Pombe inawaangamiza vijana

Pombe inawaangamiza vijana

Pombe inasababisha watt wa vigogo kufanya kufuru kivipi mkuu..??

Pombe na vinywaji hivi vikali walio kwenye mamlaka wanajua uingizwaji wake nchini na wakati mwingine wanatoa vibali wenyewe kama sio kumiliki biashara kabisa na kuchangia mapato....unadhani mkurugenzi wa say TBS akiongezewa mshahara kwa makusanyo bora bila kujali baadhi yanatoka kwenye bidhaa hatarishi watoto wake hawanufaiki? Si ni hawa hawa vijana wanatuharibia binti zetu kwenye night clubs? Si ni hawa hawa hawana heshima bara barani?
 
Waacheni Masikini wanywe "mvinyo"wazisahau shida zao. Hakuna kipindi ambacho vijana wamepiga mvinyo kama huu utawala wa "Kikwete" awamu ya pili sijui kwa nini.?!!
 
Mmoja wa wahanga wakubwa wa hii kitu ni Nicholas.
Kwa kweli Pombe ni Mbya sana

Huyu Kijana Amezeeka Ndani ya miaka 6 tu toka utoto wake.
 
Last edited by a moderator:
daa rafiki zangu kama wa 4 wamefariki kisa pombe, kuna kikundi flan cha wahitimu wa chuo mtaani wanakula gambe mpaka wanafunga mtaa. hatari sana
 
Pombe na vinywaji hivi vikali walio kwenye mamlaka wanajua uingizwaji wake nchini na wakati mwingine wanatoa vibali wenyewe kama sio kumiliki biashara kabisa na kuchangia mapato....unadhani mkurugenzi wa say TBS akiongezewa mshahara kwa makusanyo bora bila kujali baadhi yanatoka kwenye bidhaa hatarishi watoto wake hawanufaiki? Si ni hawa hawa vijana wanatuharibia binti zetu kwenye night clubs? Si ni hawa hawa hawana heshima bara barani?

Mtu kama umezoea kufanya anasa hata ukiwa sio mnywaji utafanya anasa kwa style nyingine..hao watt wa vigogo wanaowaharibu Binti zenu nightclubs na kuvunja sheria barabarani hayo ndo maisha/tabia zao..sidhani kama kunywa pombe ndo kunawafanya hivyo..wangapi wanakunywa na hawazingui
 
sio pombe akili yao tu mbovu lazima uwe na kiwango cha kuzinywa hizo bia lkn viroba hapo ndu shuhuri
 
Mtu kama umezoea kufanya anasa hata ukiwa sio mnywaji utafanya anasa kwa style nyingine..hao watt wa vigogo wanaowaharibu Binti zenu nightclubs na kuvunja sheria barabarani hayo ndo maisha/tabia zao..sidhani kama kunywa pombe ndo kunawafanya hivyo..wangapi wanakunywa na hawazingui

Sina hakika kama ulinielewa....sijasema wanakunywa pombe...ila vipato vya wazazi wao ambao ndio walitakiwa kudhibiti ubora wa bidhaa ndiyo vinawavimbisha vichwa!
 
Mkuu fikra nyepesi kama hizi zinauridhisha ubongo wako na kushindwa kufikiria matatizo makubwa yanayorudisha maendeleo ya taifa nyuma

Hahahahaha! katika mambo hayo yanayochangia umasikini pombe iko juu japo sio ya kwanza.
 
Sina hakika kama ulinielewa....sijasema wanakunywa pombe...ila vipato vya wazazi wao ambao ndio walitakiwa kudhibiti ubora wa bidhaa ndiyo vinawavimbisha vichwa!
basi tutakuwa hatukuelewana..mi nilikujibu vile ili kubaki kwenye mada husika..mana swali langu lilikuwa "pombe inasababisha vipi watt wa vigogo kufanya kufuru?" katika majibu yako nikaona umeongelea nightclubs na uvunjaji wa sheria nikajua ndo kufuru unazoziongelea ndo mana nikakujibu vile..
 
Mkuu kila kitu hugeuka kuwa Kilevi ukikitumia kupita kiasi,Ndiyo maana utasikia mtu anakwambia kuwa yeye ni mlevi wa Mpira,Movie,Kahawa,Draft,n.k.Hivyo basi ni vema kusisitiza matumizi sahihi na kiwango sahihi cha pombe.
 
Licha ya kuwa maisha ni magumu, vijana wengi wa sasa nchini Tanzania ni watumiaji wakubwa wa pombe tena zile zilizo kali.
Nakutana na vijana wanadai kuwa pesa ni ngumu na wakati mwingine wanadiriki kukuomba ukidhani kuna cha maana wanafanya kumbe ni kwenda kununulia pombe.

Hali hii ilizoeleka kuwa ni vijana wa mitaani walioshindwa kwenda shule ndio wanajihusisha na matumizi ya pombe kumbe upepo umebadilika na sasa hata wasomi wa vyuo vikuu wamekuwa ni watumiaji wa vileo.

