Herbalist Dr MziziMkavu
Platinum Member
- Feb 3, 2009
- 43,074
- 34,844
Salim Said
SIRI ya kuchelewa kwa posho za askari polisi mwezi Febuari mwaka huu imefichuka baada ya kudaiwa kuwa maafisa watatu wa jeshi hilo walitoweka na hundi ya malipo hayo yanayofikia Sh3 bilioni.
Baadhi ya maofisa wa polisi waliozungumza na gazeti hili kwa nyakati tofauti wiki hii, walielezea mazingira ya wizi huo na kusisitiza kuwa ngazi ya juu ya jeshi hilo imekuwa ikificha taarifa hizo, kwa hofu ya kuchafua sifa ya chombo hicho cha dola.
Wakizungumza kwa sharti la kutotajwa majina yao gazetini, walisema fedha hizo ziliibwa na maofisa hao watatu baada ya kubadili maelezo kwenye hati ya malipo na kuielekeza katika akaunti za mmoja wao.
Wakadai kwamba, kilichosababisha siri hiyo kufichuka ni baada ya kuchelewa kwa posho hizo na kusababisha baadhi ya askari hao kuanza kulalamika kwa maofisa wao wa juu.
Askari hao ambao baadhi walifika kwenye ofisi za gazeti hili walisema, kwa kawaida posho hizo zinatakiwa kutoka tarehe 15 ya kila mwezi, lakini mwezi Februari zilichelewa hadi Aprili 9 mwaka huu.
"Awali IGP alikanusha tuhuma hizo, lakini ni kweli zilipotea kwa sababu askari watatu waliotuhumiwa kuhusika walikamatwa na kupelekwa kizuizini katika vituo vya Msimbazi na Salenda Bridge vya jijini Dar es Salaam," mmoja wa askari hao alisema huku akihoji:
"Sasa askari wanajiuliza kwamba, kama IGP alikanusha tuhuma za wizi huo, kwanini askari hao walikamatwa?"
Juzi, Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini (IGP) Said Mwema alikataa kuzungumzia kukamatwa kwa polisi hao, ingawa Aprili 8, mwaka huu alikiri kupata malalamiko ya askari kuhusu tukio hilo.
Afande Mwema akalitaka gazeti hili liwasiliane na Msemaji wa Jeshi la polisi nchini, Kamanda Abdalah Mssika kwa maelezo zaidi kuhusiana na suala hilo.
Hata hivyo, Mssika alishindwa kutoa maelezo ya kina kuhusu tukio hilo akisema hakuwepo ofisini muda mrefu kwa sababu za kiafya.
Mimi sina taarifa yoyote kuhusu tukio hilo, kwa sababu nipo katika matibabu, sipo kazini, lakini nipe muda niulizie halafu nitakujibu, naomba namba yako ya simu ya mkononi, alisema Mssika.
Kwa muda wa siku wa mbili tangu aahidi kumpigia simu mwandishi, Kamanda Mssika hajapiga simu na alipopigiwa tena alisema: "Siwezi kukusaidia kwa hilo sasa, bado niko kwenye matibabu lakini suala hilo naendelea kulifanyia kazi."
Taarifa zaidi zimeeleza kuwa askari hao walikamatwa baada ya akaunti ya mmoja wao ambaye ni mwanamke kukutwa na kiasi hicho cha fedha na kushindwa kuzitolea maelezo ya kuridhisha.
Kinachoumiza zaidi ni kwamba posho zetu zimechelewa na aliyechelewesha amebainika halafu anawekwa ndani kwa muda mfupi na kuachiwa bila ya kuchukuliwa hatua,alilalamika askari mwingine aliyezungumza na gazeti hili.
Alisema hivi sasa maslahi ya polisi yamekuwa tatizo; posho zinachelewa, nafasi za masomo kwa askari wa kawaida hakuna na hata kupandishwa vyeo ni shida kwao.
