Polisi kupewa lengo na serikali kukusanya mapato ni sawa?

NTABWENKE

Senior Member
Aug 19, 2011
135
39
Muda mchache uliopita nilikuwa natoka KIA naelekea A Town, nikampa lift askari mmoja wa usalama barabarani ndipo nikaipata hii habari, kuwa jeshi la polisi nalo limepewa lengo la kukusanya mapato kiasi cha 1.7b kwa mwaka na kwamba makosa yameongezwa kutoka 15 hadi 30 hivyo kila askari wa usalama anatakiwa kukamata kosa moja kwa siku ili hilo kosa litozwe faini, hivyo kwa mwezi kila mmoja awe amekamata makosa 30 ili kufikia lengo, zaidi ya hapo unaweza ondolewa kwenye hicho kitengo. Na inasemekana baada ya TRA wanaofuata ni Polisi kwa ukusanyaji wa mapato. Swali ninalojiuliza hawa polisi wanabiashara gani hadi wapangiwe lengo? Na je kazi yao ni kujitahidi kupunguza makosa au ni kuyaongeza uli kupata fedha kufikia malengo? Na kuwa POlisi siku hizi ni sehemu ya mapato ya serikali? Tujadili.
 
Serkali ikitaka pata ela ya kutosha fine iwe wekundu maana ela nyingi zaenda kwa matrafiki kama rushwa
 
Hizo 1.7 bl ni kwa mkoa wa ARUSHA tu kila mkoa una lengo lake, hii ni mbali na za mifukoni. Na wakifikia lengo wanapewa barua za pongezi.
 
Wacha wapewe, wanakula hela zetu tu, vitambi hivyo. Tena hilo kosa moja ni dogo wangepewa hata ishirin kwa cku
 
​ongezeko la fine si ndio kukubali makosa yaongezeke?badala ya kuhakikisha yanapungua
 
Bora pesa iende serikalini kuliko kuishia mifukoni mwao matrafik. Na sisi raia tutashika adabu kuendesha magari mabovu na kuendesha bila nidhamu na kusababisha miajali.
 
Back
Top Bottom