Kwanza nianze kwa kusema ninamheshimu sana Waziri mkuu wangu Pinda, ajiitaye mtoto wa mkulima, lakini kwa hili la kutoa hoja dhaifu kuhalalisha posho za vikao naomba kutofautiana naye.Hebu tujikumbushe hoja hizi ambazo kimsingi sikutegemea kama zingetolewa na mtu anayetegemewa kuwa makini kama Waziri mkuu wa nchi, tena anayejiita mtoto wa mkulima. Hoja ya kwaza ni kwamba POSHO HIZI ZIKO KISHERIA na ya pili eti WABUNGE HATA HIVYO HAWAZITUMII WENYEWE BALI WANAWAPA WAPIGA KURA WAO.
Hoja hizi kama zisingetolewa na Pinda mtu ninayemheshimu, basi ningeziita HOJA HEWA.Lakini kwa vile ni Pinda sitaziita hivyo ila ntazijadili tu. Ntaanza na hoja ya kwanza eti hizi posho ziko kisheria. Kwanza Pinda ameshindwa kujielekeza katika hoja iliyokuwa mezani badala yake amechepuka na kujisemea lililokuja kichwani mwake. Hoja ya msingi haikuwa juu ya kama posho hizi ziko kinyume na sheria au la bali kilichokuwa kinatakiwa kujibiwa ni juu ya tuendelee kuwalipa wabunge posho au la.
Je kila kilichopo kisheria ni ni kizuri? au kila kilichopo kisheria kama kitaonekana kuwa kibaya hakiwezi kurekebishwa?.
Kwa swali la kwanza Jenerali Ulimwengu ashajibu, kwamba si kila kilichowekwa kisheria ni kizuri. Nami naongezea mfano hapa kwamba serikali ya Makabulu wa South Africa ilikuwepo kisheria na iliwabagua waafrika kwa mujibu wa sheria. Lakini hili halikuacha kupigiwa kelele ati kwa sababu jambo hilo(serikali ile) lilikuwepo kisheria. Pinda ni mwanasheria wote tunajua.Ina maana Pinda ashasahau juu ya Sheria mbaya (Unjust law). Kama amesahau, manake yupo katika siasa siku nyingi labda hasomi tena vitabu vya JURISPRUDENCE vinavyoeleza juu ya sheria mbovu na dawa yake nini (kamsome Sengodo Mvungi, The Right to Disobey Unjust Law, East African Law Review, 2003).
Kwa hiyo ni wazi Pinda amekataa makusudi kutwambia kama yeye mwenyewe na serikali yake yuko tayari kuandaa marekebisho ya sheria kuzifuta posho hizi. Kama ilivyo kwa watoto wa wakulima wengi, na mimi sikumwelewa kabisa Pinda.
Hebu twende katika hoja nyingine dhaifu mno iliyotolewa kutetea posho hizi, ya wabunge siyo wanaozitumia fedha hizi badala yake ni wapiga kura wao wanaoenda kuwaomba pale bungeni.Mimi nafikiri katika hili pinda anapaswa kuomba radhi kabisa kwani ni wazi amewatukana wapiga kura waliopo majimboni waliowapigia kura wabunge wale.We hebu jiulize ni wapiga kura wangapi kutoka Katavi anakotokea Pinda wanaenda viwanja vya Bunge kumwomba Pinda pesa.Au wale wakuu wa wilaya na madiwani wanaotamburishwaga katika bunge ndo wapiga kura wanaoombaomba pesa kutoka kwao?. Hivi ni wangapi wanatoka jimbo la Wawi kwenda Bungeni kumwomba hela Mh. Rashidi? wangapi kwa wiki Pinda twambie. Au wangapi wantoka Karagwe kwenda kumwomba bwana Katagira, mbunge wa kyerwa?.