Posho ya uhamisho ni haki yako, lakini polisi tunafahamishwa na kila siku tunasafiri kwa fedha zetu. Tukifika tulikohamishiwa inaweza ikapita hata miezi miwili bila kupewa posho ya safari, alisema mmoja wa askari hao na kuongeza:
Askari unalinda nyumba za viongozi, maofisi ya viongozi, lakini hata ukiomba maji katika nyumba za viongozi hao hupati, achilia mbali chakula. Tunalinda huku tukiwa na njaa.
Taarifa zilizolifikia gazeti hili zimeeleza kwamba, ingawa baadhi ya askari polisi jijini Dar es Salaam wameanza kupata posho zao za Februari, maeneo mengi ya Tanzania Bara na Visiwani hazijaanza kutolewa.
Baadhi ya mikoa ambayo askari wake waliliambia gazeti hili kwamba hawajapata posho, ni Tarime-Rorya kwa Tanzania Bara na baadhi ya mikoa ya Zanzibar hawajapata posho hizo.
Hadi sasa ndugu mwandishi hatujapata posho yetu, tunateseka kweli, tunaishi katika hali ngumu," alisena polisi mmoja wa Tarime.
Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Suleiman Kova alipoulizwa kuhusu kukamatwa kwa maofisa wa jeshi hilo wanaodiwa kuiba fedha hizo, alikataa kuzungumza kwa maelezo kuwa suala hilo liko juu ya uwezo wake bali aulizwe afande Mssika.
Hili suala Mwananchi halipo katika mamlaka yangu, mpigie Mssika. Unataka niseme jambo halafu nionekane sielewi majukumu yangu, alisema Kova.
Aprili 8, mwaka huu IGP alikiri kupata taarifa za wizi huo kutoka kwa baadhi ya askari wake ambao pia walimtaka achunguze kuhusu tukio hilo.
Lakini baadaye alikanusha wizi na kueleza kuwa posho zao zilicheleweshwa kutokana na matatizo ya kiutawala na mahesabu.
http://www.mwananchi.co.tz/newsrids.asp?id=19225
SIRI ya kuchelewa kwa posho za askari polisi mwezi Febuari mwaka huu imefichuka baada ya kudaiwa kuwa maafisa watatu wa jeshi hilo walitoweka na hundi ya malipo hayo yanayofikia Sh3 bilioni.
Baadhi ya maofisa wa polisi waliozungumza na gazeti hili kwa nyakati tofauti wiki hii, walielezea mazingira ya wizi huo na kusisitiza kuwa ngazi ya juu ya jeshi hilo imekuwa ikificha taarifa hizo, kwa hofu ya kuchafua sifa ya chombo hicho cha dola.
Wakizungumza kwa sharti la kutotajwa majina yao gazetini, walisema fedha hizo ziliibwa na maofisa hao watatu baada ya kubadili maelezo kwenye hati ya malipo na kuielekeza katika akaunti za mmoja wao.
Wakadai kwamba, kilichosababisha siri hiyo kufichuka ni baada ya kuchelewa kwa posho hizo na kusababisha baadhi ya askari hao kuanza kulalamika kwa maofisa wao wa juu.
Askari hao ambao baadhi walifika kwenye ofisi za gazeti hili walisema, kwa kawaida posho hizo zinatakiwa kutoka tarehe 15 ya kila mwezi, lakini mwezi Februari zilichelewa hadi Aprili 9 mwaka huu.
"Awali IGP alikanusha tuhuma hizo, lakini ni kweli zilipotea kwa sababu askari watatu waliotuhumiwa kuhusika walikamatwa na kupelekwa kizuizini katika vituo vya Msimbazi na Salenda Bridge vya jijini Dar es Salaam," mmoja wa askari hao alisema huku akihoji:
"Sasa askari wanajiuliza kwamba, kama IGP alikanusha tuhuma za wizi huo, kwanini askari hao walikamatwa?"
