Kifupi naomba nikushirikishe jambo hili nilikuwa kwenye mahusiano na binti mmoja kipindi hicho nipo chuo mwaka wa kwanza mpaka mwaka huu almost four years. NilijitahidI kumtimizia kila nilichoweza kimahitaji kama mpenzi Wangu. Nikamtambulisha kwetu na kwao kwa ahadi ya kuoana nae mwishoni mwaka huu.
But nilImkuta na vitu vya ajabu mno kwenye simu yake nikawa mpole but yalinishinda ikabidi tufikishane mpaka kwa mzazi wa binti mamaye mama akakiri mwanae hajatulia akaniomba msamaha kwa niaba ya binti yake mapema mwaka huu.
Kiukweli nilmkuta hana support ya wazazi nikamlea kwa kila kitu nikiamini atakuwa mke sahihi, but baada ya ugomvi ule niliamua kukaa pembeni kukaa kimya.
Tukaachana na binti but toka nimeachana nae amekuwa akizungumzia maneno machafu mengi kwa rafiki yake but kiukweli sikuwahi kuwajibu chochote hao rafki zake nliamua kukaa kimya but kila siku yanazungumzwa mapya na ni almost miezi sita imepita since tulivooachana.
So wanajamvi wenzangu nifanye lipi nimfate laivu nimpe makavu au niendlee na maisha mengne?