Mfungaji wa penalti ya mwisho na ya ushindi ya Zanzibar, Abdallah Othman akikimbia kushangiloia baada ya kumaliza mechi ya Robo Fainali ya Kombe la Mataifa ya Afrika Mashariki na Kati, CECAFA Tusker Challenge dhidi ya Burundi kwenye Uwanja wa Lugogo mjini Kampala, Uganda, Zanzibar ilishinda kwa penalti 6-5 baada ya sare ya 0-0 ndani ya dakika 90.
Ndikumana chini, shughuli ya Issa Othman Ally kushoto
Aggrey Moris akimdhibiti mshambuliaji wa Burundi
Suleiman Kassim Selembe kulia anakokota ngoma
Abdulaghan Gullam akitafuta mbinu za kumtoka mchezaji wa Burundi
Aggrey Morris anapanda kusaidia mashambulizi baada ya kuokoa
Selembe anapasua katikati ya watu
Issa Othman Ally anaondoka na mpira mbele ya wachezaji wa Burundi
Jaku Juma akipambana na beki wa Burundi
Ndikumana akijuta baada ya kukosa penalti
Balozi wa Tanzania nchini Ugamda, kulia akimpongeza kocha wa Zanzibar
Wachezaji wa Zanzibar wakimpongeza Abdallah Othman
Wachezaji wa Zanzibar na baadhi ya viongozi wakimpongeza Abdallah Othman katikati aliyesujudu
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.