Juzi, Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini (IGP) Said Mwema alikataa kuzungumzia kukamatwa kwa polisi hao, ingawa Aprili 8, mwaka huu alikiri kupata malalamiko ya askari kuhusu tukio hilo.
Afande Mwema akalitaka gazeti hili liwasiliane na Msemaji wa Jeshi la polisi nchini, Kamanda Abdalah Mssika kwa maelezo zaidi kuhusiana na suala hilo.
Hata hivyo, Mssika alishindwa kutoa maelezo ya kina kuhusu tukio hilo akisema hakuwepo ofisini muda mrefu kwa sababu za kiafya.
Mimi sina taarifa yoyote kuhusu tukio hilo, kwa sababu nipo katika matibabu, sipo kazini, lakini nipe muda niulizie halafu nitakujibu, naomba namba yako ya simu ya mkononi, alisema Mssika.
Kwa muda wa siku wa mbili tangu aahidi kumpigia simu mwandishi, Kamanda Mssika hajapiga simu na alipopigiwa tena alisema: "Siwezi kukusaidia kwa hilo sasa, bado niko kwenye matibabu lakini suala hilo naendelea kulifanyia kazi."
Taarifa zaidi zimeeleza kuwa askari hao walikamatwa baada ya akaunti ya mmoja wao ambaye ni mwanamke kukutwa na kiasi hicho cha fedha na kushindwa kuzitolea maelezo ya kuridhisha.
Kinachoumiza zaidi ni kwamba posho zetu zimechelewa na aliyechelewesha amebainika halafu anawekwa ndani kwa muda mfupi na kuachiwa bila ya kuchukuliwa hatua,alilalamika askari mwingine aliyezungumza na gazeti hili.
Alisema hivi sasa maslahi ya polisi yamekuwa tatizo; posho zinachelewa, nafasi za masomo kwa askari wa kawaida hakuna na hata kupandishwa vyeo ni shida kwao.
Posho ya uhamisho ni haki yako, lakini polisi tunafahamishwa na kila siku tunasafiri kwa fedha zetu. Tukifika tulikohamishiwa inaweza ikapita hata miezi miwili bila kupewa posho ya safari, alisema mmoja wa askari hao na kuongeza:
Askari unalinda nyumba za viongozi, maofisi ya viongozi, lakini hata ukiomba maji katika nyumba za viongozi hao hupati, achilia mbali chakula. Tunalinda huku tukiwa na njaa.
Taarifa zilizolifikia gazeti hili zimeeleza kwamba, ingawa baadhi ya askari polisi jijini Dar es Salaam wameanza kupata posho zao za Februari, maeneo mengi ya Tanzania Bara na Visiwani hazijaanza kutolewa.
Baadhi ya mikoa ambayo askari wake waliliambia gazeti hili kwamba hawajapata posho, ni Tarime-Rorya kwa Tanzania Bara na baadhi ya mikoa ya Zanzibar hawajapata posho hizo.
Hadi sasa ndugu mwandishi hatujapata posho yetu, tunateseka kweli, tunaishi katika hali ngumu," alisena polisi mmoja wa Tarime.
Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Suleiman Kova alipoulizwa kuhusu kukamatwa kwa maofisa wa jeshi hilo wanaodiwa kuiba fedha hizo, alikataa kuzungumza kwa maelezo kuwa suala hilo liko juu ya uwezo wake bali aulizwe afande Mssika.
Hili suala Mwananchi halipo katika mamlaka yangu, mpigie Mssika. Unataka niseme jambo halafu nionekane sielewi majukumu yangu, alisema Kova.
Aprili 8, mwaka huu IGP alikiri kupata taarifa za wizi huo kutoka kwa baadhi ya askari wake ambao pia walimtaka achunguze kuhusu tukio hilo.
Lakini baadaye alikanusha wizi na kueleza kuwa posho zao zilicheleweshwa kutokana na matatizo ya kiutawala na mahesabu.
http://www.mwananchi.co.tz/newsrids.asp?id=19225