Platnumz na Bayport wafutiwe leseni

Platnumz na Bayport wafutiwe leseni

devinyo1987

JF-Expert Member
Joined
Mar 12, 2021
Posts
266
Reaction score
372
Ndugu wanaJF, Mim ni mwalimu nilipata shida ya dharura mwaka 2014 nikakopa mkopo wa chap chap hapa Platnum lakini mwisho wa kulipa ulikuwa ni mwaka 2019. Nashangaa hadi leo wananikata deni, nimejaribu kufuatilia ofisi zao makao makuu hakuna msaada nataka niwashitaki

Hata hivyo ningeshauri hawa Bayport na Platnum wakaguliwe ni matapeli wanaongezea watu madeni ya ajabu na hata ukitaka kusitisha mkopo hawakubali ni wasumbufu.

PLATNUM NA BAYPORT siyo bank za kukopa ni matapeli bora ufe na njaa kuliko hawa wazandiki. Wafutiwe leseni matapeli wakubwa hawa.
 
Swali: Mko wangapi wenye malalamiko kama ya kwako?

Sina shida ya kuwatetea lakini nadhani kama wangekuwa na mapungufu sidhani kama wangeendelea kuwepo mpaka leo.

Na kama una ushahidi tatizo ni nini kwenda kwenye mamlaka zinazohusika upate haki yako?.
 
PLATNUM NA BAYPORT
sio bank za kukopa ni matapeli bora ufe na njaa kuliko hawa wazandiki .....wafutiwe leseni matapeli wakubwa hawa
Hahahahaa..

Mkuu, kwani ulikopa ngapi, kwa riba gani, na umekatwa ngapi hadi sasa?
 
Hahahahaa..

Mkuu, kwani ulikopa ngapi, kwa riba gani, na umekatwa ngapi hadi sasa?
Eeeh atueleze ukweli tupige hesabu hapa

Ni kweli Platinum, BayPort na Blue Finance wana matatizo ila sio matatizo ya kuzidisha kukata mkopo hata ukimaliza

Ujanja wao uko kwenye riba za hivyo hivyo na hapo ndo wengi wanapoibiwa. Anachoongea na afisa mikopo na kilicho kwenye mikataba vinakua having uwiano. Ila kwakua watu wengi huwa wana haraka tu ya kuzishika hela mkononi wanasaini haraka haraka. Hapo ndo unajikuta unakatwa mkopo miaka 10
 
Usipoteze muda kuja kulalamika huku mitandaoni. Chukua mkataba wako na hao BYPORT/PLATINUM nenda nao kwa mawakili wape maelekezo yako halafu waachie waupitie kifungu kwa kifungu huo mkataba kati yako na hizo kampuni. Kama wakiona jamaa wanakuibia basi unawauzia kesi unaingia nao mkataba nao unasubiri mpunga. Siku hizi mawakili wapo wengi sana wanasubiri watu waliodhulumiwa kama nyie ili wawasaidie mpate haki zenu na wao wapate chochote kitu. Wewe unalia lia huku mitandaoni wakati unaweza kukuta una mamilioni yanakusubiri kutokana na uonevu wa hizo kampuni.

Lakini angalizo kwa mleta uzi wengi wenu nimeona huwa mnasaini hiyo mikataba kizembe bila hata kuisoma kipengele kwa kipengele kwa sababu mna shida na mnataka pesa haraka haraka basi manaanguka tu saini. Hizo kampuni hakuna haja ya kuzifutia leseni ila wakipatikana watu wawili au watatu wakadai haki zao mahakamani na wakashinda wakalipwa mamilioni lazima watajirekebisha tu.
 
Ndugu wanaJF, Mim ni mwalimu nilipata shida ya dharura mwaka 2014 nikakopa mkopo wa chap chap hapa Platnum lakini mwisho wa kulipa ulikuwa ni mwaka 2019. Nashangaa hadi leo wananikata deni, nimejaribu kufuatilia ofisi zao makao makuu hakuna msaada nataka niwashitaki

Hata hivyo ningeshauri hawa Bayport na Platnum wakaguliwe ni matapeli wanaongezea watu madeni ya ajabu na hata ukitaka kusitisha mkopo hawakubali ni wasumbufu.

PLATNUM NA BAYPORT siyo bank za kukopa ni matapeli bora ufe na njaa kuliko hawa wazandiki. Wafutiwe leseni matapeli wakubwa hawa.
Hayo makato kwanini usiwasiliane na Mwajiri wako asitishe??
 
