Nyendo
JF-Expert Member
- Jun 4, 2017
- 1,194
- 4,112
Polisi Mkoani Kigoma wanamshikilia mwalimu wa shule ya msingi Mwanga iliyopo Manispaa ya Kigoma Ujiji Zakaria Richard mwenye umri wa miaka 30 kwa tuhuma za kumbaka na kumlawiti Mwanafunzi mwenye miaka 10 anayesoma darasa la tano katika shule hiyo.
Mwanafunzi huyo [Ambaye jina lake limehifadhiwa] alikabidhiwa na wazazi wake kwa mwalimu huyo, kwa lengo la kumfundisha masomo ya ziada [tution] na badala yake mwalimu huyo alianza kumfanyia vitendo vya kikatili.
Hata hivyo uchunguzi bado unaendelea na pindi utakapo kamilika mtuhumiwa atafikishwa mahakamani kwa ajili ya taratibu za kisheria.
Pia, Kamanda wa Polisi Mkoani Kigoma amewaasa wazazi kua makini pale wanapowakabidhi watotot wao kwa walimu kwa ajili ya kufundishwa masomo ya ziada. Amesema wahakikishe wanafalitia kwa karibu maendeleo ya watoto wao
Mwanafunzi huyo [Ambaye jina lake limehifadhiwa] alikabidhiwa na wazazi wake kwa mwalimu huyo, kwa lengo la kumfundisha masomo ya ziada [tution] na badala yake mwalimu huyo alianza kumfanyia vitendo vya kikatili.
Hata hivyo uchunguzi bado unaendelea na pindi utakapo kamilika mtuhumiwa atafikishwa mahakamani kwa ajili ya taratibu za kisheria.
Pia, Kamanda wa Polisi Mkoani Kigoma amewaasa wazazi kua makini pale wanapowakabidhi watotot wao kwa walimu kwa ajili ya kufundishwa masomo ya ziada. Amesema wahakikishe wanafalitia kwa karibu maendeleo ya watoto wao