Ahsante sana P,
Huyu mama anasema ameishi miaka yote hiyo na hajawahi kumsimulia mtu yeyote mambo yake hadi alipoamua kunisimulia mimi baada ya kukutana kwenye net. Amejitahidi sana na anasema anampenda mume wako. Hata akisafiri lazima atamfuatilia kwe sms nzuri na kumpigia simu. Ila mume akipiga basi kuna shida au kuna kitu anataka kuuliza. Na anasema sms kutoka kwa mume wake ziko dry sana zaidi ya amri ya afande!
=Preacher;1376829
1. Maombi ya mtu mmoja ni tofauti sana na maombi ya mapatano - atafute waombaji wawili au zaidi (walio rohoni) wafunge na kuomba pamoja kwani Mungu anasema "lolote mtakalopatana duniani na kuomba, nitafanya"
2. Ajichunguze alimwomba Mungu ampe mume au alikurupuka? Kama alikurupuka, aombe sala ya toba kwanza.
3. Ajue kwenye maisha kuna majaribu mengi - alichukulie kama jaribu na aelewe kwenye kila jaribu kuna mlango wa kutokea hivyo asikate tamaa
4. Amsamehe mumewe aendelee kumhudumia, kumpenda na kujali familia yake (afanye wajibu wake)
5. Amwombee pia huyo mumewe - nguvu za giza zimtoke
Labda huyu mume ana wapenzi wengine na anamfanyia visa ili aondoke .............yeye asiondoke kwani mume huyo ni haki yake.
6. Awe pia na ujasiri wa kumwuliza mume wake - asimwogope - amwulize ............kulikoni???????????
Hope ushauri wangu utasaidia.[/
ka ushauri kangu kadogo kwako mtu mzima,usije ukaanza 'yale mambo yetu' na huyu mama(maana kaumizwa na hujui kwanini of all the people ka-open up kwako tu)hata kama ni mtandaoni.mzee usije ukapatwa huruma ukaona umpe bi mkubwa faraja ukijua ni kwenye net tu.ya watu kuchinjwa na strangers huanza hivihivi.Au pia inawezekana ukawa ni mtego mama chanja wako baadae akakuchombeza(kimtego)mzee ukafumaniwa mtandaoni.ni hayo tu mkubwa.
Mimi namshauri a (MULTPLY HIS PRESENCE BY ZERO), yani azidishe na sifuri tu, maana kila namba ukizidisha na sifuri ataendelea kupata sifuri. Kama hana ulemavu ni wakati wake wa kufanya kazi kwa bidii zote ili awalee wanae wawili ambao ni zawadi toka kwa Mungu. Akipata muda wa kupumzika atoke na wanae akajipe raha nje ya nyumbani. Kama ana marafiki awapigie simu na kuchat kama anavyofanya yeye."Amelaaniwa yule amtumainie mwanadam"matatizo haya si yy peke yake,wako watu wengi sana miaka ya sasa,waume kwa wake,yy aendelee kuwa mke mwema mwenye kuitunza na kuipenda familia yake,kumpa mumewe huduma kila kinyongo.chakula,maji mipango etc(najua ni ngum sana)lkn pia aangalie wapi alipokosea yy kama mke,kuomba ushauri ni jambo jema maana ndio hasa anapopata Amani ndani ya moyo wake,lkn pia aangalie si kila mtu ni wa kuomba ushauri.Kila mtu aliletwa duniani kwa dhumuni la Mungu na si mwanadam hivyo amtangulize Mungu ktk kila jambo na aamini kila kitu kina mwisho wake.Pole sana Mama.
wako wengi sana DCHii ni story ya mwanamke mmoja ambaye nimekutana naye katika harakati za kupeana ushauri wa kutatua matatizo yanayotusibu katika mahusiano. Amekubali niiweke hapa ili kupata maoni ya wadau. Matatizo yake ni mengi sana ila kwa ufupi ni kama ifuatavyo:
1. Suala na unyumba katika ndoa yao yenye umri wa karibia miaka 4 wakiwa na watoto 2, limekumbwa na ukame wa ajabu. Wanashiriki tendo la ndoa kama mara 2 tu kwa mwezi na ni lazima mume atake. Mwanamke akiomba anaambiwa kuwa mume hawezi kufanya tendo la ndoa mara kwa mara. Wakati wa uchumba wao na siku za awali za ndoa yao, walikuwa wakishiriki tendo la ndoa hata zaidi ya mara 2 kwa week na wote waliliridhika na kufurahia tendo hilo. Hali ilianza kubadilika baada ya kama miaka 2 hivi. Mbaya zaidi hata kama mmoja akirudi safari baada ya kukaa kwa muda mrefu kiasi cha week nzima au zaidi, bado hakuna uhakika wa tendo la ndoa!
