,385
Katika hatua nyingine, Mbunge wa Urambo Magharibi, Profesa Juma Kapuya (CCM), juzi alijisalimisha katika ofisi ya CHADEMA akimuomba Zitto azungumzie matatizo ya barabara katika jimbo lake ili aweze kusaidiwa.
Kapuya alitoa ombi hilo katika ofisi za CHADEMA wilaya baada ya Zitto kuwasili eneo hilo saa 9.30 mchana kwa ajili ya kufanya mkutano wa hadhara, ikiwa ni kutekeleza ahadi yake aliyoitoa wakati alipohutubia mkutano wa awali kwa njia ya simu wiki tatu zilizopita.
Akiwa ofisini hapo, Prof. Kapuya alihojiwa na Zitto akitaka kujua sababu ya kuikodishia Halmashauri ya Kaliua nyumba yake huku akiwa ni mmoja wa madiwani wa wilaya hiyo wanaopaswa kuhakikisha halmashauri inakuwa na majengo yake.
"Karibu mzee katika ofisi zetu, lakini unaweza kuniambia kama uamuzi wako wa kuikodishia halmashauri nyumba yako hauingiliani na vikwazo vya kuiwezesha kupata majengo yake?" alihoji Zitto.
Katika kujitetea, Prof. Kapuya alisema sababu ya kufanya biashara hiyo na halmashauri ni kutokana na wilaya kutokuwa na majengo yake binafsi.
"Ni kweli mimi ninakodisha, lakini kiasi ninachochukua ni kidogo kuliko kile anachochukua Waziri Magufuli katika Wilaya ya Chato, kwani naye anaikodishia halmashauri ya wilaya yake jengo linalotumika kama ofisi," alisema Kapuya.
Katika hali ya kuonyesha kuwa anaomba Zitto asizungumzie upungufu uliopo katika jimbo lake, Prof. Kapuya alimuomba azungumzie matatizo ya barabara.
Zitto alisema kimaadili kiongozi anapofanya biashara sehemu anayoweza kuwa na uamuzi inasababisha hali ya kulinda maslahi ya kiongozi huyo ikiwa ni pamoja na kukwamisha mradi wa eneo husika usikamilike au kujiongezea gharama katika biashara husika.
Alimueleza Prof. Kapuya kuwa kinachosabaisha Mkoa wa Tabora usiendelee, ni pamoja na matatizo ya ubinafsi kati ya wabunge wa mkoa huo, huku akiwaambia waache tofauti zao na Mbunge wa Urambo Mashariki, Samuel Sitta katika kuwatumikia wananchi.
Kapuya alitoa ombi hilo katika ofisi za CHADEMA wilaya baada ya Zitto kuwasili eneo hilo saa 9.30 mchana kwa ajili ya kufanya mkutano wa hadhara, ikiwa ni kutekeleza ahadi yake aliyoitoa wakati alipohutubia mkutano wa awali kwa njia ya simu wiki tatu zilizopita.
Akiwa ofisini hapo, Prof. Kapuya alihojiwa na Zitto akitaka kujua sababu ya kuikodishia Halmashauri ya Kaliua nyumba yake huku akiwa ni mmoja wa madiwani wa wilaya hiyo wanaopaswa kuhakikisha halmashauri inakuwa na majengo yake.
"Karibu mzee katika ofisi zetu, lakini unaweza kuniambia kama uamuzi wako wa kuikodishia halmashauri nyumba yako hauingiliani na vikwazo vya kuiwezesha kupata majengo yake?" alihoji Zitto.
Katika kujitetea, Prof. Kapuya alisema sababu ya kufanya biashara hiyo na halmashauri ni kutokana na wilaya kutokuwa na majengo yake binafsi.
"Ni kweli mimi ninakodisha, lakini kiasi ninachochukua ni kidogo kuliko kile anachochukua Waziri Magufuli katika Wilaya ya Chato, kwani naye anaikodishia halmashauri ya wilaya yake jengo linalotumika kama ofisi," alisema Kapuya.
Katika hali ya kuonyesha kuwa anaomba Zitto asizungumzie upungufu uliopo katika jimbo lake, Prof. Kapuya alimuomba azungumzie matatizo ya barabara.
Zitto alisema kimaadili kiongozi anapofanya biashara sehemu anayoweza kuwa na uamuzi inasababisha hali ya kulinda maslahi ya kiongozi huyo ikiwa ni pamoja na kukwamisha mradi wa eneo husika usikamilike au kujiongezea gharama katika biashara husika.
Alimueleza Prof. Kapuya kuwa kinachosabaisha Mkoa wa Tabora usiendelee, ni pamoja na matatizo ya ubinafsi kati ya wabunge wa mkoa huo, huku akiwaambia waache tofauti zao na Mbunge wa Urambo Mashariki, Samuel Sitta katika kuwatumikia wananchi.