SI KWELI Prof. Janabi dawa ya ugonjwa wa presha

SI KWELI Prof. Janabi dawa ya ugonjwa wa presha

Baada ya kuitathmini taarifa hii, tumebaini kuwa si ya kweli.
1753700739343.png

 
Tunachokijua
Madai

Kumekuwepo na kipande cha video kinachomuonesha Mkurugezi wa Shirika la afya duniani (WHO) kanda ya Afrika, Prof. Mohamed Janabi akizungumzia kuwa kuna tiba ya moyo ambayo inaweza kumfanya mtu akapona kwa kutumia kikombe kimoja

Uhalisia wa madai hayo

JamiiCheck imefuatilia na kujiridhisha kuwa kipande hicho cha video kimehaririwa kwa teknolojia ya Akili Unde (AI).

Kipande hiko cha video kinachomuonesha Prof. Janabi kinaoneakana kuhaririwa kutoka kwenye moja ya mazungumzo aliyoyafanya Mkurugenzi huyo na baadae kuwekewa maneno hayo yanayosikika.

Ufuatiliaji kwa kutumia nyenzo za kubaini maudhui yaliyotengenezwa kwa Akili Unde, JamiiCheck imebaini kuwa sauti iliyottumika katika video hiyo ni ya kutengeneza kwa Akili Unde na wala si sauti halisi ya Prof. Janabi.
Back
Top Bottom