Polisi walima shamba.....

Polisi walima shamba.....

Boflo

JF-Expert Member
Joined
Jan 20, 2010
Posts
4,383
Reaction score
4,412
Kuna jamaa alifungwa jela miaka 7 kwa
kosa la wizi wa mamilioni ya pesa. Baada
ya miaka 2 akiwa jela anapata barua toka
kwa babake, Mwanangu mpendwa
umeniacha ktk hali ya uzee na maradhi,
wakati wa kutayarisha shamba umefika, na sina mtu wa kunilimia, natamani
ungekuwepo ukanisaidia kulima na
kupanda mahindi. Tutaonana mungu
akipenda.


Mtoto akajibu. Baba tafadhali usije lima
ktk hilo shamba kwa sasa mpaka nitoke
jela, pesa zote nilizoiba nimezifukia ktk
shamba hilo.


Kwa kuwa barua zote za wafungwa
husomwa na polisi wa gerezani. Baba siku
ya pili alipoamka akakuta polisi zaidi ya
100 wanalima shamba. Mpaka
wakamaliza wasipate kitu. Mtoto
akamwandikia babake.


Mpendwa baba natumai msaada niliokupa
umeufurahia, panda mahindi sasa


Mjini akili shamba kilimo
 
Hahahahahaha yaan raha sna

Sent from my BlackBerry 9800 using Jamie's
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom