Ponda aigharimu Serikali milioni 10/-

Ponda aigharimu Serikali milioni 10/-

Intelijensia bana.

Hakuna intelijensia yoyote ni ni pinda tu hao wanatutia hasara! Ponda ana kosa gani la kutugharimu namna hii? Hata wakati wa Mbowe walitutia hasara hivi hivi kwa kumrusha mpaka Arusha kutoka Dar kwa ndege eti kujibu mashitaka. Leo kesi hata haijulikani kama ipo na itakwisha lini kwasababu haina mashiko. Mtindo wa pinda wengi waliopo serikalini kufungua kesi zisizo na maana ndio unaotugharimu. Angalia jinsi walihangaika na kesi za kuwabambikia watu kesi za ugaidi na hatimaye kushindwa. Kesi hizo zimetugharimu kwasababu ya upinda wao kwani pia walikuwa wanawakamata watu wasiokuwa na hatia na kuwasafirisha kwa ndege mara Dar, Mwanza na kisha Igunga na Tabora walikoambulia aibu lakini wakiwa wametutia hasara kubwa! pinda kabisa hao!
 
Hizo hela wamempa nani? wakati helkopta ni ya polisi na viwanja vya gofu. Mbona mnatupiga sana fix wabongo? tumewakosea nini nyie waandishi mpaka muandike uongo wa namna hii. Basi wangekodisha Costal Airline 14 seater ingetosha na gharama zake isingefika milioni tatu.
 
Visima vya CCM havitoi maji na fedha ni za mkopo wa dunia utakaolipwa kwa riba sasa kipi bora ndugu yangu CDM kuelimisha umma na kuikomboa nchi au kuchimba visima visivyo na maji?

Duh kama helicopter garama yake ni kubwa hivyo dakika 45 tu ni milioni 5 basi CDM watakua wako fiti sana kifedha manake hiyo helicopter wakati wa campain waliirusha sana let say 12hrs *30days *10,682,031=3,845,531,160 yaani kwa mwezi mmoja CDM walikua wanatumia 3.8billions aisee sasa CHADEMA itabidi mbadilishe mtindo wa campain hiyo hela mnayotumia kwa kurusha helicopter katika campain muwapelekee maendeleo vijijini kwa kujenga visima kuwaletea maji wananchi watawapeni kura tu badala ya kuchoma hela angani muwe mkitumia magari
 
[h=2][/h]


*Usafiri wa helikopta waitafuna dola mara 71 ya gharama ya gari
ULINZI wa Katibu wa Jumuiya na Taasisi za Kiislamu, Sheikh Ponda Issa Ponda, akiwa gerezani na anapopelekwa mahakamani, umeanza kuvitesa vyombo vya Dola. Habari zilizolifikia gazeti hili na kuthibitishwa na Kamanda wa Kikosi cha Anga wa Jeshi la Polisi, zinaeleza kuwa serikali juzi ilitumia kiasi cha shilingi 10,682,031 kama gharama za usafiri wa helikopta za kumpeleka na kumrudisha kiongozi huyo mahakamani mkoani Morogoro.

MTANZANIA Jumatano kupitia vyanzo vyake vilivyoko ndani na nje ya Jeshi la Polisi, limedokezwa kuwa gharama za kurusha helikopta kwa dakika 45 hadi saa moja ni dola za Marekani 3,000 hadi 3,300 ambazo ni sawa na shilingi 5,341,032.85 .

Hivyo gharama za kwenda na kurudi kwa saa jumla yake ni dola za Marekani 6,600 ambazo ni sawa na shilingi 10,682,031.

Akithibitisha hilo, Kamanda wa Kikosi cha Anga wa Jeshi la Polisi, Antony Mwami alisema gharama za kurusha helikopta kwa dakika 45 ni dola 3,000 ambazo ni sawa na shilingi milioni tano.

Katika uchunguzi wake gazeti hili limebaini kuwa gharama hizo zilizotumika kwa siku moja tu, zingetosha kumsafirisha Ponda kwenda Morogoro na kurudi mara 71, endapo ungetumika usafiri wa gari wa kawaida.

Gazeti hili limebaini kuwa kwa usafiri wa kawaida wa gari, gharama za kutoka Dar es Salaam hadi Morogoro hazizidi shilingi 150,000.

Juzi Jeshi la Polisi kwa kutumia helikopta yake inayodaiwa kuwa na uwezo wa kubeba watu wanane, lilimsafirisha Sheikh Ponda hadi mkoani Morogoro ambako alipandishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi na kusomewa mashtaka ya uchochezi yanayomkabili.

