ntamaholo
JF-Expert Member
- Aug 30, 2011
- 12,906
- 6,909
Hbr. Wanajamvi.
Jana nilikuwa kwenye msiba, ambpo pamoja na utani wa makabila yetu, SIASA huwa ni ajenda mhimu watu wenye uelewa tofauti wanapokutana. Kati ya vitu tlivyoongea, kimoja kimenivutia na kufikiria kukileta kwenu ili kukifikisha kwa wahusika kwa urahisi zaidi. Kitu hicho ni sera ya ardhi.
Ni wazi kuwa, tunayo sera na sheria ya ardhi, ambayo imetoa mamlaka ya utoaji hatimiliki za kimila kwa serikali za mitaa. Lakini malengo ya utoaji hatimiliki, upanuliwe na kuwekewa sheria nzito ili kuzuia uuzaji holela wa aridhi. Maoni ya wananzengo yalikuwa kama ifuatavyo:-
(a) Aridhi yote ipimwe na ipewe hatimiliki. serikali iandae mipango kamambe ya kuhakikisha ardhi yote imepimwa kama walivyo RWANDA, BOTSWANA, LIBYA na wananchi kumilikishwa n.k
(b) Iundwe sheria kali ya kudhibiti uuzaji wa ardhi hasa kwa wageni ili wanapokuja kuwekeza, wenye ardhi, tukubaliane kumiliki hisa za kampuni kwa thamani ya ardhi yetu. Hii itasaidia kuwaingiza wenye ardhi kwenye biashara kubwa tena zenye faida.
(d) Serikali ibaki na jukumu la kuwalea wote wenye ardhi, na mtu akifanya kinyume, basi sheria ichukue mkondo wake.
Ilivyo sasa hivi, ardhi inatambulika ni mali ya umma. Viongozi mda wowote wanamamlaka ya kunyang'anya ardhi ya mtu kwa kisingizio cha maslahi ya umma, wakati ukweli umma haunufaiki. Sehemu zote za migodi, watu wamenyang'anywa ardhi zao na hwajalipwa fidia na hawanifaiki kwa lolote.
kama wangemilikishwa ardhi ile, wawekezaji wangelazimika kugawa hisa kwa wamiliki wa ardhi na hivyo kuwawezesha wenyeji kumiliki hisa katika uchimbaji wa madini.
Tibaijuka, ni nafasi yako, ukifanikiwa hili, utakumbukwa milele, kama huwezi, vyama mbadala wekeni suala hili katika ajenda zenu ili 2015, utekelezaji wake uanze.
nawasilisha.
Jana nilikuwa kwenye msiba, ambpo pamoja na utani wa makabila yetu, SIASA huwa ni ajenda mhimu watu wenye uelewa tofauti wanapokutana. Kati ya vitu tlivyoongea, kimoja kimenivutia na kufikiria kukileta kwenu ili kukifikisha kwa wahusika kwa urahisi zaidi. Kitu hicho ni sera ya ardhi.
Ni wazi kuwa, tunayo sera na sheria ya ardhi, ambayo imetoa mamlaka ya utoaji hatimiliki za kimila kwa serikali za mitaa. Lakini malengo ya utoaji hatimiliki, upanuliwe na kuwekewa sheria nzito ili kuzuia uuzaji holela wa aridhi. Maoni ya wananzengo yalikuwa kama ifuatavyo:-
(a) Aridhi yote ipimwe na ipewe hatimiliki. serikali iandae mipango kamambe ya kuhakikisha ardhi yote imepimwa kama walivyo RWANDA, BOTSWANA, LIBYA na wananchi kumilikishwa n.k
(b) Iundwe sheria kali ya kudhibiti uuzaji wa ardhi hasa kwa wageni ili wanapokuja kuwekeza, wenye ardhi, tukubaliane kumiliki hisa za kampuni kwa thamani ya ardhi yetu. Hii itasaidia kuwaingiza wenye ardhi kwenye biashara kubwa tena zenye faida.
(d) Serikali ibaki na jukumu la kuwalea wote wenye ardhi, na mtu akifanya kinyume, basi sheria ichukue mkondo wake.
Ilivyo sasa hivi, ardhi inatambulika ni mali ya umma. Viongozi mda wowote wanamamlaka ya kunyang'anya ardhi ya mtu kwa kisingizio cha maslahi ya umma, wakati ukweli umma haunufaiki. Sehemu zote za migodi, watu wamenyang'anywa ardhi zao na hwajalipwa fidia na hawanifaiki kwa lolote.
kama wangemilikishwa ardhi ile, wawekezaji wangelazimika kugawa hisa kwa wamiliki wa ardhi na hivyo kuwawezesha wenyeji kumiliki hisa katika uchimbaji wa madini.
Tibaijuka, ni nafasi yako, ukifanikiwa hili, utakumbukwa milele, kama huwezi, vyama mbadala wekeni suala hili katika ajenda zenu ili 2015, utekelezaji wake uanze.
nawasilisha.