Pita hapa nikukumbushe jambo moja zuri sana, Kisha uliishi na ukapate baraka, ukabalikiwe

Pita hapa nikukumbushe jambo moja zuri sana, Kisha uliishi na ukapate baraka, ukabalikiwe

Beira Boy

JF-Expert Member
Joined
Aug 7, 2016
Posts
23,961
Reaction score
42,166
Amani iwe nanyi watumishi wa MUNGU katika KRISTO

Neno la MWENYEZI MUNGU katika kitabu cha nabii yeremia 2:19 neno linasema, uovu wako mwenyewe utakurudi maasi yako yatakukaripia, ujue basi, ukaone ya kuwa ni jambo baya sana na uchungu, kwa kuwa umemwacha, BWANA, MUNGU wako, na ya kuwa moyoni mwako hakuna kunihofu, asema BWANA, Bwana wa majeshi

Neno hilo ndugu zangu wana wa MUNGU linasisitiza juu ya ubaya wa kumwacha MUNGU na kutokumhofu MUNGU MWENYEZI MFALME WA WAFALME

Kumwacha MUNGU kupo kwa aina nyingi, kwa mfano
1, kutokufanya mazoez ni kumwacha MUNGU
2, kukata miti ovyo ni kumwacha MUNGU
3, usela mwingi ni kumwacha MUNGU
4, kutokufanya ibada ni kumwacha MUNGU

Hiyo ya nne ndo kubwa zaid
5, kutokuwajali masikin na wahitaji ni kumwacha MUNGU
6, kutokuwaombea wengine mbele za MUNGU nako pia ni kumwacha MUNGU

Nitaifafanua hiyo namba 6, mkristo ambaye anaanza maombi kwa kujiombea yeye mwenyewe pasipo kuanza kuwaombea wengine huyo hafai na amemwacha MUNGU kabisa , tujifunze kuwaombea wengine hasa VIJANA, MAFISADI, WAGONGWA, WAJANE, YATIMA, WASAFIRI , WANANDOA , WAGANE

kwanini tuwaombee VIJANA, kwa sasa hapa dunian vijana ndo kundi linatoseka zaid kuanzia elimu, mahusiano, ajira na kipato, vijana wengi huamka asubuhi wakiwa hawajui wanaenda kufanya kazi wapi na kazi ipi

Basi ndugu zangu tuwatie moyo vijana na tuwaombee sana kwa MWENYEZI MUNGU

Tuendelee kudumu mbele za MWENYEZI MUNGU bila kuchoka

Asanten sana watumishi

BWANA awabariki

SAYUNI BOY
 
Ubalikiwe sana wengi kwenye maombi huwa tunaanza kulia na shida zetu kwanza
 
Back
Top Bottom