PreGE2025 Polisi wafika Ofisi za ACT Wazalendo kumkamata Janeth Rithe kwa agizo la ZCO

PreGE2025 Polisi wafika Ofisi za ACT Wazalendo kumkamata Janeth Rithe kwa agizo la ZCO

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla)

Waufukweni

JF-Expert Member
Joined
May 16, 2024
Posts
4,393
Reaction score
14,500
Shangwe Ayo, Naibu Katibu wa Habari, Uenezi na Mahusiano ya Umma wa ACT Wazalendo na Waziri Kivuli wa Utumishi wa Umma na Utawala Bora, kupitia ukurasa wake wa X (zamani Twitter), ametangaza kuwa Polisi wamevamia ofisi za chama hicho na kumkamata Mwenyekiti wa Ngome ya Wanawake Taifa, Janeth Rithe.

1750411739184.png
Shangwe ameandika kuwa polisi wamedai kuwa wanatekeleza agizo kutoka kwa ZCO (Ofisa Upelelezi wa Mkoa). Hata hivyo, haijabainika wazi ni kwa sababu gani kiongozi huyo wa wanawake anatafutwa na vyombo vya dola.

Screenshot 2025-06-20 122841.png

Janeth Rithe pia amethibitisha kupokea ujumbe kuhusu kutakiwa kwake na Vyombo vya Usalama, akisema: "Ni kweli nimeletwa ujumbe kwamba nahitajika, ndiyo naelekea kwa ZCO."
 
Hivi Hawa wanasiasa hawawezi kuhubiri siasa kwa agenda zao bila kuweka matusi kwa Raisi wa Nchi?

Wanadhani ipo namna ya kuporomosha matusi kwa Raisi halafu Dola ikakaa kimya?
 
Shangwe Ayo, Naibu Katibu wa Habari, Uenezi na Mahusiano ya Umma wa ACT Wazalendo na Waziri Kivuli wa Utumishi wa Umma na Utawala Bora, kupitia ukurasa wake wa X (zamani Twitter), ametangaza kuwa Polisi wamevamia ofisi za chama hicho na kumkamata Mwenyekiti wa Ngome ya Wanawake Taifa, Janeth Rithe.

Shangwe ameandika kuwa polisi wamedai kuwa wanatekeleza agizo kutoka kwa ZCO (Ofisa Upelelezi wa Mkoa). Hata hivyo, haijabainika wazi ni kwa sababu gani kiongozi huyo wa wanawake anatafutwa na vyombo vya dola.

Ile clip ya jana kuwa raisi kachanganyikiwa
 
Siku hz ht mtu akifanya uhalifu anakja kutafuta huruma huku. Eti hatutarudi nyuma, yaani hautarudi nyuma kufanya uhalifu? Utarudi tu kwa kulazimishwa
Punguza kunywa VISUNGURA na matumizi ya UGORO Mkuu hii itakusaidia kutafakari kwa kina kabla ya kuandika.

Una jeshi gani la kupambana na uhalifu wewe? Huyo mafwele mwenyewe ni mhalifu anayestahili kuwa amenyongwa kwa kuua watu.
Mbona hatujawahi kusikia jeshi la polisi limewakamata wale wanaotajwa na CAG kutoka lumumba kila mwaka???
 
Back
Top Bottom