Mr Pixel3a
JF-Expert Member
- Sep 15, 2021
- 5,053
- 7,265
Mkufunzi wa shule ya uongozi Eng. Hamfrey Polepole amevishutumu vyombo vya kibeberu IMF na World Bank kwa kusababisha umasikini mkubwa na utegemezi wa milele kwa kutoa mikopo kandamizi kwa nchi masikini Kama Tanzania, na ameionya Serikali iliyopo madarakani kuwa makini na mikopo hiyo.
Wananchi wa Kenya waliandamana kupinga mkopo uliokopwa imf nchini Kwao Ila hata Tanzania juzi imekopeshwa mkopo mkubwa wa Tsh 1.3 trilioni na pole pole anasema huko ni kuingia katika mdomo wa mamba yaani ukoloni mamboleo chini ya mabeberu.
Mkufunzi huyo mzalendo ambaye alidai serikali imepigwa photocopy alienda mbali na kumkemea Amos makala RC wa Dar kuwa aache kunyanyasa masikini wamachinga, Bali atende haki. Huyu hapo chini
Wazee was kuunda tatizo na kulitatua