kavulata
JF-Expert Member
- Aug 2, 2012
- 16,247
- 16,169
Kinachosababisha watu wampuuze Polepole kile anachokisema kuhusu siasa ni ile historia yake ya kuwa kiongozi muhimu wakati wa serikali ya Magufuli. Polepole angeweza kumshauri Magufuli aandike katiba mpya ya serikali 3 lakini hakufanya hivyo
Polepole angeweza kumshauri Magufuli asivifungie vyama vya siasa kufanyakazi zao za kikatiba lakini hakufanya hivyo.
Polepole angeweza kumshauri Magufuli awatafute wahuni waliompiga risasi Lissu lakini hakufanya hivyo.
Polepole angeweza kumshauri Magufuli asimchague Samia kuwa makamu wa Rais wake lakini hakufanya hivyo
Polepole alikuwepo wakati mifuko ya hifadhi inaporwa fedha zake na wastaafu kukosa fedha zao lakini alikaa kimya.
Polepole anafahamu kuwa wajumbe wa Mkutano MKuu wa CCM wana akili zao timamu pengine kuliko yeye lakini yeye anawaona wajumbe wote hawana akili na hawana wanachokijua kuhusu CCM kuliko yeye.
Polepole anajikasimisha jukumu zito sana la kuitetea CCM na Tanzania bila kutaja jukumu hilo amepewa na akina nani. Yaani yeye anakijua chama kuliko wajumbe wote wa CCM na ana uchungu na tanzania kuliko watanzania wengine
Polepole alikaa kimya alipowasikia wahuni wakijitokeza hadharani kutaka kubadilisha katiba ili kuongeza muda wa ukomo wa Rais madarakani. Hoja hii haikukutana na hasira kubwa na kali kutoka kwa yeyote, kuonyesha kuwa jambo la kubadilisha katiba kuongeza muda lilikuwa linazungumzika wakati muda ukifika. Walikuwa wanapima atmosphere ya huko nje tu
Polepole huyu alikaa kimya wakati Mzee Warioba anachapwa kibao.
Polepole ni kama vile anahitaji msaada ya matibabu kuliko kumshangaa na kumsakama. Hajui kama amekalia kuti kavu kama walilokalia wezake waliowahi kukalia makuti makavu kama Mzee Makamba, Kinana, Lowasa, Mzee Aboud Jumbe, Sharif, Kingunge, Kolimba, Sumaye, Msindai, Kambona, Membe, Mrema, John Malecela, Salmin, Ali Karume, Nape na wengine wengi wasio na idadi. Anataka kuangua dafu moja kwa kuutikisa mnazi mzima. Ana umri gani yeye wa kuifahamu CCM kiasi hicho?
Polepole angeweza kumshauri Magufuli asivifungie vyama vya siasa kufanyakazi zao za kikatiba lakini hakufanya hivyo.
Polepole angeweza kumshauri Magufuli awatafute wahuni waliompiga risasi Lissu lakini hakufanya hivyo.
Polepole angeweza kumshauri Magufuli asimchague Samia kuwa makamu wa Rais wake lakini hakufanya hivyo
Polepole alikuwepo wakati mifuko ya hifadhi inaporwa fedha zake na wastaafu kukosa fedha zao lakini alikaa kimya.
Polepole anafahamu kuwa wajumbe wa Mkutano MKuu wa CCM wana akili zao timamu pengine kuliko yeye lakini yeye anawaona wajumbe wote hawana akili na hawana wanachokijua kuhusu CCM kuliko yeye.
Polepole anajikasimisha jukumu zito sana la kuitetea CCM na Tanzania bila kutaja jukumu hilo amepewa na akina nani. Yaani yeye anakijua chama kuliko wajumbe wote wa CCM na ana uchungu na tanzania kuliko watanzania wengine
Polepole alikaa kimya alipowasikia wahuni wakijitokeza hadharani kutaka kubadilisha katiba ili kuongeza muda wa ukomo wa Rais madarakani. Hoja hii haikukutana na hasira kubwa na kali kutoka kwa yeyote, kuonyesha kuwa jambo la kubadilisha katiba kuongeza muda lilikuwa linazungumzika wakati muda ukifika. Walikuwa wanapima atmosphere ya huko nje tu
Polepole huyu alikaa kimya wakati Mzee Warioba anachapwa kibao.
Polepole ni kama vile anahitaji msaada ya matibabu kuliko kumshangaa na kumsakama. Hajui kama amekalia kuti kavu kama walilokalia wezake waliowahi kukalia makuti makavu kama Mzee Makamba, Kinana, Lowasa, Mzee Aboud Jumbe, Sharif, Kingunge, Kolimba, Sumaye, Msindai, Kambona, Membe, Mrema, John Malecela, Salmin, Ali Karume, Nape na wengine wengi wasio na idadi. Anataka kuangua dafu moja kwa kuutikisa mnazi mzima. Ana umri gani yeye wa kuifahamu CCM kiasi hicho?