Kama umejiridhisha na mkataba wako nenda FCC kama sikosei inaitwa Fair Competition Commission watakusaidia vizuri sana
 
Ndugu wanaJF, Mim ni mwalimu nilipata shida ya dharura mwaka 2014 nikakopa mkopo wa chap chap hapa Platnum lakini mwisho wa kulipa ulikuwa ni mwaka 2019. Nashangaa hadi leo wananikata deni, nimejaribu kufuatilia ofisi zao makao makuu hakuna msaada nataka niwashitaki

Hata hivyo ningeshauri hawa Bayport na Platnum wakaguliwe ni matapeli wanaongezea watu madeni ya ajabu na hata ukitaka kusitisha mkopo hawakubali ni wasumbufu.

PLATNUM NA BAYPORT siyo bank za kukopa ni matapeli bora ufe na njaa kuliko hawa wazandiki. Wafutiwe leseni matapeli wakubwa hawa.
Pole sana kwa maumivu unayopitia. Kwanza nikuambie ukweli, hizo taasisi siyo za kitapeli kama unavyodhani. Ni taasisi zilizo sajiliwa kihalali kabisa kuendesha shughuli za kifedha zikiwemo hizo za kukopesha! Zina leseni za kuendesha hizo biashara, na zinalipa kodi ya serikali.

Tatizo ndugu lipo kwako! Ulichukua mkopo wao kwa kuyasikiliza maneno matamu na ya uongo kutoka kwa wale maafisa wao wa mikopo. Na hukuusoma mkataba, na pia hukumshirikisha mwanasheria. Ulichofanya ni kusaini tu zile karatasi za mkataba, na kusubiria tu mzigo kuingia kwenye akaunti yako ndani ya masaa 24!

Ukweli ni huu; Hizo taasisi zina riba kubwa sana. Na sababu ni kwamba, na zenyewe zinakopa kwenye mabenki haya ya kawaida ili kuendeshea hizo shughuli zao. Na mbaya zaidi inawezekana kabla ya mkopo wako kuisha, walikushawishi kutop up kwa kigezo cha kukupa hela nyingi zaidi! Lakini mwisho wa siku ukaambulia hela kidogo, huku makato na miaka ya kumaliza deni ikiongezeka.

Njia za kufanya: Kawaombe wakupe mchanganuo wa mkopo wako. Ili uone ulipo anzia, na unapo ishia. Baada ya hapo, nenda kwa afisa utumishi ukaombe mwongozo. Kama haiwezekani, nenda CWT! Maana na wenyewe wanakula 2% ya mshahara wako kila mwezi uone kama nao watakusaidia.

Na mwisho kabisa, uwe balozi kuanzia sasa kwa walimu wenzako na hasa hawa walio ajiriwa hizi siku za karibuni, na watumishi wengine wenye tamaa ya mikopo ya haraka, kwenda kukopa kwenye benki zinazo tambulika kama crdb, nmb, tpb,nbc, nk. Badala ya kwenye taasisi za kifedha kama hizo platinum credit, bayport, faidika, nk.
 
Shida ni kitu kibaya sana, Mambo yakiwa magumu hata kusoma mkataba wao unaona ufala unachojali mpunga uingie kwenye akaunti, pesa ikiisha akili ndo inarudi taratibu 😂😂😂😂
 
Kuna kipindi kuna mjumbe alileta mrejesho mzuri tu, alienda akawafanyia vurugu za maana sana hadi wakampa haki take. Sikumbuki ule Uzi unaitwaje, usiende kiboya watakudharau yaani nenda kama faru akiyejeruhiwa, mbona watatafutana tu!
 
Ndugu wanaJF, Mim ni mwalimu nilipata shida ya dharura mwaka 2014 nikakopa mkopo wa chap chap hapa Platnum lakini mwisho wa kulipa ulikuwa ni mwaka 2019. Nashangaa hadi leo wananikata deni, nimejaribu kufuatilia ofisi zao makao makuu hakuna msaada nataka niwashitaki

Hata hivyo ningeshauri hawa Bayport na Platnum wakaguliwe ni matapeli wanaongezea watu madeni ya ajabu na hata ukitaka kusitisha mkopo hawakubali ni wasumbufu.

PLATNUM NA BAYPORT siyo bank za kukopa ni matapeli bora ufe na njaa kuliko hawa wazandiki. Wafutiwe leseni matapeli wakubwa hawa.
Pole mwalimu kama kawaida yenu mnapigwa na CWT, CCM, Bayport, Credit, Faidika sasa na Platinum, na bado mnashangilia.
 