Pili Pinda ni mkristo, tena amesoma seminali.Anaijua sana dini na ninaamini anamwogopa mungu. Sasa Pinda leo atwambie ametoa wapi andiko katika Biblia linalomwelekeza kuwasaidia maskini wanaotoka kwenye jimbo lake kumwomba fedhe kisha atangaze kwamba anawapa fedha hao ombaomba.Hii ni dhambi kubwa sana inayopaswa kuungamwa.Na kama hatofanya hivyo basi sidhani kama huruma ya mungu haina kikomo kwa mtu asiyejutia dhambi yake.
Hoja hizi kama zisingetolewa na Pinda mtu ninayemheshimu, basi ningeziita HOJA HEWA.Lakini kwa vile ni Pinda sitaziita hivyo ila ntazijadili tu. Ntaanza na hoja ya kwanza eti hizi posho ziko kisheria. Kwanza Pinda ameshindwa kujielekeza katika hoja iliyokuwa mezani badala yake amechepuka na kujisemea lililokuja kichwani mwake. Hoja ya msingi haikuwa juu ya kama posho hizi ziko kinyume na sheria au la bali kilichokuwa kinatakiwa kujibiwa ni juu ya tuendelee kuwalipa wabunge posho au la.
Je kila kilichopo kisheria ni ni kizuri? au kila kilichopo kisheria kama kitaonekana kuwa kibaya hakiwezi kurekebishwa?.
Kwa swali la kwanza Jenerali Ulimwengu ashajibu, kwamba si kila kilichowekwa kisheria ni kizuri. Nami naongezea mfano hapa kwamba serikali ya Makabulu wa South Africa ilikuwepo kisheria na iliwabagua waafrika kwa mujibu wa sheria. Lakini hili halikuacha kupigiwa kelele ati kwa sababu jambo hilo(serikali ile) lilikuwepo kisheria. Pinda ni mwanasheria wote tunajua.Ina maana Pinda ashasahau juu ya Sheria mbaya (Unjust law). Kama amesahau, manake yupo katika siasa siku nyingi labda hasomi tena vitabu vya JURISPRUDENCE vinavyoeleza juu ya sheria mbovu na dawa yake nini (kamsome Sengodo Mvungi, The Right to Disobey Unjust Law, East African Law Review, 2003).
Kwa hiyo ni wazi Pinda amekataa makusudi kutwambia kama yeye mwenyewe na serikali yake yuko tayari kuandaa marekebisho ya sheria kuzifuta posho hizi. Kama ilivyo kwa watoto wa wakulima wengi, na mimi sikumwelewa kabisa Pinda.
Hebu twende katika hoja nyingine dhaifu mno iliyotolewa kutetea posho hizi, ya wabunge siyo wanaozitumia fedha hizi badala yake ni wapiga kura wao wanaoenda kuwaomba pale bungeni.Mimi nafikiri katika hili pinda anapaswa kuomba radhi kabisa kwani ni wazi amewatukana wapiga kura waliopo majimboni waliowapigia kura wabunge wale.We hebu jiulize ni wapiga kura wangapi kutoka Katavi anakotokea Pinda wanaenda viwanja vya Bunge kumwomba Pinda pesa.Au wale wakuu wa wilaya na madiwani wanaotamburishwaga katika bunge ndo wapiga kura wanaoombaomba pesa kutoka kwao?. Hivi ni wangapi wanatoka jimbo la Wawi kwenda Bungeni kumwomba hela Mh. Rashidi? wangapi kwa wiki Pinda twambie. Au wangapi wantoka Karagwe kwenda kumwomba bwana Katagira, mbunge wa kyerwa?.
Pili Pinda ni mkristo, tena amesoma seminali.Anaijua sana dini na ninaamini anamwogopa mungu. Sasa Pinda leo atwambie ametoa wapi andiko katika Biblia linalomwelekeza kuwasaidia maskini wanaotoka kwenye jimbo lake kumwomba fedhe kisha atangaze kwamba anawapa fedha hao ombaomba.Hii ni dhambi kubwa sana inayopaswa kuungamwa.Na kama hatofanya hivyo basi sidhani kama huruma ya mungu haina kikomo kwa mtu asiyejutia dhambi yake.