Picha za mkutano wa CHADEMA kata ya Kimandolu -Arusha

Nanyaro Ephata

JF-Expert Member
Jan 22, 2011
1,221
1,788
Wakuu
Leo tumeendelea na mikutano yetu ya hadhara ya kuzungumza na wananchi,na kusikiliza kero zao,leo tulikuwa kimandolu,na kesho tarehe 10.1.2012 tutakuwa Kaloleni.
 
Sawa mkuu, nawakubali! Makamanda kazini.., hicho ndo chama chenye kufuata misingi na taratibu za wapiga kura wake. Viva CHADEMA!
 
Wakuu
Leo tumeendelea na mikutano yetu ya hadhara ya kuzungumza na wananchi,na kusikiliza kero zao,leo tulikuwa kimandolu,na kesho tarehe 10.1.2012 tutakuwa Kaloleni.

mbona nimeona tangazo uswahilini linasema mkuu wa mkoa bwn magesa atakuwepo ofisi ya mtendaji kata ya kaloleni hiyo kesho?!
 
Wakuu
Leo tumeendelea na mikutano yetu ya hadhara ya kuzungumza na wananchi,na kusikiliza kero zao,leo tulikuwa kimandolu,na kesho tarehe 10.1.2012 tutakuwa Kaloleni.

Kwa mwendo huu tutawaona CDM wakiishia kuvutia mikutano mikubwa, lakini ukifika wakati wa uchaguzi sisiemu wakichukua utawala kwa kutumia UWT!!! Haki na utawala wa sheria ni kwa CDM, lakini kwa mtindo huu wa rule of the jungle sisiemu na magamba yake wataendelea kuangamiza taifa hili!!!!! Hivi zile siku 100 ndiyo ziliishia wapi?? au zilikuwa miongoni mwa mbinu za UWT??? Lakini mwelekeo wa uchumi utawaumbua tu na siku moja kichaa mmoja atasema enough is enough!!!!!!!!!!! Hapo???????????
 
asante kwa taarifa ( feedback - kuwa mkutano umefanyika kama ulivyo pangwa )

lakini hii taarifa ni too short haielezi nini kilijili huku muitikio wa watu ulikuwaje, Ni viongozi gani walikuwepo ,kadi mligawa ? etc

halafu title haimatch kabisa au ulichoka sana POLE NA UCHOVU MKUU

GOD BLESS YOU - AMEN !!!
 
asante kwa taarifa ( feedback - kuwa mkutano umefanyika kama ulivyo pangwa )

lakini hii taarifa ni too short haielezi nini kilijili huku muitikio wa watu ulikuwaje, Ni viongozi gani walikuwepo ,kadi mligawa ? etc

halafu title haimatch kabisa au ulichoka sana POLE NA UCHOVU MKUU

GOD BLESS YOU - AMEN !!!

OK labda nije kwa namna hii Mikutano yote ya CDM.imekuwa na mafanikio makubwa kuanzia ule wa nmc, kata ya Elerai na hata kimandolu watu wengi wameonekana kuwa na ari na wanahudhuria mikutano hata hii midogo ya kata tofauti na siku za nyuma ambako ili watu waje lazima waletwe wasanii mbalimbali ili kuhamasisha.

Wengine hawapendi kuja kwenye mikutano lakini wanasikiliza kwa mbali.

Kuna wale ambao wanakuwa kama wapita njia kwa miguu au kwa magari karibu na maeneo ya mikutano husitisha safari zao kwa nyakati fulani ili kusikiliza hotuba zenye kutoa taswira ya wapi tumetoka na tunakokwenda na nchi hii inawafaidisha wakina nani.

Mikutano hiyo inapokaribia kwisha ndipo utadhani inaanza maana watu wanaongezeka kuja kwa wingi na zaidi wakati wa kuondoka wengi hujitokeza barabarani na wakiwa na alama juu ya vidole viwili kuashiria kuiunga mkono chadema.

Na karibu mikutano yote watu wengi wamekuwa wakiwabana chadema kwenda kufungua matawi yao ya mitaa ya karibu na kufanya mikutano iwe na ladha ya tofauti.

Na kila mikutano hii inapofanyika inakuwa pia na polisi wengi wanaokuja kwa siri kusikiliza chadema wataongea nini ili wawakamate na wengine hurekodi kisirisiri na mpaka mmoja juzi alikamatwa kata ya Elearai na pia mara nyingi nimekuwa nawaona maofisa wa TISS wasiopungua watano wale ninaowafahamu na wanakuwa na mionekano ya tofauti kwa jinsi walivyo siku zote ili kujifanya ni wanachadema ili waweze kunasa yanayoendelea (USISAHAU HII NI MIKUTANO YA KATA) wanahangaika sana lakini ndiyo hivyo watu wamashawakubali sana chadema kwa kifupi hayo tu ila kuna mengi sana na kwa wale wanapenda kupiutano hiyo ingia kwenye facebook wall ya Ephata Nanyaro utazikuta chache alizoweza kupiga mikutano hiyo.
 
Na kila mikutano hii inapofanyika inakuwa pia na polisi wengi wanaokuja kwa siri kusikiliza chadema wataongea nini ili wawakamate na wengine hurekodi kisirisiri na mpaka mmoja juzi alikamatwa kata ya Elearai na pia mara nyingi nimekuwa nawaona maofisa wa TISS wasiopungua watano wale ninaowafahamu na wanakuwa na mionekano ya tofauti kwa jinsi walivyo siku zote ili kujifanya ni wanachadema ili waweze kunasa yanayoendelea (USISAHAU HII NI MIKUTANO YA KATA) wanahangaika sana lakini ndiyo hivyo watu wamashawakubali sana chadema kwa kifupi hayo tu ila kuna mengi sana na kwa wale wanapenda kupiutano hiyo ingia kwenye facebook wall ya Ephata Nanyaro utazikuta chache alizoweza kupiga mikutano hiyo.
vipi hatima yyake kwa hasi na ali kamatwa kwa kosa gani ?

Mkuu tuliambiwa kuwa mwaka huu CDM itafanya uchaguzi wa viongozi wa mashina ili kuimarisha chama ngazi ya chini kabisa - glass root vipi hili linatekelezwa huko mliko
 
vipi hatima yyake kwa hasi na ali kamatwa kwa kosa gani ?

Mkuu tuliambiwa kuwa mwaka huu CDM itafanya uchaguzi wa viongozi wa mashina ili kuimarisha chama ngazi ya chini kabisa - glass root vipi hili linatekelezwa huko mliko

Aliyekamatwa hakuwa wazi kama alikuwa ofisa usalama au alikuwa ni pandikizi tu na makamanda wa chadema walitaka kuiformat simu yake lakini mbunge G. Lema Aliwataka makamanda wamwachie na wasifute chochote ili ujumbe uwafikie kwa wale waliomtuma hata kama ni JK.

Matawi yanaendelea kufunguliwa kama kawaida na watu wana mwamko mkubwa na kuipokea chadema kwa matumaini makubwa ya hatima yao kimaendeleo.
 
View attachment 45052
View attachment 45053
Kimandolu 4.jpg
Hizo ni baadhi ya picha za mkutano wa chadema uliofanyika kata kimandolu....
 
Back
Top Bottom