Mwanapropaganda
JF-Expert Member
- Aug 19, 2014
- 4,235
- 2,512
Licha ya kuwa maisha ni magumu, vijana wengi wa sasa nchini Tanzania ni watumiaji wakubwa wa pombe tena zile zilizo kali.
Nakutana na vijana wanadai kuwa pesa ni ngumu na wakati mwingine wanadiriki kukuomba ukidhani kuna cha maana wanafanya kumbe ni kwenda kununulia pombe.
Hali hii ilizoeleka kuwa ni vijana wa mitaani walioshindwa kwenda shule ndio wanajihusisha na matumizi ya pombe kumbe upepo umebadilika na sasa hata wasomi wa vyuo vikuu wamekuwa ni watumiaji wa vileo.
Nimefanya uchunguzi usio na shaka na kubaini kuwa vijana wengi wa sasa wanaotumia vileo ni wale wenye umri wa kuanzia miaka 17 kwenda juu na wengi wao wakiwa ni wanafunzi wa taasisi za elimu ya juu.
Kwa vyovyote iwavyo hili ni tatizo ambalo linachangia kurudisha nyuma maendeleo ya vijana na taifa la kesho.
Nadhani kuna watu wameliona na wanaliona hili, wewe kama mzazi/mlezi una mpango wa namna gani wa kumuepusha kijana wako asijiingize kwenye tabia mbovu ya unywaji wa pombe?
Tusemezane
Nakutana na vijana wanadai kuwa pesa ni ngumu na wakati mwingine wanadiriki kukuomba ukidhani kuna cha maana wanafanya kumbe ni kwenda kununulia pombe.
Hali hii ilizoeleka kuwa ni vijana wa mitaani walioshindwa kwenda shule ndio wanajihusisha na matumizi ya pombe kumbe upepo umebadilika na sasa hata wasomi wa vyuo vikuu wamekuwa ni watumiaji wa vileo.
Nimefanya uchunguzi usio na shaka na kubaini kuwa vijana wengi wa sasa wanaotumia vileo ni wale wenye umri wa kuanzia miaka 17 kwenda juu na wengi wao wakiwa ni wanafunzi wa taasisi za elimu ya juu.
Kwa vyovyote iwavyo hili ni tatizo ambalo linachangia kurudisha nyuma maendeleo ya vijana na taifa la kesho.
Nadhani kuna watu wameliona na wanaliona hili, wewe kama mzazi/mlezi una mpango wa namna gani wa kumuepusha kijana wako asijiingize kwenye tabia mbovu ya unywaji wa pombe?
Tusemezane