Walienda kuzoa bure dollar za watu wakaacha vikampuni uchwara vya kijambazi...BOT sijui huwa wanafanya kazi gani kwa kweli kuhusu usimamizi wa vikampuni vya uongo kwenye mambo ya mikopo...
 
Miradi
Ndugu wanaJF, Mim ni mwalimu nilipata shida ya dharura mwaka 2014 nikakopa mkopo wa chap chap hapa Platnum lakini mwisho wa kulipa ulikuwa ni mwaka 2019. Nashangaa hadi leo wananikata deni, nimejaribu kufuatilia ofisi zao makao makuu hakuna msaada nataka niwashitaki

Hata hivyo ningeshauri hawa Bayport na Platnum wakaguliwe ni matapeli wanaongezea watu madeni ya ajabu na hata ukitaka kusitisha mkopo hawakubali ni wasumbufu.

PLATNUM NA BAYPORT siyo bank za kukopa ni matapeli bora ufe na njaa kuliko hawa wazandiki. Wafutiwe leseni matapeli wakubwa hawa.
Miradi ya kuumiza watumishi wa umma.( Walimu)
 
jamaa kweli ni aakurupuka!

amekurupuka kukopa mkopo bila kusoma wakamchapa!

amekurupuka kuandika uzi jf na wadau wanamshusha wenge.

naona kama kautelekeza uzi wake.
ticha acha kukurupuka
 
Mkuu kwanza tuliza akili maana naona ktk uzi wako umechanganya issues. Moja, aliyekupiga ni Platnum lakini wewe kwenye kichwa cha uzi wako umewaingiza hadi Bayport. Pili, unachotakiwa kudai wewe ni kupata haki yako na siyo kupendekeza hizo taasisi kufutwa.Inavyo onekana kwako wewe ni kuwa zikifutwa utafurahi hata kama hukupata haki yako, hiyo siyo sawa mkuu.
 
Usipoteze muda kuja kulalamika huku mitandaoni. Chukua mkataba wako na hao BYPORT/PLATINUM nenda nao kwa mawakili wape maelekezo yako halafu waachie waupitie kifungu kwa kifungu huo mkataba kati yako na hizo kampuni. Kama wakiona jamaa wanakuibia basi unawauzia kesi unaingia nao mkataba nao unasubiri mpunga. Siku hizi mawakili wapo wengi sana wanasubiri watu waliodhulumiwa kama nyie ili wawasaidie mpate haki zenu na wao wapate chochote kitu. Wewe unalia lia huku mitandaoni wakati unaweza kukuta una mamilioni yanakusubiri kutokana na uonevu wa hizo kampuni.

Lakini angalizo kwa mleta uzi wengi wenu nimeona huwa mnasaini hiyo mikataba kizembe bila hata kuisoma kipengele kwa kipengele kwa sababu mna shida na mnataka pesa haraka haraka basi manaanguka tu saini. Hizo kampuni hakuna haja ya kuzifutia leseni ila wakipatikana watu wawili au watatu wakadai haki zao mahakamani na wakashinda wakalipwa mamilioni lazima watajirekebisha tu.
Mkuu unachoongea ni sahihi, mwezi Jana nilipata shida ya 2M hivyo ikabidi nipite Ofisi ya faidika ili nikope kiasi tajwa,kilichonishangaza ni kuwa nilipewa fomu ya mkopo ni saini harafu niwaache maafisa mkopo wakijaza taarifa za mikopo,mfano kiasi nilichochukua na makato,nilishangaa sana,hapa ndo watu wanapopigwa wakikutana na maafisa wahuni,imagine umesaini fomu ukaondoka na kumuacha afisa mikopo akijaza taarifa za mkopo huoni kuwa anaweze jaza kiasi chochote anachotaka na ukitaka kumpeleka mahakamani lazima akushinde maana ulisaini mwenyewe bila kuona kilichojazwa.


Watumishi tuwe makini tofauti na hapo tutazidi kuibiwa na kubaki kulalama,nilichofanya nilimwambia ajaze fomu yote anipe nisome taarifa zote na ndo nisaini na baada ya hapo nikaiscan fomu Kama kielelezo Cha baadae.

Naamini mtoa mada na wewe utakuwa ulijisahau katika ujazaji wa mkataba hapo ndo chanzo Cha maumivu yako.
 
Back
Top Bottom