Posho ya madaraka kwa Walimu

Posho ya madaraka kwa Walimu

Kashi

JF-Expert Member
Joined
Jan 6, 2013
Posts
897
Reaction score
747
Mwaka jana Wizara ya Utumishi ilitoa waraka kuhusiana na posho ya madaraka kwa Walimu wakuu, wakuu wa shule na Waratibu Elimu Kata na ikaelezwa kuwa utekelezaji utaanza July mosi 2015. Kuna Wilaya yoyote wameanza kulipwa?
 
Fanya kazi!! si MSHAHARA mnapata??? BALANCE hicho hicho! hii Nchi TUNA MAMBO MENGI YA KUFANYA........
 
Waalimu mnapaswa kupigania ili posho ilipwe kwa wote, sio walimu wakuu tu. Polisi, Magereza na Wanajeshi wanapewa posho wakat vituo vyao vya kaz vipo mjini na mazingira yao ya kazi ni afadhali kuliko yenu. Msikubali kudharauliwa kwasababu ya chaki zenu wakati wenye bunduki wananyenyekewa! Where is CWT when u need it the most?
 
Wakuu washule watafune capitation grants,michango mbalimbali shuleni,fedha za misaada,wengi hawafundishi bado walipwe posho za ziada wakati kazi nyingi wanafanya walimu.serikali ifikirie vizuri sivyo matokeo yataporomoka ghafla.walimu nao walipwe posho ya kufundishia kama ilivyokuwa zamani enzi za Mwinyi.
 
Wakuu washule watafune capitation grants,michango mbalimbali shuleni,fedha za misaada,wengi hawafundishi bado walipwe posho za ziada wakati kazi nyingi wanafanya walimu.serikali ifikirie vizuri sivyo matokeo yataporomoka ghafla.walimu nao walipwe posho ya kufundishiakama ilivyokuwa zamani enzi za Mwinyi.
Hapo kwenye red kumbuka kuwa wakuu wana shughuli nyingi za kiutawala japo wanafundisha pia. Hapo kwenye kijani ni kweli kabisa inatakiwa hii kitu Serikali ilifanyie kazi haraka ili kurejesha morali ya walimu.
 
Huu mwaka wa uchaguzi serikali haitalipa hizo posho tusubiri mwakani
 
Mimi ni Mwalimu mishahara imeongezwa sana tufanye kazi kwa bidii,Tsh716,000 naona posho sio lazima halafu sisi ni vijana 25yrs

Unakaa wapi wewe...! Njoo dsm ulipe pango la nyumba laki 300000, umeme 50000,maji 40000, nauli kazini 100000, weka chakula uonw utabaki na shilingi ngapi?.....! Kweli wewe umeboreshewa mshahara
 
Unakaa wapi wewe...! Njoo dsm ulipe pango la nyumba laki 300000, umeme 50000,maji 40000, nauli kazini 100000, weka chakula uonw utabaki na shilingi ngapi?.....! Kweli wewe umeboreshewa mshahara

Naishi Dar toka nilipoajiriwa,ni PM namba yako kama ni mwalimu,tufahamiane
 
Je wewe unayetaka kulipwa bajeti ya serikali peke yako

Acha kuwaza kimaskini wewe, na hao wanaolipwa milioni 12 kwa mwezi ni bajeti ya nani? Kama unajithaminisha kwa laki saba utalipwa hizo hizo. Ukijipa thamani kubwa utalipwa kwa thamani yako. TAFAKARI!!
 
Mimi ni Mwalimu mishahara imeongezwa sana tufanye kazi kwa bidii,Tsh716,000 naona posho sio lazima halafu sisi ni vijana 25yrs
Sema mimi ni kijana, halafu hata kama ni kijana usipende kuridhika kwa vitu vidogo vidogo. Laki saba?
 
Sema mimi ni kijana, halafu hata kama ni kijana usipende kuridhika kwa vitu vidogo vidogo. Laki saba?

Mkuu usipoteze mda kubishana na mtoto.Ameshakuambia ni under 25 bado hajayajua maisha mwache akue kwanza.
 
Back
Top Bottom