Posta Arusha na wizi wa Parcel zetu

MVUMBUZI

JF-Expert Member
Jan 8, 2011
5,182
2,304
Siku za hivi karibuni katika posta ya Arusha (Meru na Clock Tower) kumekuwa na upotevu mkubwa wa vifurushi hususani vile vinavyotoka nje ya nchi. Hata pale ambapo kifurushi kina kuwa na tracking number lakini pindi tu kikifika Arusha kifurushi kinapotea katika mazingira ya utata.

Kuna wakati unakuta kikaratasi cha kuchukua mzigo kwenye sanduku lako lakini ukifika kaunta eti utaambiwa mzigo hauonekani na inaweza kuchukua hadi siku kadhaa za ufuatiliaji ndipo uambiwe ooh ulikuwa umechanganywa na hadithi nyiingi za kiujanja ujanja.

Tulichogundua ni kuwa kitengo cha sorting au kina wafanyakazi wasio waaminifu na hivyo kuiba vifurushi kwa njia za kijanja au wafanyakazi hao ni wazembe kupindukia na hivyo kutokuwepo umakini katika kufanya sorting.

Pia uchunguzi umeonyesha kuwako idadi kubwa ya wazee katika posta ya Arusha haswa Meru kiasi cha kushindwa kutimiza wajibu wao kwa ubora na umakini unaotakiwa.

Tunaomba mamlaka husika itusaidie kufuatilia jambo hili ili kuwabaini wafanyakai wasio waaminifu na wazembe na hivyo kusababisha upotevu mkubwa wa vifurushi ya wateja haswa ile vinavyotumwa toka nchi a Marekani na Ulaya.


Kwa mfano kwa kipindi cha mwaka mmoja nimepotea zaidi ya vifurushi vitano kwa maelezo eti anwani imekosewa wakati tangu mzigo unatumwa ninau track kwenye mtandao.
 
Kinachoturudisha nyuma wabongo ama waafrika nikukosa uaminif. Imetukosti sana hili jambo.
 
Wananusa wakiona kitu cha thamani wanapotea makusudi
 
mimi ni mlizwa mmojawapo..nimepigwa tarehe mpaka nimechoka..
 
Hii hali imeshamiri sana hapa Arusha na hakuna anayefanya ufuatiliaji kiasi kwamba kabla hujaagiza kitu nje unajishauri mara mbili. Wezi wako kitengo cha sorting na kurekodi. Mizigo ya watu inaibiwa kabla haijapelekwa kuwa registered.
Tena wakishakujua ndi utaibiwa kila wakati. Mimi parcel zangu karibu 3 zilipotea na wala hawaonyeshi kujali zaidi ya kupiga blalh blah tu. Hawa hawana tofauti na majambazi tu
 
Hawa hawajui watu wananunua vitu nje kwa bei kubwa halafu wao wanakuja na kukiiba tu kirahisi. Inabidi watengenezewe mtego ili mwizi ajulikane au wajulikane kwani inaonyesha siyo mtu mmoja bali kamtandao
 
Mkuu umeongea, uaminifu bado sana katika bara letu, Ongeza na customer care mbovu vurugu tupu.

Hata competence za wafanyakazi ni zile za mwaka 47. kaangalie walivyochoka sio watu wa kuona kitu kizuri wakakiacha. Nimeshapoteza zaidi ya parcel 6 ambazo zina tracking number lakini zikifika hapo wale wa kuingiza kwenye system na register hawaingizi wakishajua ni kitu kinachomfaa.
Lazima wajue tunaingia gharama kununua hivi vitu hatupewi kama zawadi hivyo wawe na huruma kwa wateja
 
Nina marafiki zangu watatu ambao pia parcel zao za kutoka nje eti hazionekani na inawezekana zilitumwa kama barua siyo parcel.Kwa hiyo parcel ikitumwa kama barua na si kifurushi ndio wana haki ya kuiiba?
 
Wafanyakazi wengi wa posta Arusha wameanzza kufanya kazi hapo tangu wakiwa wasichana na wengine waulana hadi wanazeeka na hiyo hii imesababisha wafanye kazi kimazoea. Hii safu inatakiwa iangaliwe upya ili kurudisha imani kwa wateja.

Vitu vingi vinavyoibiwa ni vilei vya watu binafsi ila wanaogopa vitu vinavyotumwa kupitia taasisi
 
Wafanyakazi wengi wa posta Arusha wameanzza kufanya kazi hapo tangu wakiwa wasichana na wengine waulana hadi wanazeeka na hiyo hii imesababisha wafanye kazi kimazoea. Hii safu inatakiwa iangaliwe upya ili kurudisha imani kwa wateja.

Vitu vingi vinavyoibiwa ni vilei vya watu binafsi ila wanaogopa vitu vinavyotumwa kupitia taasisi

Mvumbuzi it seems you know them extremely well. why don't you see the higher authority?
You are very familiar with. Is that a cut throat strategy?
 
Umri au uzoefu un à uhusiano na wizi?hapana lawama kwa Mkurugenzi posta TANZANIA na meneja kanda awaamishe
 
Iko SIKU nitapiga Kelele za Mwizi, mwizi hapo Meru posta hadi watie akili, Ngoja ni ute cha Orkokola ETI Na kakituo kadogo ka TCA na mwenyewe parcel zinapotea!
 
Back
Top Bottom