Sheikh Ponda aliwasili kwa helikopta hiyo na kutua kwenye uwanja wa gofu, Morogoro akiwa chini ya ulinzi mkali wa polisi na alipakiwa tena kwenye gari maalumu ambalo liliongozana na mengine matatu ya polisi kuelekea eneo la mahakamani.

Baada ya kumalizika kusomwa kwa kesi hiyo, msafara ule ule ulimrejesha uwanja wa gofu saa
 
Mnashangaa ya Ponda? Mbona aliyekua waziri wa ulinzi hapo nyuma JUMA KAPUYA alishawahi kwenda kijijini kwao na ndege ya jeshi hamkuuliza garama yake ilikua shi ngapi?
 
Mfumo kristu kazini, wako tayar kwa gharama yoyote kuhakikisha waislam wanakandamizwa.
Time will tell
 
Duh kama helicopter garama yake ni kubwa hivyo dakika 45 tu ni milioni 5 basi CDM watakua wako fiti sana kifedha manake hiyo helicopter wakati wa campain waliirusha sana let say 12hrs *30days *10,682,031=3,845,531,160 yaani kwa mwezi mmoja CDM walikua wanatumia 3.8billions aisee sasa CHADEMA itabidi mbadilishe mtindo wa campain hiyo hela mnayotumia kwa kurusha helicopter katika campain muwapelekee maendeleo vijijini kwa kujenga visima kuwaletea maji wananchi watawapeni kura tu badala ya kuchoma hela angani muwe mkitumia magari
Chadema watazirudisha tu hizo wakiingia madarakani
 
Kenya mbali na gharama nyingine, walitumia $ 600,000 kukodisha ndege iliyomrudisha Sheikh Abdullah Faisal kwao Jamaica!...hivyo ndivyo mfumo kristo unavyofanya kazi.

acha udini wewe
 
Hivi hizo gharama za kutumia helicopter kwa dk45 mnazipimaje ndugu zangu watanzania hadi kufikia $3000?
kale ka msemo "wajinga ndio waliwao/wanaoliwa" kasije kakawa kana apply hapa.


Insurance =$200.
Aviation fee=$150.
Mafuta=$400. Ukichakachua hata $100 inatosha!
Wages and security=$200.
Mambo madogomadogo $150.( sigara na chachandu zingine!!) Na jioni za baridi pale kona bar!!)


Jumla ya gharama =$1100,

Pamoja na:-

Na muandishi wa hizi gharama na bosi wake $ 1900 !!

Jumla yote ni $3000!

Hapo utatamani uwe wewe ndio huyo mwandishi wa gharama!
 
acha kupindisha mada au post ilyoko mezani we kifudufudu

Duh kama helicopter garama yake ni kubwa hivyo dakika 45 tu ni milioni 5 basi CDM watakua wako fiti sana kifedha manake hiyo helicopter wakati wa campain waliirusha sana let say 12hrs *30days *10,682,031=3,845,531,160 yaani kwa mwezi mmoja CDM walikua wanatumia 3.8billions aisee sasa CHADEMA itabidi mbadilishe mtindo wa campain hiyo hela mnayotumia kwa kurusha helicopter katika campain muwapelekee maendeleo vijijini kwa kujenga visima kuwaletea maji wananchi watawapeni kura tu badala ya kuchoma hela angani muwe mkitumia magari
 
Kweli CDM kiboko, kwani kila kitu SI unit ni CDM. Hivi mnpokimbilia kuona kuwa CDM ilitumia gharama kubwa mmejiuliza kwanza haya?
1. Hivi ule msafara wa magari ulikouwa unatumiwa na JK, ukijumlisha gharamna ya mafuta na p/diem za watu wote aliokuwa anafuatana nao mnajua gharama yake?
2. Je mnajua kwamba upande wa manunuzi, watumishi walio wengi wa Serikali na idara zake wanapandisha gharama? usije shangaa, helicopter kama hiyo CDM wanaweza kuirusha Dar to Moro, kwa gharama huenda nusu ya hiyo.
3. Suala kama la Ponda kusafirishwa kwa helicopter au ilivyotokea kwa Kileo kusafirishwa kwenda Tabora kwa helicopter ni mwendelezo wa matumizi yasiyo ya lazima. Haya mambo kama ya Ponda yasingefikia hapa kama si udhaifu wa Serikali

afadhal umewaambia manake chadema inataka kuwatoa roho kila kitu chadema
 
jadili mada ilyoko mezani we ng'ombe, ya udini peleka mk8nd8ni kwako...

Halafu ungeongea kiswahili tupu! Ungetusaidia kuelewa!
Sasa ukituchanganyia na kiluga humu!
Mhhhh!! Utatuua mwana wane!
 
Back
Top Bottom