Masiya
JF-Expert Member
- Apr 2, 2012
- 7,602
- 7,343
Najua katika muda wote wa udahili tumelalamika sana, wengine wametukana sana na kadhalika. Ni kweli kumekuwa na magumu na machungu mengi yamewasibu na yanawasibu waombaji (haya yote yamelalamikiwa humu). Lakini nauliza tumewahi kufikiria yepi yanawasibu maafisa udahili ambao inabidi wafanye kazi na mifumo hii? Mko wachache simu zinapigwa usiku na mchana, mifumo inazingua, TCU wanawapa deadline lakini multiple selection ndio zinachanja kabla ya kujua mna nafasi ngapi zimebakia mnatakiwa mfungue dirisha lijalo. Code ndio hazijulikani zinaenda vipi. Na kadhalika. TCU/NACTE wanabana na Management ya Vyuo inabana-kabla ya saa nne usiku hujatoa mguu ofisini. MIMI NAWAPA POLE KWA KAZI NGUMU MNAYO PAMBANA NAYO KWA UJUMLA (hata kama kati yenu kuna wenye matatizo). Baada ya zoezi hili nafikiri itakuwa vizuri mkatafakari UPYA mfumo mzima na kutoa maoni yenu jinsi ya kuuboresha ili mwakani tusirudi tena hapa-hasa hapo KWENYE MATATIZO YA MULTIPLE SELECTION. Sisi tunahamia HESLB ni zamu yao kuwananga sasa.