nngu007
JF-Expert Member
- Aug 2, 2010
- 15,862
- 5,797
Chama cha Mapinduzi kimefanikiwa kuibwaga CHADEMA katika uchaguzi mdogo wa Udiwani uliofanyika katika Kata ya Bugarama wilayani Kahama mkoani Shinyanga.
Habari zilizopatikana zimesema, katika uchaguzi huo ulifanyika leo CCM imepata kura 1145
CHADEMA: 772 na TADEA: 156 wagombea wakiwa Nixon Igoko (CCM) Erasmus Francis (CHADEMA) na Clement Michael (TADEA) .
Pia habari zilizopatikana kutoka Kata ya Shinyanga mjini ambako pia uchaguzi mdogo wa Udiwani umefanyika, zimasema CCM imeshinda. Hata hivyo hatukuweza kupata mizania ya ushindi huo kwa kura.
---
Chanzo cha taarifa: Bashir-Nkoromo blog
Katibu wa Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM, Itikadi na Uenezi, Nape Nnauye na Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Sinyanga Hamis Mgeja wakishiriki kucheza ngoma ya Baswezi kwenye mkutano wa kampeni za udiwani kata ya Bugarama mkoani humo.
Madiwani wa Kata za Kahama wakiwa na mgombea Udiwani wa CCM, Kata ya Bugarama katika wilaya hiyo Nixon Ikoko wakati wa mkutano wa kufunga kampeni za udiwani katika kata hiyo, uliohutubiwa na Katibu wa Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM, Itikadi na Uenezi, Nape Nnauye.
Katibu wa Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM, Itikadi na Uenezi, Nape Nnauye akimsikiliza kwa makini Mbunge wa Msalala, Ezekiel Maige wakati akimuombea kura mgombea udiwani wa CCM Kata ya Bugarama, kwenye mkutano wa kufunga kampeni za CCM uliofanyika mji mdogo wa Bugarama.
Katibu wa Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM, Itikadi na Uenezi, Nape Nnauye akimnadi mgombea wa Udiwani kata ya Bugarama, Nixon Igogo kwenye mkutano wa kufunga kampeni za udiwani za CCM.
Katibu wa Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM, Itikadi na Uenezi, Nape Nnauye Mbunge wa Msalala, Ezekiel Maige wakiwa na watafiti wa madini kutoka kampuni ya Majordrilling, katika kijiji cha Kakola wilayani Kahama mkoani Shinyanga
Wazee wakifuatilia kwa makini hotuba ya Katibu wa Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM, Itikadi na Uenezi, Nape Nnauye alipohutubia mkutano wa kufunga kampeni za udiwani za CCM Kata ya Bugarama, Kahama mkoani Shinyanga.
Kina mama wakifuatilia kwa makini hotuba ya Katibu wa Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM, Itikadi na Uenezi, Nape Nnauye, Kata ya Bugarama
Mzee wa miaka 98, Nickson Toma akifuatilia kwa makini mkutano wa kampeni za udiwani Kata ya Bugarama mkoani Shinyanga uliohutubiwa na Katibu wa Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM, Itikadi na Uenezi, Nape Nnauye
Source: http://www.wavuti.com/#ixzz2AhP4louo