Mzito Kabwela
JF-Expert Member
- Nov 28, 2009
- 18,857
- 7,618
Nijuavyo mimi, alichokosea Majaliwa ni kusema anaunda Tume yeye kama yeye....alitakiwa kusema ametumwa na nanihii kuunda tume na ripoti itapelekwa kwa nanihii kwa maamuzi....Katika mazishi ya kitaifa ya ndugu zetu walio fariki kwa ajali ya moto pale Morogoro ulitueleza tena kwa sauti ya msisitizo kuwa unaunda Tume ili itoe ripoti kama kuna uzembe wa vyombo vya usalama (ambao upo) na nani anastahili kuwajibishwa.
Leo idadi ya vifo imefikia 101 na siku tatu za kutoa taarifa tume yako zimezaa na kuwa wiki kadhaa.
Mtaani kuna fununu kuwa umeagizwa kutoka "juu" uachane na hayo mambo jee ni kweli ilikuwa funika kombe mwanaharamu apite? Na huko juu wanakozuia uachane na hayo jee wanahusikaje na vifo hivyo?
Tunaamini wewe una tofauti na wao, tuambie tume yako ina majibu gani na hatua gani zimechukuliwa kwa wazembe walio shindwa kuzuia