Herbalist Dr MziziMkavu
JF-Expert Member
- Feb 3, 2009
- 42,319
- 33,125
Mkurugenzi wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai (DCI), Robert Manumba
Jeshi la Polisi linakwepa kutoa tamko la kukataa au kuthibitisha madai yaliyotolewa na Naibu Waziri wa Ujenzi, Dk. Harrison Mwakyembe, kwamba linatumiwa na mafisadi kutokana na taarifa iliyotoa kuwa ugonjwa unaomsumbua waziri huo hautokani na kulishwa sumu.
Mkurugenzi wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai (DCI), Robert Manumba, hivi karibuni alisema uchunguzi uliofanywa na jeshi hilo na kupata taarifa toka Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii, ugonjwa unaomsumbua Dk. Mwakyembe hautokani na kulishwa sumu.
Hata hivyo siku moja baada ya tamko hilo, lDk. Mwakyembe aliibuka na kueleza kuwa Jeshi hilo lina ufinyu wa uelewa unaojitokeza kwenye tamko lake unaosisitiza kuwa hakunywesha.
Dk. Mwakyembe alieleza kuwa vyombo vya dola likiwemo Jeshi la Polisi vinapelekeshwa na mafisadi ndiyo maana vimetoa taarifa kwamba hakulishwa sumu ambayo inatofautiana na ile iliyotolewa na madaktari waliokuwa wakimtibu nchini India.
Msemaji wa Polisii, Advera Senso, alipopigiwa Ijumaa ya wiki iliyopita alimtaka mwandishi kuwasilisha maswali ya mambo anayotaka kuyauliza kwa maandishi ili yajibiwe. Jumanne wiki hii NIPASHE iliwasilisha maswali, lakini
tangu juzi hadi jana Senso amekuwa akipiga danadana kutoa majibu ya maswali hayo.
Juzi alipofuatwa ofisini kwake, alisema maswali ameyapokea, lakini yapo katika ofisi ya utawala na kuahidi jana kufuatilia ili yaweze kujibiwa lakini kinyume chake amedai kuwa bado hayajajibiwa.
Jeshi la Polisi limeanza kumsaka mchawi aliyeibua madai hayo ili ashtakiwe mahakamani kutokana na uamuzi wa kupeleka jalada la mashtaka kwa Mkurugenzi wa Mashtaka (DPP). Senso, alisema jalada hilo limeshapelekwa kwa DPP ingawa hakuwa tayari kueleza kwa kina wanaotuhumiwa katika jalada hilo.
CHANZO: NIPASHE