Pombe inawaangamiza vijana

Pombe inawaangamiza vijana

Mkuu kila kitu hugeuka kuwa Kilevi ukikitumia kupita kiasi,Ndiyo maana utasikia mtu anakwambia kuwa yeye ni mlevi wa Mpira,Movie,Kahawa,Draft,n.k.Hivyo basi ni vema kusisitiza matumizi sahihi na kiwango sahihi cha pombe.

Lakini hapa nimezungumzia ulevi wa pombe.
 
Mkuu nadhani wazungumzia ulevi haswa haswa.., maana huwa kuna wanywaji wa pombe na walevi wa pombe!
Swala la ulevi linaelekea kuwa janga la taifa na pengine niseme hauhitajiki utafiti wa kisanyansi kuhakiki hili.
Mitaani mwetu kumejaa vijana walevi wa kupindukia. Mfano mzuri ni asubuhi ukitupia macho kwenye vibaraza vya maduka tayari vijana wana viroba/banana.., wengine wameshalewa tayari!
Pita jioni, mara nyingi utawakuta wengi wao wako pale pale!

Jiulize swali, nguvu kazi ya taifa wanawajibika saa ngapi kujiingizia kipato cha kujikimu na kulewea!?
Je kwa style hii tutakuwa na taifa la aina gani huko mbeleni?

Wenzetu Kenya wako kwenye kampeni ya kupiga vita ulevi kwa maana wameshatambua kuwa ni janga.., kazi kwetu kusemezana na vijana wetu wapunguze ama kuacha ulevi kabisa!!

kidogo wewe umeongea point
 
Pombe gani aneangamiza vijana??? Pombe huyu huyu tunaemjuwa kachaguliwa juzi mbona mnamsingizia
 
Acha niwanong'oneze wasije wakanisikia! "Msilitaje jina la Rais (Pombe) kwenye masuala ya ulevi!"
Hahahaaa natania tu.
 
Back
Top Bottom