Abdull Kazi
JF-Expert Member
- Dec 29, 2012
- 323
- 255
Nimeongea na baadhi ya madereva wakaeleza mtu huyo huanza majukumu yake hayo kuanzia saa 11:30 jioni
https://www.tzabroad.com/2022/01/19/kauli-ya-mh-rais-mama-samia-suluhu-hassan-kila-mbuzi-anakula-kwa-urefu-wa-kamba-yake-isitumike-vibaya/
Hivi Karibuni katika maeneo ya Chanika Kuna mtu ameibuka akijitambulisha kuwa ni Askari,anatumia gari binafsi yenye namba T673 DRL na mara zote hutembea na Redio mfano wa Redio call akiwa amevaa nguo za kiraia.
Kazi aliyojipa mtu huyu ambaye wajihi wake ni mweusi na mfupi wastani wa futi Tano ni kukamata magari ya daladala Majira ya jioni kwa Yale yanayofanya makosa Kisha hutoa plate number na kuwaagiza wahusika wamfuate.
Jana Mei 28 alikamata magari mawili yanayofanya safari Kati ya Chanika na Segerea kwa tuhuma za kukatisha ruti na nyingine kuovateki sehemu isiyo sahihi
Baada ya kukamata moja alitoa plate number na nyingine akamuambia dereva amfuate
Wote walielekea eneo la baa ya Sonate Chanika na kupaki hapo Kisha wahusika wakatoa fedha na kuachiwa
Nimeongea na baadhi ya madereva wakaeleza mtu huyo huanza majukumu yake hayo kuanzia saa 11:30 jioni
hii nchi haijawahi kuwa na hakiUnakamatwa na raia na wewe unatoa helaa. Kwanini hao madereva wasimdunde.
Nimeongea na baadhi ya madereva wakaeleza mtu huyo huanza majukumu yake hayo kuanzia saa 11:30 jioni.Hivi Karibuni katika maeneo ya Chanika kuna mtu ameibuka akijitambulisha kuwa ni Askari, anatumia gari binafsi yenye namba T673 DRL na mara zote hutembea na Redio mfano wa Redio call akiwa amevaa nguo za kiraia.
Kazi aliyojipa mtu huyu ambaye wajihi wake ni mweusi na mfupi wastani wa futi Tano ni kukamata magari ya daladala Majira ya jioni kwa Yale yanayofanya makosa Kisha hutoa plate number na kuwaagiza wahusika wamfuate.
Jana Mei 28 alikamata magari mawili yanayofanya safari kati ya Chanika na Segerea kwa tuhuma za kukatisha ruti na nyingine kuovateki sehemu isiyo sahihi.
Baada ya kukamata moja alitoa plate number na nyingine akamuambia dereva amfuate.
Wote walielekea eneo la baa ya Sonate Chanika na kupaki hapo Kisha wahusika wakatoa fedha na kuachiwa.
Nimeongea na baadhi ya madereva wakaeleza mtu huyo huanza majukumu yake hayo kuanzia saa 11:30 jioni.
Ndo maana Gaidi aliachiwa kumbe mahakama haziko huru !Mahakama zingekuwa huru huu ujinga uisingekuwepo
Magari ya abiria ndio yanakuwa na vibali vilivyokamilika zaidi kuliko ya private, hupendelea kukamata magari ya abiria sababu ndio yanatembea na pesa muda wote, na pia kuliko kupoteza root moja kwa siku kwa kupotezewa muda na askari ni bora kumpa hela uendelee na mishe.Tatizo la wabongo ni waoga sana kuhoji. Kitendo cha huyo mtu kutokuwa na uniform tayari kunatia shaka kiasi cha kuhalalisha maswali.
Ila ndio maana anafuata magari ya abiria maana anajua mengi yao huwa hayapo kamili kivibali.
Sababu wanatenda makosa kimakusudiKwanini nao wanakubali kutapeliwa?