Nimefanya uchunguzi usio na shaka na kubaini kuwa vijana wengi wa sasa wanaotumia vileo ni wale wenye umri wa kuanzia miaka 17 kwenda juu na wengi wao wakiwa ni wanafunzi wa taasisi za elimu ya juu.

Kwa vyovyote iwavyo hili ni tatizo ambalo linachangia kurudisha nyuma maendeleo ya vijana na taifa la kesho.
Nadhani kuna watu wameliona na wanaliona hili, wewe kama mzazi/mlezi una mpango wa namna gani wa kumuepusha kijana wako asijiingize kwenye tabia mbovu ya unywaji wa pombe?

Tusemezane

Hii mada imenigusa, Mimi nafanya Kazi kwenye Taasisi flani kubwa tu, Nina Rafiki yangu tumeajiriwa pamoja, Mwenzangu amenizidi kidogo Kipato kulingana na Kazi yake, Ila maisha anayoishi yanatia uchungu kwa kweli, Yaani huwa anafikia anadaiwa Bili hadi inafika laki Nane, Mimi pamoja na Kipato changu Kidogo, Nimemudu kununua kausafiri kangu na kiwanja, Yeye hata wazo hilo hana, Anaishi kwenye nyumba za Ofisi na kuendekeza Pombe.
 
Wanywe tu Tra waongeze mapato...ni bora tupambane na wala unga,mana halipiwi hata kodi
 
Licha ya kuwa maisha ni magumu, vijana wengi wa sasa nchini Tanzania ni watumiaji wakubwa wa pombe tena zile zilizo kali.
Nakutana na vijana wanadai kuwa pesa ni ngumu na wakati mwingine wanadiriki kukuomba ukidhani kuna cha maana wanafanya kumbe ni kwenda kununulia pombe.

Hali hii ilizoeleka kuwa ni vijana wa mitaani walioshindwa kwenda shule ndio wanajihusisha na matumizi ya pombe kumbe upepo umebadilika na sasa hata wasomi wa vyuo vikuu wamekuwa ni watumiaji wa vileo.

Nimefanya uchunguzi usio na shaka na kubaini kuwa vijana wengi wa sasa wanaotumia vileo ni wale wenye umri wa kuanzia miaka 17 kwenda juu na wengi wao wakiwa ni wanafunzi wa taasisi za elimu ya juu.

Kwa vyovyote iwavyo hili ni tatizo ambalo linachangia kurudisha nyuma maendeleo ya vijana na taifa la kesho.
Nadhani kuna watu wameliona na wanaliona hili, wewe kama mzazi/mlezi una mpango wa namna gani wa kumuepusha kijana wako asijiingize kwenye tabia mbovu ya unywaji wa pombe?

Tusemezane

Punguani wahed, anajisemeaga ff;

vijana ndio wanaunda sehemu kubwa ya population ya tz inayoendeshwa kwa kodi za pombe,
vijana endeleeni kupiga vyombo serikali ipate ile mil 238 ya wabunge.
 
Hahahahaha! katika mambo hayo yanayochangia umasikini pombe iko juu japo sio ya kwanza.

Si kweli mkuu, mie nimesoma Economics sijawahi kuskia tafiti yoyote kwamba pombe inaleta umaskini au uhusiano kati ya pombe na umaskini. Pombe wanakunywa watu wa level zote yaana maskini, wa kipato cha na matajiri. Pombe ni kama kiburudisho kingine tu kama vile ngono, kwenda disco, kunywa soda au juice, kuhudhulia matamasha ya music, kwenda beach, kuchat au kuongea na simu, kuvuta bange na madawa ya kulevya. Vyote hivyo vinafanywa na watu walio maskini na matajiri na ambapo vyote vinahitaji pesa ili uweze kuvipata. Sasa unapoishambulia pombe peke yake unakuwa kama una chuki binafsi na pombe. Kuna mtu hanywi pombe lakini kila siku ananunua malaya na kulipia gest. Ina maana maskini wote hapa Tanzania ni wanywa pombe ?, wasiokunywa pombe wote matajiri ?
 
Mkuu nadhani wazungumzia ulevi haswa haswa.., maana huwa kuna wanywaji wa pombe na walevi wa pombe!
Swala la ulevi linaelekea kuwa janga la taifa na pengine niseme hauhitajiki utafiti wa kisanyansi kuhakiki hili.
Mitaani mwetu kumejaa vijana walevi wa kupindukia. Mfano mzuri ni asubuhi ukitupia macho kwenye vibaraza vya maduka tayari vijana wana viroba/banana.., wengine wameshalewa tayari!
Pita jioni, mara nyingi utawakuta wengi wao wako pale pale!

Jiulize swali, nguvu kazi ya taifa wanawajibika saa ngapi kujiingizia kipato cha kujikimu na kulewea!?
Je kwa style hii tutakuwa na taifa la aina gani huko mbeleni?

Wenzetu Kenya wako kwenye kampeni ya kupiga vita ulevi kwa maana wameshatambua kuwa ni janga.., kazi kwetu kusemezana na vijana wetu wapunguze ama kuacha ulevi kabisa!!
 
Back
Top Bottom