2. Mawasiliano ndani ya nyumba hasa hasa yale ya kimahaba nalo limekuwa tatizo. Yaani ni kama vile wanaishi maktaba. Muda mwingi mume akiwa nyumbani anacheza na simu yake akituma na kupokea sms kutoka kwa watu tofauti. Pia mume akiwa nje na jamaa wengine anakuwa mchangamfu sana, akiongea na vicheko juu.
3. Vitu vingi vya mume vimefunigiwa katika mkoba (brief case) wenye password ambayo mke hajui. Pia mume anazo account za benki ambazo mke wake hazijui kabisa. Na simu za mume zimewekewa password ingawa vitu vyote vya mke ikiwemo simu, account za bank n.k viko wazi na mume anavivinjari wakati wowote anaopenda.
4. Ni nadra kwa mume kukubali na kusifia (to appreciate) kitu alichokifanya mke. Na mara nyingi anamkatisha tamaa katika mipango yake anayomshirikisha.
Kutokana na haya matatizo na mengine mengi, huyo mama amekosa raha muda mrefu na aliwahi kufikiria kujidhuru (got closer to attempt suicide) ila kwa sasa ameamua kutafuta ushauri ama wa kuokoa ndoa au maisha yake. Amesali sana, amfeunga sana na kubadili makanisa kama nguo za mashidano ya mavazi lakini bado nazunguka pale pale. Kwa hiyo wadau nawaomba ushauri wenu ili niongeze kwenye package ya counseling ninayoendelea nayo kwa sasa.
Wasalaam, ....Babu DC
Mkuu huu wasi wasi unatokea wapi? Kama angekuwa ni mwanamume mwenzangu ndo ameniomba ushauri ungesema hivyo? Halafu mbona watu kibao wanaomba ushauri kila siku na tunajadiliana na kubadilisha mawazo yanaisha? Na je huamini kwamba kuna watu wanatoa huduma kama hizi professionally?
Nadhani wanaume tuna tatizo kubwa. Kwani kila mwanamke lazima utembee naye? Mbona wapo wengi wamenizunguka. Iweje nihangaike na vivuli vya kwenye mtandao?
Hata hivyo jaribu kufuatilia DC ni mtu wa namna gani linapokuja suala la personal intergrity tena kwenye mambo ya ndoa. Vinginevyo wasi wasi wa namna hiyo unaweza kuwa unatupa picha yako mwenyewe.
[/COLOR]
samahani sana,labda umenielewa vibaya.angekua mwanaume pia ningesema nilichosema kwani msisitizo wangu sana ulikua,kama amepata pa kuongelea matatizo yake(kakuamini na kufunguka kwako),uhusiano waweza kukua toka mtandaoni hadi kukutana uso kwa uso,na huyu ni mgeni kabisa kwako,humfahamu,hata hujui kama anachokwambia ni ukweli halisi au vipi.sasa kutokana na matukio kadhaa niliyosikia na kusoma kuhusu watu waliodhuriwa na strangers(kwani wengi walikutana na watu au hadithi tofauti na walizosikia mtandaoni)waz just tryna be cautious mzee!natambua wapo wanaofanya hivi proffessionaly,umakini tu ndo ulikua msisitizo wangu,sijui hata umeelewa kitu gani.
Kuhusu your personal integrity,mi sio mgeni sana hapa japo sidhani kama pia toka kwenye post tu unaweza pata picha halisi ya mtu(mi si mtaalam wa mambo haya) ila kwa niliyo highlight hapo inanifanya nifikiri zaidi kuhusu hiyo P.I.yako.zaidi sana,SAMAHANI SANA KAMA NIMEKUKWAZA!